Sheria ya Manunuzi yaua ‘upigaji dili’

Sheria ya Manunuzi yaua ‘upigaji dili’

Hata hivyo kwa hii sheria itahitaji kwa kila manunuzi wawe na cash money.
Maana unafuu serikali iliyokua ikiupata ni pale supplies walipokua wanatumia pesa zao kufanya manunuzi kisha serikali inawalipa kwa installment.
Uko sahihi vinginevyo riba ya kuchelewesha malipo iongezwe kulingana na soko
 
Huu mswada haujaeleweka, mfno wanaposema ofc ya summa itanunua kiwandani, au kwa


mwakilishi Wa Kampuni
au kwa muuzaji Wa jumla
Wanasahau Kuwa wauzaji Wa jumla hawapendi kufanya kazi na serikali kuepuka usumbufu Wa kudai, na hawako tayari kuijopesha serikali, na hawako tayari kuomba tender za hizo taasisi.na sio ofc zote za umma mahali zilipo kuna wauzaji Wa jumla au mwakilishi Wa kampuni, mfn ofc ya umma iko mtwara na inataka computer 2 , je muuzaji Wa jumla au mwakilishi anatoka wapi hapo mtwara ? hii sheria inamapungufu makubwa sana
labda itabidi aende dasalamu kununua,au azifuate chaina kiwandani
 
Ukiona sehemu kuna maneno mengi jua hakuna cash. Hakuna biashara ngumu na presha Kama kufanya biashara na serikali, rafiki zangu wawili walishajinyonga kwa sababu ya msongo wa mawazo. Serikali haina muda maalumu na sahihi wa kulipa, tena usilogwe ukakopa benki halafu uka supply serikalini. Utakufa na presha.hata hao wanao pandisha bei Mara kumi mm naona ni sawa kutokana na mateso wanayoyapata.
 
Uko sahihi kabisa hapa iko shallow sana na imejikita kwenye service Zaidi mfano ujenzi wa barabara kama bei ya soko inataka km ya lami ijengwe kwa milioni 800 akaja mzabuni akatenda kwa milioni 600 sasa huo ubora utapatikanaje? au huyo muuzaji wa jumla au kiwanda vinauhusiana vipi na ujenzi wa barabara?

Soma vizuri hayo mapendekezo; gharama halisi kwa ubora mzuri. Lakini pia ktk bajeti ya Mh. Mipango, kila wizara au taasisi ya serikali haitaruhusiwa kufanya biashara na mzabuni yeyote kwanza na kisha kupeleka madai serikalini. Kila wizara/taasisi ya umma itatakiwa kupeleka bajeti yake kwa serikali na fedha zitakuwa zinalipwa on monthly basis kwa bajeti yao iliyopelekwa serikalini.
Dharura na matumizi ya namna hiyo yatapelekwa serikalini as they happen. Hapa accountability itahusika Sana as kila jambo litakaloombewa pesa litatakiwa kutolewa maelezo na kuonyeshwa ukamilifu wake.
 
Hapo kuuziwa bei ya soko lazima cash ihusike. Pesa za umma zitoke mpaka upeleke invoice ya huduma. Malipo ni baada ya wiki mpaka mwezi. Mtaji unalala
 
hata itungwe sheria mpya ya manunuzi bila ya sheria mama ya nchi(katiba) kurekebishwa watu wataendelea kupiga dili tu sheria ya manunuzi iliyopo ni nzuri vipengele vichache ndo vinahitaji marekebisho. Swali la kujiuliza ni kina nani wanahusika na wizi kwenye manunuzi jibu ni wakuu wa idara, mawaziri, na makatibu wakuu pamoja na raisi ndo wahusika wakuu bila kuwa na katiba yenye kuwabana viongozi wa umma hata itungwe sheria mpaya kutoka mbinguni wataendelea kuiba tu mikataba mingi ni ya siri na huko ndo wizi unafanyika kirahisi katiba mpya ndo dawa ya kila kitu itatupunguzia kero nyingi, kilio chetu watanzania kiwe katiba mpya ikipatikana kutakua na uwoga wa uongozi wa umma.
Hapo katiba ya sasa ina mpungufu yapi kuhusu sheria ya manunuzi ya sasa.
 
Katika kukidhi haja ya kuondoa malalamiko ya sheria iliyopo kutumika kuibia nchi, marekebisho hayo yamesisitiza bei za huduma na bidhaa zitakazotolewa ziwe za soko, ununuzi ufanyike moja kwa moja kiwandani badala ya kupitia kwa mtu wa kati na mkataba wa manunuzi, lazima usainiwe mbele ya mashuhuda.


Hapa pana shida kidogo mbona kama aya hizi zinapingana au mimi ndie niliyeshindwa kuelewa ,naona watu wa kati juu wanakatazwa huku chini wanakubaliwa, which is which?

(Aidha, ili kupata bei iliyo chini ya soko bila kuathiri ubora wa bidhaa au huduma, ofisi husika kwa nia ya kupata thamani ya fedha na ubora wa juu, imetakiwa kufanya ununuzi wa bidhaa na huduma mahususi moja kwa moja kutoka kwa mtengenezaji, au kiwandani, mwakilishi wa mtengenezaji au wa kiwanda, muuzaji wa jumla au mtoa huduma.)
 
  • Thanks
Reactions: MJJ
Madalali watakufa kifo cha kawaida kabisa.
Laiti kama jambo hili la kunyonga madalali lingeshuka chini hadi kwa wapangaji wa nyumba.


Aisee umenena cha maanana kweli kabisa, unakosa kupanga chumba sababu huna hela ya dalali tena anakupangia sio maelewano
 
Hii in hawamu ya tano ya hapa kazi tu hacheni kuishi kwa mazoea tumpe muda tuone utekelezaji watu tulisha kalili madilidili sasa yamekuwa dirisha kwanza tupongeze walau hii hatua ya kuthubutu mambo mengine yanarekebika,walau tunaona kuwa kuna kitu Raisi anataka aifanyie hii nchi ili isonge mbele tusimkate maini.
 
Hapo katiba ya sasa ina mpungufu yapi kuhusu sheria ya manunuzi ya sasa.
nadhani hujanielewa katiba ndio sheria mama ss kama katiba iliyopo inaruhusu viongozi wa umma kufanya mambo wanavyopenda hata utunge sheria ngumu kiasi gani ya manunuzi watazidi kuiba tu, lazima iwepo katiba inayowabana viongozi wa umma kwa mfano kuwakataza kufanya biashara wawapo madarakani la sihivyo unakuta kiongozi anahusika kwenye mchakato wa manunuzi wakati yeye mwenyewe ana uhusiano na kampuni zinazogombea tenda husika huoi hapo kuna mianya ya wizi, mfano mzuri ni mitambo ya dowans na richmond ilivyonunuliw haina haja kuelezea raisi alivyoingilia
 
Soma vizuri hayo mapendekezo; gharama halisi kwa ubora mzuri. Lakini pia ktk bajeti ya Mh. Mipango, kila wizara au taasisi ya serikali haitaruhusiwa kufanya biashara na mzabuni yeyote kwanza na kisha kupeleka madai serikalini. Kila wizara/taasisi ya umma itatakiwa kupeleka bajeti yake kwa serikali na fedha zitakuwa zinalipwa on monthly basis kwa bajeti yao iliyopelekwa serikalini.
Dharura na matumizi ya namna hiyo yatapelekwa serikalini as they happen. Hapa accountability itahusika Sana as kila jambo litakaloombewa pesa litatakiwa kutolewa maelezo na kuonyeshwa ukamilifu wake.

Unaijua serikali? Au unaisikia? Mwezi wa pili Tanroads wameaward kazi kulingana na budget waliyopeleka na karibuni wanaambiwa wawapunguzie wazabuni sehemu ya kazi kwa vile pesa hazijapatikana. Hela za zabuni za miradi ya "Works" huwa zinapatikana kulingana na makusanyo kasoro donor funded projects hela zake huwa zipo tayari kabla ya mradi kuanza
 
.

Aidha, ili kupata bei iliyo chini ya soko bila kuathiri ubora wa bidhaa au huduma, ofisi husika kwa nia ya kupata thamani ya fedha na ubora wa juu, imetakiwa kufanya ununuzi wa bidhaa na huduma mahususi moja kwa moja kutoka kwa mtengenezaji, au kiwandani, mwakilishi wa mtengenezaji au wa kiwanda, muuzaji wa jumla au mtoa huduma.

.


Chanzo: Habari Leo

Sasa hiki ndiyo nini? Kwani kuna tofauti gani na utaratibu wa sasa? Au kwa kuwa wameongeza neno 'kiwandani' ndiyo maana wameamua kuiita sheria mpya?
 
Sheria ingekuwa bora kama manunuzi ya serikali yangekuwa yanabase kwenye cash budget, sasa hapo mzabuni ana supply vitu pasi kujua ni lini atalipwa pesa yake. Unakuta mtu anasupply vitu kuja kulipwa ni baada ya miaka miwili, mitatu. Sasa hapo hata kile anacholipwa tyri thamani yake imeshuka, vingenevyo kuwepo kipengere kuwa baada ya kusupply unatakiwa uwe umelipwa dani ya muda fulani mfano "payment to be made 21 days after delivery " hapo tutatenda haki na kwa wazabuni, vingenevyo ni kukandamiza upande mmoja tu, na hivyo kukosa sifa ya kuwa sheria bora make sheria inapaswa kubana pande zote. Chukulia umesupply kalamu kwa sh 200 kwa bei ya soka kwa kipindi hiki halafu uje kulipwa hiyo 200 baada ya miaka 2, Je hapo kuna haki kweli?
 
Hii in hawamu ya tano ya hapa kazi tu hacheni kuishi kwa mazoea tumpe muda tuone utekelezaji watu tulisha kalili madilidili sasa yamekuwa dirisha kwanza tupongeze walau hii hatua ya kuthubutu mambo mengine yanarekebika,walau tunaona kuwa kuna kitu Raisi anataka aifanyie hii nchi ili isonge mbele tusimkate maini.
Hawamu = awamu
hacheni = acheni
Kalili = kariri

Tukiachana na hayo makosa tuje kwenye hoja yako. Kwani watu wanamkosoa Rais au wanahoji ili kuboresha kusudi iwe makini?
 
Sheria ingekuwa bora kama manunuzi ya serikali yangekuwa yanabase kwenye cash budget, sasa hapo mzabuni ana supply vitu pasi kujua ni lini atalipwa pesa yake. Unakuta mtu anasupply vitu kuja kulipwa ni baada ya miaka miwili, mitatu. Sasa hapo hata kile anacholipwa tyri thamani yake imeshuka, vingenevyo kuwepo kipengere kuwa baada ya kusupply unatakiwa uwe umelipwa dani ya muda fulani mfano "payment to be made 21 days after delivery " hapo tutatenda haki na kwa wazabuni, vingenevyo ni kukandamiza upande mmoja tu, na hivyo kukosa sifa ya kuwa sheria bora make sheria inapaswa kubana pande zote. Chukulia umesupply kalamu kwa sh 200 kwa bei ya soka kwa kipindi hiki halafu uje kulipwa hiyo 200 baada ya miaka 2, Je hapo kuna haki kweli?
Mkuu hizo dead lines zipo na ndio maana unasikia serikali inadaiwa fidia kwa kuchelewa kulipwa, mara nyingi hizi serikali haziwi fair kwa supplier
 
Safi sana! Vitu kama hivi huwezi kusikia opportunist wakivichambua na kusifia zaidi ya kuvizia matukio ya kupiga siasa. Tungeweka utaratibu wa sheria kama hizi kutobadilishwa zaidi ya kuboreshwa zaidi bila kuondoa msingi wa uanzishwaji wake.
 
Safi sana! Vitu kama hivi huwezi kusikia opportunist wakivichambua na kusifia zaidi ya kuvizia matukio ya kupiga siasa. Tungeweka utaratibu wa sheria kama hizi kutobadilishwa zaidi ya kuboreshwa zaidi bila kuondoa msingi wa uanzishwaji wake.
Ungeeleweka vizuri tu bila kuingiza "opportunists" sheria zichambuliwe kwa mkutadha huo bila kuingizia grudges zetu
 
Back
Top Bottom