tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 26,021
- 25,423
Mhadhiri mwandamizi mstaafu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) na gwiji wa sheria nchini, Profesa Issa Shivji (pichani), amesema ni muumini wa muundo wa Muungano wa serikali mbili tangu zamani.
Alisema hayo jana kwenye kipindi cha Nipashe, kinachorushwa kila siku asubuhi na Radio One Stereo.
Profesa Shivji alisema amekuwa muumini wa muundo wa serikali mbili tangu mwaka 1983 na kwamba, wanaosema amebadili msimamo wake ni waongo, kwani katika kipindi hicho walikuwa bado hawajazaliwa.
Alisema hakuna siku, ambayo aliwahi kusema wala kushauri uwapo wa muundo Muungano wa serikali tatu.
Wanaosema kuwa kuna chama kinachonisukuma na ambacho ninaegemea kwenye msimamo wao, kuhusu muundo wa serikali tatu hayo ni maoni yao binafsi, alisema Profesa Shivji.
Kauli ya Profesa Shivji inakuja, huku kukiwa na shutuma kutoka kwa watu mbalimbali, ambao wamekuwa wakimlaumu kuwa ni kigeugeu, kwani huko nyuma aliwahi kusema kwamba, Zanzibar ina haki ya kuwa na mamlaka kamili.
Profesa Shivji akizungumzia Tume wa Warioba, alisema kuwa hakuwahi kutoa maoni yake kwenye Tume hiyo, isipokuwa aliitwa katika hatua za awali ili kutoa maelezo na mwongozo wa masuala ya kuzingatiwa katika kutengeneza katiba. Machi 30, mwaka huu, Profesa Shivji akizungumza kwenye kongamano la wasomi wa vyuo vikuu, lililoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, alisema Katiba ya Zanzibar ndiyo sababu kubwa ya mgogoro ndani ya Muungano.
Alisema marekebisho ya 10 mwaka 2010 ya Katiba ya Zanzibar yaliyoitambua Zanzibar kuwani nchi yenye mamlaka na mipaka yake na kumpa mamlaka rais wa Zanzibar kugawa maeneo ya mkoa, wilaya, na kupora madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ndiyo sababu ya matatizo katika Muungano.
Alisema pia kwamba, marekebisho mengine yaliyofanyika mwaka 1993 katika katiba hiyo yaliipa Zanzibar mamlaka ya kuwa na bendera na wimbo wa Taifa na kupendekeza kwamba, njia bora ya kulinda Muungano wenye muundo wa serikali mbili, ni kuondoa marekebisho hayo katika Katiba ya Zanzibar.
Profesa Shivji ambaye alikuwa mzungumzaji mkuu, alifafanua kuwa wanaotaka serikali tatu hawajui historia ya Muungano na ni wanasiasa, ambao ni wavivu kusoma na hawataki kufanya uchambuzi kabla ya kuzungumzia jambo linalowafikia.
Tume ya Jaji Joseph Warioba ilipendekeza muundo wa serikali tatu kwa maelezo kuwa ndiyo utakaokuwa mwarobaini wa kero za Muungano.
Jumatatu wiki hii, wajumbe wawili wa Bunge Maalumu la Katiba, Tundu Lissu na Jussa Isamail Ladhu waliitisha mkutano wa waandishi wa habari mjini Dodoma na kumtuhumu Prof. Shivji kuwa anasaliti msimamo na machapisho yake aliyoyasimamia kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita kwa lengo la kuifurahisha serikali na CCM. Lissu na Jussa walisema wanamshangaa Prof. Shivji kwa matamshi yake na kutoamini kama aliyoyasema ilikuwa ni kwa akili yake au alishinikizwa.
Lissu alisema msimamo wa sasa wa Profesa Shivji kwamba Muungano wa serikali mbili unapaswa kudumishwa, umeshtua kwa kuwa unapingana na maandiko yake aliyochapisha kwenye vitabu mbalimbali yakipinga muundo wa serikali mbili.
Lissu alisema mwaka 1990 Prof. Shivji alitoa mhadhara wa kiprofesa uliosababisha apewe u-profesa akizungumzia misingi ya kisheria na uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema kuwa ili makubaliano ya Muungano yaweze kupata uhalali, ni lazima yatungiwe sheria ya kuridhia makubaliano hayo na mabunge ya nchi washirika.
Jussa alisema machapisho ya Profesa Shivji ndiyo yaliyochangia kuamsha vuguvugu la Wazanzibari kudai haki kwenye muundo wa Muungano, hivyo anashangazwa na kitendo cha Profesa Shivji kuyageuka machapisho yake na kutangaza hadharani kuunga mkono muundo ambao alikuwa akiukosoa kwa miaka mingi.
Alisema kitendo hicho kimemkwaza kwa kuwa yeye ni miongoni mwa Wazanzibar waliompatia ushirikiano mkubwa wakati akifanya utafiti wa masuala ya Muungano Visiwani Zanzibar.
CHANZO: NIPASHE
:yield:
Alisema hayo jana kwenye kipindi cha Nipashe, kinachorushwa kila siku asubuhi na Radio One Stereo.
Profesa Shivji alisema amekuwa muumini wa muundo wa serikali mbili tangu mwaka 1983 na kwamba, wanaosema amebadili msimamo wake ni waongo, kwani katika kipindi hicho walikuwa bado hawajazaliwa.
Alisema hakuna siku, ambayo aliwahi kusema wala kushauri uwapo wa muundo Muungano wa serikali tatu.
Wanaosema kuwa kuna chama kinachonisukuma na ambacho ninaegemea kwenye msimamo wao, kuhusu muundo wa serikali tatu hayo ni maoni yao binafsi, alisema Profesa Shivji.
Kauli ya Profesa Shivji inakuja, huku kukiwa na shutuma kutoka kwa watu mbalimbali, ambao wamekuwa wakimlaumu kuwa ni kigeugeu, kwani huko nyuma aliwahi kusema kwamba, Zanzibar ina haki ya kuwa na mamlaka kamili.
Profesa Shivji akizungumzia Tume wa Warioba, alisema kuwa hakuwahi kutoa maoni yake kwenye Tume hiyo, isipokuwa aliitwa katika hatua za awali ili kutoa maelezo na mwongozo wa masuala ya kuzingatiwa katika kutengeneza katiba. Machi 30, mwaka huu, Profesa Shivji akizungumza kwenye kongamano la wasomi wa vyuo vikuu, lililoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, alisema Katiba ya Zanzibar ndiyo sababu kubwa ya mgogoro ndani ya Muungano.
Alisema marekebisho ya 10 mwaka 2010 ya Katiba ya Zanzibar yaliyoitambua Zanzibar kuwani nchi yenye mamlaka na mipaka yake na kumpa mamlaka rais wa Zanzibar kugawa maeneo ya mkoa, wilaya, na kupora madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ndiyo sababu ya matatizo katika Muungano.
Alisema pia kwamba, marekebisho mengine yaliyofanyika mwaka 1993 katika katiba hiyo yaliipa Zanzibar mamlaka ya kuwa na bendera na wimbo wa Taifa na kupendekeza kwamba, njia bora ya kulinda Muungano wenye muundo wa serikali mbili, ni kuondoa marekebisho hayo katika Katiba ya Zanzibar.
Profesa Shivji ambaye alikuwa mzungumzaji mkuu, alifafanua kuwa wanaotaka serikali tatu hawajui historia ya Muungano na ni wanasiasa, ambao ni wavivu kusoma na hawataki kufanya uchambuzi kabla ya kuzungumzia jambo linalowafikia.
Tume ya Jaji Joseph Warioba ilipendekeza muundo wa serikali tatu kwa maelezo kuwa ndiyo utakaokuwa mwarobaini wa kero za Muungano.
Jumatatu wiki hii, wajumbe wawili wa Bunge Maalumu la Katiba, Tundu Lissu na Jussa Isamail Ladhu waliitisha mkutano wa waandishi wa habari mjini Dodoma na kumtuhumu Prof. Shivji kuwa anasaliti msimamo na machapisho yake aliyoyasimamia kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita kwa lengo la kuifurahisha serikali na CCM. Lissu na Jussa walisema wanamshangaa Prof. Shivji kwa matamshi yake na kutoamini kama aliyoyasema ilikuwa ni kwa akili yake au alishinikizwa.
Lissu alisema msimamo wa sasa wa Profesa Shivji kwamba Muungano wa serikali mbili unapaswa kudumishwa, umeshtua kwa kuwa unapingana na maandiko yake aliyochapisha kwenye vitabu mbalimbali yakipinga muundo wa serikali mbili.
Lissu alisema mwaka 1990 Prof. Shivji alitoa mhadhara wa kiprofesa uliosababisha apewe u-profesa akizungumzia misingi ya kisheria na uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema kuwa ili makubaliano ya Muungano yaweze kupata uhalali, ni lazima yatungiwe sheria ya kuridhia makubaliano hayo na mabunge ya nchi washirika.
Jussa alisema machapisho ya Profesa Shivji ndiyo yaliyochangia kuamsha vuguvugu la Wazanzibari kudai haki kwenye muundo wa Muungano, hivyo anashangazwa na kitendo cha Profesa Shivji kuyageuka machapisho yake na kutangaza hadharani kuunga mkono muundo ambao alikuwa akiukosoa kwa miaka mingi.
Alisema kitendo hicho kimemkwaza kwa kuwa yeye ni miongoni mwa Wazanzibar waliompatia ushirikiano mkubwa wakati akifanya utafiti wa masuala ya Muungano Visiwani Zanzibar.
CHANZO: NIPASHE
:yield: