Sheria ya Uchaguzi ni mbovu! Kuendelea kuitumia sio Ujinga? Kuwabebesha masikini gharama za Uchaguzi sio Dhambi?

Sasa tujiulize kama anafanya haya wazi wazi, nyuma ya pazi atakuwa anatupiga kiasi gani ukizingatia hajali na wala hana uchungu

HUYU BWANA ANA STRATEGY YAKE YA KUTUIBIA KAMA NCHI NA NDIO MAANA AMEAMUA KUCENTRALIZE REVENUE COLLECTION ZOTE ZA SERIKALI NA KUWEKA WATU WAKE KWENYE STRATEGIC POSITIONS KAMA PALE BENKI KUU NA HAZINA!! FEDHA IKIWA IMEKUSANYWA MAHALA PAMOJA NI RAHISI KUPIGA!!
 
Wewe Salary Slip unaonekana unaumia sana kuhusu hii serikali
Yaani sijui umefanywa nini kila siku majungu majungu na chuki.
Wewe kama umeichukia ni wewe usije kuleta kilasiku umbea. Hao wabunge wanahama kwa kuwa CHEDEMA kuna shida na washajua kuwa chama kinakufa 2020 sasa utawalisha wewe.
Wenzio siasa ni kazi na kwa kuwa ni kazi basi huwezi kukaa mahali ambapo unaona panakoelekea ni kufa. Ni sawa na wachezaji wa mpira kuhama club au wafanyakazi kuacha kazi shirika fulani na kwenda shirika lingine.
 
Wewe Salary Slip unaonekana unaumia sana kuhusu hii serikali
Yaani sijui umefanywa nini kila siku majungu majungu na chuki.
Wewe kama umeichukia ni wewe usije kuleta kilasiku umbea. Hao wabunge wanahama kwa kuwa CHEDEMA kuna shida na washajua kuwa chama kinakufa 2020 sasa utawalisha wewe.
Wenzio siasa ni kazi na kwa kuwa ni kazi basi huwezi kukaa mahali ambapo unaona panakoelekea ni kufa. Ni sawa na wachezaji wa mpira kuhama club au wafanyakazi kuacha kazi shirika fulani na kwenda shirika lingine.
Pathetic creature! !
 
Hili ndio swali ambalo kila mtu mwenye akili timamu anapaswa kujiuliza maana teyari ameshatuthibitishia kuwa hana huruma wala uchungu na kodi zetu.

Sasa tujiulize kama anafanya haya wazi wazi, nyuma ya pazi atakuwa anatupiga kiasi gani ukizingatia hajali na wala hana uchungu?

Wabongo mkija kushituka, jamaa teyari bilionea.
Kama anaweza kufanya uchafu huu hadharani, then huko, huko kuliko na mtoto wa dada, huko kwa msajili wa hazina, huko BOT kuna nini???????????????????????????????????????
 
Habari wana JF,
Naomba kueleweshwa kidogo na tujadili kwa pamoja jambo hili.

Kumekuwa na hamahama ya baadhi ya watu waliopewa dhamana na wananchi, hasahasa madiwani na wabuge kuhama chama fulani na kuhamia chama kingine, na kibwagizo cha wimbo huu wa kuhamahama ni kuhunga mkono juhudi za kiongozi.
Nimekuwa nikijiuliza maswali yafuatayo:

1: Je, bajeti ya kuendeshea kampeni na kusimamia hizo chaguzi za marudio ilikuwepo au hizo fedha zinatoka wapi?

2: Je bunge lilipitisha hizo fedha?

3: Gharama ya uchaguzi wa i) wabunge, ii)madiwani ni shilingi ngapi kwa kia mmoja?

4: Fedha ambazo zimeshatumika kwenye hizi chaguzi zilizofanyika kwutokana na watu kuhama vyama ni kiasi gani mpaka sasa?

5: Je kama chaguzi hizo zisizo za lazima hazikufanyika/hazikutokea, je fedha hizo zisinge weza kufanya jambo linguine lenye tija kwa nchi na wananchi kwa ujumla kama kujenga shule, hospitali, maji n.k.?

Naomba niishia hapa kwa sasa

– KARIBUNI KUCHANGIA NA KUTOA MAWAZO YENU- .
 
Mbunge au Diwani aliyeachia nafasi hiyo kwa kujiuzulu au kufariki basi tusifanye uchaguzi mdogo, tumpitishe mshindi wa pili kwenye uchaguzi mkuu uliopita kushika wadhifa huo.
Hi itasaidia sana kuokoa pesa zinazotumika kufanyia chaguzi ndogo.
TANZANIA NI YETU SOTE.
 
Nakubaliana kabisa kwamba demokrasia ni gharama lakini gharama nyingine zinaweza kuepukika. Kama tumefanikiwa kupunguza gharama kwa kudhibiti safari za nje hili la kupunguza gharama za demokrasia hata kwa kurekebisha sheria tu linatushindaje?!......niishie hapo tafadhali!
 
MWANASIASA mkongwe, Ibrahim Kaduma, ameibuka na kutoa kauli nzito kuhusu wabunge wanaojiengua upinzani na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Amekishauri chama hicho kuwachunguza watu hao kwa miaka miwili hadi mitatu kabla ya kuwapa vyeo au kuruhusu kugombea nafasi yoyote.

Sambamba na hilo, ameshauri kufanyika marekebisho ya Katiba na kuruhusu mgombea binafsi na inapotokea mtu anahama chama, abaki na cheo chake ili kuepusha gharama kubwa za uchaguzi mdogo unaofanyika mara kwa mara.
Mwanasiasa huyo aliyasema hayo juzi wakati wa mjadala wa hali ya kisiasa, uchumi na maendeleo ya Tanzania, uliojumuisha wadau mbalimbali wa vyama vya wafanyakazi wa nchi mbalimbali duniani, ulioandaliwa na shirika la kimataifa la Ujerumani (FES).

Katika mjadala huo, miongoni mwa waliohudhuria ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Hamphrey Polepole, na wabunge kutoka Bunge la Uingereza.

Kaduma ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya awamu ya kwanza, chini ya Mwalimu Julius Nyerere, alisema wanaokwenda CCM si wote wanajua falsafa ya chama hicho bali wanakwenda kuganga njaa.

“Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la madiwani na wabunge kuhamia CCM. kwa maoni yangu sioni kama wanahamia kwa vile wanajua na kuipenda falsafa ya CCM bali kwenda kutafuta maslahi na vyeo,” alisema na kuongeza:

“Sijaona sababu za msingi za kuhama kwao, nawaona kama waganga njaa na si kukipenda chama. Nashauri turudi kwenye utaratibu wa enzi za Mwalimu Julius Nyerere ambako unapokuwa mwanachama kabla ya kupewa cheo, unapewa miaka miwili au mitatu ya kuchunguzwa.”

Kwa mujibu wa Kaduma, si sawa mtu kuhamia CCM na siku inayofuata anapewa cheo au anateuliwa kugombea nafasi aliyokuwa nayo kwa tiketi ya chama hicho bila kuulizwa kama anaijua falsafa ya chama na ni mhubiri wa falsafa hiyo.
“Hatuko kwenye kisiwa, wenzetu Ujerumani walishaachana na hili la mtu akihama wanarejea kwenye uchaguzi mdogo. Kwao akihama chama anaendelea na ubunge wake huku akiwakilisha wananchi. Kwa nini tusiige kutoka huko,” alisema Kaduma.

Pia alisema suala la gharama za uchaguzi mdogo ni mzigo kwa Watanzania na ili kuepukana na jambo hilo, ni kuruhusu mgombea binafsi ambaye ameamua kutokukubaliana na falsafa za chama chake lakini bado anaweza kuendelea kuwawakilisha wananchi.

“Hakuna ubishi kuwa gharama za uchaguzi ni mzigo kubwa kwa nchi na unabebwa na Watanzania wote. Ifike mahali tulibadili hili kwa kuepuka uchaguzi mdogo, labda iwe kwa lazima sana na suluhisho ni mgombea binafsi,” alisisitiza
Hapa Kaduma amesema kweli,
Bandiko langu hili linasadifu
Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law!, Kuendelea Kuitumia ni Ujinga?, Kuwabebesha Masikini Gharama za Uchaguzi ni Dhambi!. - JamiiForums
P
 
Back
Top Bottom