Shibuda: CCM ni chama cha maskini na wanyonge

Shibuda: CCM ni chama cha maskini na wanyonge

Huyu mbunge ipo siku atasaliti ata familia yake make aeleweki.
 
Wakuu hacheni unafiki na maigizo ktk mambo makini, hivi nani anaamini kuwa ccm ya leo inawatetea wanyonge? Tukianza kuelezana ukweli kwenye hili tutakimbiana.
 
Shibuda yuko sahihi kwani kwenye kutetea maslahi ya Watanzania hatuna kudi kuweka itikadi za kichama.
 
Huyu mzee hapendi unafiki, hilo tatizo lake...hupenda kuusema ukweli hata ukiwa mchungu kiasi gani
 
tutaenda naye hivyohivyo tu kama gari bovu tukiona hawezi kutuathiri tutafika naye 2015 ila asahau ubunge kupitia CHADEMA labda safari hii aende NCCR au arudi kwaoCCM. CHADEMA sio size yake, tulifanya makosa kumkaribisha ila hatuna jinsi hebu twende naye hivyo hivyo kiubishi, ubishi. Tutafika!!

As great thinker, kosa lake liko wapi hapo??? Mara ngapi wamesimama wabunge wa upinzani kwenye majukwaa na bungeni wakiisifu serikali ya ccm kwa utendaji bora??? Rejea hotuba ya mbowe, joseph selasini wakiwa kilimanjaro mbele ya rais kikwete wakati anazindua barabara zilizojengwa na ccm mkoani humo..juzi kati hapa bungeni wabunge wa chadema wameipongeza sana serikali ya ccm hadi zitto akatoa karipio... Au tatizo lako ni shibuda kama shibuda????
 
Kuna watu wamesoma heading tu na kuanza kutoa comment wakati ukimsoma kwa makini amewapiga dongo CCM kiaina kwa kutumia sanaa ya lugha
 
mkuu, wala usiogope; shibuda kwa mikono yake miwili alichukua kamba na kujininginiza mwenyewe, kwa sasa ana rusharusha miguu tu; chadema hatuna haja ya kupoteza mda wetu kuhangaika na mtu kama shibuda; tumewaachia wapiga kura wake wamsurubu wenyewe ifikapo 2015.

shibuda atakuwa hajui hili kweli?labda magamba wamwokoe 2015 kwa kutumia polisi na tume ya uchaguzi kumtangaza mbunge.cdm waanze kutayarisha mgombea mwingine.kila nikijaribu kumsoma kutoka kila kona nashindwa kumpata kabisa.wanajf mnampata nyie.?
 
Akichangia ktk hotuba ya wizara ya ardhi, mh John Shibuda, mbunge wa maswa kupitia CHADEMA amekisifia CCM kuwa ni chama cha maskini na wanyonge na ambacho kimelinda maslahi ya watanzania tangu uhuru.

Shibuda amemtaka waziri wa ardhi ahakikishe anatekeleza sera ya CCM ya kueatetea wanyonge kwa kuwaondoa wafanyabiashara wote wanaoishi kwenye nyumba za serikali maarufu kama quoters!!!!

Amewaita wafanyabiashara hao wanaoishi kwenye nyumba za serikali/Quoters kuwa ni wahujumu, wanyonyaji na hivyo waziri ahakikishe wanaachia nyumba hizo ili zitumiwe na watumishi wa umma ambao ni maskini.

Aidha ameitaka serikali iwauzie nyumba wafanyakazi waliokaa mda mrefu kuanzia miaka 20 kwani hawajajenga kwa kupenda bali ni kipato duni.

Vipi mtampa nafasi ya kugombea huyu kada wenu ambae uku tunamtumia kuongeza ruzuku yetu.
 
Tokea umeajiriwa na lumumba tarehe 20/4/2013 Naona unataka uwe mfanyakazi bora hata uwapite wakina chama Ritz ZeMarcopolo
Mkuu Precise pangolin
Hivi vijana wa mtaa wa Togo mna matatizo gani? Inakuwaje mnaogopa ukweli? kichekesho chenyewe ni pale mnaopoukimbia mti uliojaa matunda ya ukweli na kujificha chini ya kivuli chake.

Chama
Gongo la mboto DSM
CC Ritz
 
Last edited by a moderator:
CCM imeishachakachuliwa, Jembe na Nyumba zinatakiwa kuondolewa kweye bendera ya CCM!
 
Shibuda kayaona ya CDM amefananisha na ya CCM kafikia conclusion, nyinyi mlioko nje na kutokwa na povu humu jf ndo mnashindwa kumuelewa.
 
Hivi GOGO LA UDI wakimfukuza Ruzuku Itapungua Au Kuunda Kambi Rasmi Ya Upinzani Kutapwaya.? Maana Shibuda Na Zitto Kwa Mujibu Wa Mashabiki Wa Chadema Watu Hawa Ni Wasaliti Kwao.......lakini Kutokana Na Ubunge Inakuwa Ngumu Kuwatoa Maana Majimbo Yao Juhudi Zao Binafsi Ndizo Zilizowapa Ubunge Na Si Chama!
Ila angekuwa Mbunge Mwingine Ambako Kuna Uhakika Wa Ushindi Wangeshatimuliwa Zamani Sana. Mark The Words!
 
shibuda . Amekomaa kisiasa. Hana siasa za majungu kama kina Mbowe.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom