Shinyanga: Ajenti wa Basi la Kisibo akanyagwa na Basi hilo na kufariki hapo hapo wakati akirukia kwenye Basi hilo

The Humble Dreamer

JF-Expert Member
Oct 12, 2015
7,442
10,233
Mwanaume aliyetambulika kwa jina moja la Athumani amefariki dunia mara baada ya kukanyagwa na gari hilo katika stendi kuu ya mabasi ya Shinyanga, mwili wake umepelekwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga.

Taarifa zinasema kua Basi hilo linalofanya safari zake kati ya Mwanza na Dar es Salaam lilimkanyaga Ajenti Athumani wakati akirukia kwenye Basi hilo na kisha kuangukia uvunguni mwa Basi na kukanyagwa na kufariki dunia hapo hapo.

20200327_124145_rmscr-1.jpg


Polisi wako pembeni wanaangalia tu.

Pia wanaoonekani pichani wakimsaidia marehemu ni wananchi wakawaida sana, mashaka yangu ni je, wana uelewa wa kutosha juu ya maambukizi ya magonjwa ama virusi pindi ikitokea ajali ilihali wenye mavazi mazuri wamesimama wakitazama kama viongozi waelekezi tu?.....

Ushauri: Hii tabia ya kurukia gari au kushuka kwenye gari wakati gari hilo likiwa kwenye motion ni hatari sana. Watu wengi hufanya hivyo ili kuokoa muda au kuonyesha wepesi ila fahamu unahatarisha uhai wako. Ni vema usubiri gari lisimame ushuke.
 
Huyu jamaa baada ya kukanyagwa na kisbo, mabasi mengine mawili yamempitia juu hali iliyopelekea kusagika kabisa.

Haya mabasi yalikuwa yanafukuzana kutoka getini. Amekufa kifo kibaya sana.

RIP Athuman
Inasemekana gari iliyomkanyaga ni basi la Kisbo tena kwa matairi ya nyuma, sasa wewe na hayo mabasi mengine mawili yaliyompitia juu sijui taarifa yako umeitoa wapi, una maanisha hayo mabasi yalikuwa yamekaribiana kiasi hicho mpaka madereva wa mabasi ya nyuma wasimuone marehemu?!

Ngumu kumeza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku zote nasema..
Shortcut is Wrongcut
Hua najiuliza watu hua wanawahi nini huko (bodaboda?) Ingemdhuru nini kusubiri lisimame...

Hapo ukute mfukoni kabebelea sanitizer ili kujikinga na corona hafu harakaharaka ndio zimemmaliza
Ila mkuu kifo hakina mazingira rafiki sana!
 
Haya mambo kwao ni ya kawaida sana (Japo ni risky kubwa sana), ila kifo kikifika kimefika tu. Tonge la ugali ulilolila kwa miaka na miaka linaweza kukukaba na kukuua,

R.I.P
Yes kifo kikifika kimefika..lakin lazima kila mmoja achukue tahadhari kwa njia zote!

Kazoea kufanya hivyo ila ni risk ya maisha yake binafsi!
 
Kwa magari ya mikoani kwenye vituo vya njiani huwa wanashusha hivyo hivyo hata abiria hali hii inaweza kusababisha madhara makubwa sana kwa abiria kama ilivyotokea kwa huyo konda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Exactly..imekua ni kama tabia miaka mingi!

Hua wanatumia physics fln pale ndani ya sekunde chache rakini ni hatar kwa uhai..Wakati mwingine tunajiwaishia wenyewe kukitafuta kifo
 
Back
Top Bottom