Shida tunazozipata wapangaji hazivumiliki

Shida tunazozipata wapangaji hazivumiliki

Gluk

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2017
Posts
1,859
Reaction score
3,024
Kama kuna watu wanapata shida sana hapa mjini basi ni sisi wapangaji hususani sisi wa kipato cha chini.

Hii nyumba niliyopanga ina visanga sijawahi kuona. Kisanga cha kwanza mvua ikinyesha kidogo tu godoro lazima lielee si bondeni ila maji yanaingia mithili ya mtu aliyeko nje.

Kwahiyo kipindi hiki cha masika nimekuwa kama mtu mwenye watoto wanaokojoa kitandani kila jua linapowaka lazima nianike godoro nje.

Nimekaa miezi miwili ila naona kama nimekaa mwaka mzima kwa tabu ninayoipata. Hivi vyumba vya elfu 30,000 ni pasua kichwa sana hapa mjini.

Upande wa pili wa kupata totozi kipindi hiki nimekuwa mpole maana naogopa kupata aibu ya karne pale nitakapomleta mtoto gheto na mvua ikanyesha.

Wito kwa wenye nyumba mnatutesa sana wapangaji kutupangishia vyumba vinavyoingiza maji pindi mvua inyeshapo ili hali mnajua

Acha niishie hapa maana nina hasira sana na huyu landlord.
 
Pole mkuu.
Umenikumbusha hili shairi la muamerika Langstone Hughes.. Ballad of the landlord

Landlord, landlord,
My roof has sprung a leak.
Don't you 'member I told you about it
Way last week?

Landlord, landlord,
These steps is broken down.
When you come up yourself
It's a wonder you don't fall down.

Ten Bucks you say I owe you?
Ten Bucks you say is due?
Well, that's Ten Bucks more'n I'l pay you
Till you fix this house up new.

What? You gonna get eviction orders?
You gonna cut off my heat?
You gonna take my furniture and
Throw it in the street?

Um-huh! You talking high and mighty.
Talk on-till you get through.
You ain't gonna be able to say a word
If I land my fist on you.

Police! Police!
Come and get this man!
He's trying to ruin the government
And overturn the land!

Copper's whistle!
Patrol bell!
Arrest.
Precinct Station.
Iron cell.
Headlines in press:
MAN THREATENS LANDLORD
TENANT HELD NO BAIL
JUDGE GIVES NEGRO 90 DAYS IN COUNTY JAIL!
 
Hili shairi limenifanya nicheke sana badala ya kusikitika.
Hahaa
Lipo na uhalisia japo liliongelea landlords wa Kiamerika waliokuwa wakiibia tenants wao bila kufanya marekebisho miaka hiyo ya zamani.
Japo metaphorically ilikuwa ni serikali ya America ilivyoakuwa haijali jamii ya watu wa chini hasa weusi.
Usijali mkuu haya ni maisha tu duniani kote yapo, ni kupambana tu kujikwamua.
 
Hahaa
Lipo na uhalisia japo liliongelea landlords wa Kiamerika waliokuwa wakiibia tenants wao bila kufanya marekebisho miaka hiyo ya zamani.
Japo metaphorically ilikuwa ni serikali ya America ilivyoakuwa haijali jamii ya watu wa chini hasa weusi.
Usijali mkuu haya ni maisha tu duniani kote yapo, ni kupambana tu kujikwamua.
Asante mkuu kwa kunipa moyo acha nipambane ili kuepuka msoto huu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom