Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,931
Hujasema kuwa ni kodi ipi inayotakiwa kulipwa Tanzania ili iwe kigezo cha kumuwezesha mtu kupiga kura. Mimi naishi nje ya Tanzania, lakini nalipa kodi nchini Tanzania kila mwaka.Utapiga vipi kura wakati hulipi kodi TZ? Nyie mnaojiita WTZ mnaoishi nje ya nchi mnataka kupiga kura bila ya kuchangia kodi. Mnafanya kazi nje ya nchi, hamlipi kodi TZ; lakini mnataka mpewe haki kama WTZ wengine. Kama mnataka kupiga kura lipeni kodi ya kipato mnachoingiza.
Kwa mfano, raia wa USA analipa kodi ya nchi hata kama akifanya kazi nje ya nchi. Sasa kwanini nyinyi hamlipi kodi? Sisi tunaumia huku Bongo na tunalipa kodi; kwa sababu tunataka maendeleo ya Taifa letu. Naliomba Bunge lichukue hatua kali dhidi ya watu wanaoishi nje ya nchi wanaotaka kupiga kura bila ya kulipa kodi. Inaumiza sana kuona WTZ wanaoishi nje ya nchi hawalipi kodi; lakini wanapewa haki kama raia wengine ambao wanalipa kodi. Tunaomba Bunge lipitishe Muswaada kuhusu haki za wanaolipa kodi na wasiolipa kodi.
Kama hulipi kodi pia FISADI. Kwa hiyo hawa wanaojiita WTZ wanaoishi nje ya nchi ni MAFISADI pia.
Ninalipa kodi za viwanja na majengo yangu mbalimbali, pamoja na magari yangu ambayo yapo barabarani. Sasa utaniambia nini, kuwa silipi kodi? Ee bwana we, wacha mchezo!!