Duma R. SIFFI
Member
- Nov 18, 2011
- 7
- 0
Sikuamini machoni na masikioni baada ya kuhudhuria semina iliyohusisha mawakala kutoka NHC na Wafanyakazi wa St. Johns University of Tanzania a.k.a Mazengo compus. Kilichoniacha hoi ni kwamba wanatushauri tukanunue nyumba za Medeli residential apartment na bei ya ofa kama alivyosema mtoa mada ni Milioni 111 na point kazaa yaani Tsh. 111 milion. Swali ni je, 1. Kuna mfanyakazi gani wa St. John na mtanzania kwa ujumla anayeweza kununua hizo nyumba? 2. Atakuwa analipwa kiasi gani kwa mwezi? Nashindwa kuamini kuwa kwa hela za kihalali kabisa kama unaweza kuwa na hela kiasi hicho. Nadhani ipo haja ya kuishauri serikali yetu mara mbimbili