Shida tunazozipata wapangaji hazivumiliki

Shida tunazozipata wapangaji hazivumiliki

Ndo Mimi Mkuu tena huyu Mpangaji wa ni kero kwa wenzake anaomba mpaka kachumbari.
Hunitendei haki kuanika madhaifu yangu katika hadhara hii landlord tambua kuwa hiyo nyumba ni ya urithi kwahyo soon mtagawana na wewe utakuwa mpangaji kama mimi.
 
Kama kuna watu wanapata shida sana hapa mjini basi ni sisi wapangaji hususani sisi wa kipato cha chini.

Hii nyumba niliyopanga ina visanga sijawahi kuona. Kisanga cha kwanza mvua ikinyesha kidogo tu godoro lazima lielee si bondeni ila maji yanaingia mithili ya mtu aliyeko nje.

Kwahiyo kipindi hiki cha masika nimekuwa kama mtu mwenye watoto wanaokojoa kitandani kila jua linapowaka lazima nianike godoro nje.

Nimekaa miezi miwili ila naona kama nimekaa mwaka mzima kwa tabu ninayoipata. Hivi vyumba vya elfu 30,000 ni pasua kichwa sana hapa mjini.

Upande wa pili wa kupata totozi kipindi hiki nimekuwa mpole maana naogopa kupata aibu ya karne pale nitakapomleta mtoto gheto na mvua ikanyesha.

Wito kwa wenye nyumba mnatutesa sana wapangaji kutupangishia vyumba vinavyoingiza maji pindi mvua inyeshapo ili hali mnajua

Acha niishie hapa maana nina hasira sana na huyu landlord.
chai kama chai nyingine[emoji23]
 
Jenga yako/panga kwenye Bei kubwa/ endelea kuvumilia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom