Napendekeza sasa ikiwezekana mdahalo uitishwe kati ya vijana waliohama kutoka CCM kuhamia CHADEMA na wale WALIOFUKUZWA kutoka CHADEMA wakahamia CCM.Kwa kutumia falsafa ya Mwalimu nyerere kwamba ili tuendelee tunahitaji Watu,Ardhi na siasa safi ni vyema sasa tukaamua kubadili mkondo wa siasa zetu kama vijana wa kizazi hiki na kufanya siasa za kistaarabu na kujenga taswira mpya ya siasa za mfumo wa vyama vingi hapa Tanzania.
Kamanda Ally Bananga na Alphonce Mawazo walitoka CCM na kuhamia CHADEMA na kujiunga na vuguvugu la mabadiliko huku Juliana Shonza na Mtela Mwampamba wakifukuzwa CHADEMA kwa usaliti na jaribio la kuhujumu vuguvugu la mabadiliko kisha wakajiunga na CCM(maadui wa Mabadiliko) na katika kuonyesha jinsi CCM walivyofilisika kisera na kiitikadi wakaamua kuwapokea na kuzunguka nao kwenye majukwaa kushambulia viongozi na wanachama wa CHADEMA na hasa kwenye mambo binafsi