Sheria mpya ya mifuko ya hifadhi ya jamii,Wafanyakazi wa umma na wasio wa umma kufa masikini

BRAND

JF-Expert Member
Jun 2, 2013
295
249
Serikali ya Tanzania imekusudia kupeleka muswada bungeni utakaoleta utaratibu mpya wa jinsi ya kulipa mafao kwa wastaafu wote walio jiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii,kupitia sheria hiyo ambayo serikali inataka itumike kulipa mafao ya wastaafu itakuwa hivi.

Kila mstaafu wa umma au binafsi atapewa robo ya kile anachotakiwa kupewa baada ya kustaafu kazi, yaani kama anatakiwa apewe millioni 100 basi yeye atapewa million 25,halafu baada ya malipo hayo kufanyika ni kwamba mstaafu atakuwa anapewa kila mwezi nusu ya basic salary yake aliyokuwa anapata kabla ya yeye kustaafu,malipo hayo atakayo kuwa anapata mstaafu yatakoma pindi tu atakapo fariki.

Ikumbukwe kwamba kujiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii ni lazima kwa mwajiriwa yoyote na umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria ni miaka 60.

Msimamo wa vyama vya wafanyakazi:

Vyama vya wafanyakazi vimepinga muswada unaotaka kupelekwa bungeni na serikari, mara zote tatu vyama vya wafanyakazi walipo kutana na wawakilishi wa serikali huko mbeya,dodoma na hata mara ya mwisho arusha walipokutana hasira zilijitokeza kupinga jambo hilo kwani ni unyonyaji uliokithili unaotakiwa kuletwa,kwa mujibu wa mnyetishaji wangu mkutano wa mwisho kati ya wawakilishi wa serikali na vyama vya wafanyakazi unatarajiwa kufanyika Dar kabla ya bunge kuanza mwishoni mwa mwezi huu,ili ikiwezekana muswada huo upelekwe kujadiliwa na wabunge wa wakilishi wa wananchi.

Inasemekana kwanba muswada huu wa sheria ulitakiwa kupelekwa bungeni tangu mwezi Novemba ktk bunge lililopita,ilishindikana kutoka na suala la escrow kuchukua muda mwingi zaidi.

Wachache wafanyakazi nilio sikia maoni yao wamesikitika na wanaona kama sheria hiyo ikipita basi waajiriwa wengi watakufa maskini kwani mtu wa miaka 60 kwa Tanzania anakuwa na muda mchache sana wa kuishi,ukizigatia wengi wao wanategemea pesa za kustaafu ili wajenge nyumba nzuri na kuanzisha vitega uchumi tofauti...!!

NB: Serikali imeikopa sana mifuko hii ya hifadhi ya jamii kiasi kwamba inashindwa kujiendesha vizuri,hivyo inatafuta namna ya kuiokoa na balaa la kufilisika.Chuo kikuu cha Dodoma ni fedha za mifuko hii hadi leo bado hazijarudi!
 
Kwani sasa lump sum ni asolimia ngapi? Tucta wakomalie asilimia 80 ya basic pay kama ilivyo kwa mafao ya viongozi Wa umma.
 
Ndugu kama hao Serikali wamekutuma uje hapa upime maoni ya wafanyakazi, basi warudishie majibu kuwa hilo suala lao la kishetani wakae nalo majumbani mwao! Waambie kuwa kama wameichoka amani ya nchi hii bahati mbaya sina maneno ya kukuonesha ni jinsi gani nilivyochukizwa na hilo wazo katili namna hiyo, na laiti ungekuwa karibu yangu ningekuonesha robo ya hasira niliyonayo kwa kukata pua yako ili uwafikishie salamu hao waliokutuma uje kubeep wafanyakazi! Waambie Serikali waagize mabomu ya kuua kabisa na sio ya machozi pia wasisahau risasi za moto, naapa kuwa nitahakikisha nafanya kitu ambacho Serikali hawataamini kama mimi ndiye nimetekeleza hilo! Waambie hao Serikali sera zao mbovu ndio zimetufikisha hapa tulipo, bado tena hawaridhiki wanataka kutufungia jiwe la kusagia nafaka shingoni!?
 
Hii sheria ikipitishwa na Bunge, ninaamini nchi haitakaa na amani!
 
Ndugu kama hao Serikali wamekutuma uje hapa upime maoni ya wafanyakazi, basi warudishie majibu kuwa hilo suala lao la kishetani wakae nalo majumbani mwao! Waambie kuwa kama wameichoka amani ya nchi hii bahati mbaya sina maneno ya kukuonesha ni jinsi gani nilivyochukizwa na hilo wazo katili namna hiyo, na laiti ungekuwa karibu yangu ningekuonesha robo ya hasira niliyonayo kwa kukata pua yako ili uwafikishie salamu hao waliokutuma uje kubeep wafanyakazi! Waambie Serikali waagize mabomu ya kuua kabisa na sio ya machozi pia wasisahau risasi za moto, naapa kuwa nitahakikisha nafanya kitu ambacho Serikali hawataamini kama mimi ndiye nimetekeleza hilo! Waambie hao Serikali sera zao mbovu ndio zimetufikisha hapa tulipo, bado tena hawaridhiki wanataka kutufungia jiwe la kusagia nafaka shingoni!? Tumeshawachoka shenzi zao, manina zao!

Nani katumwa na serikari? Kweli una hasira,mbona uzi umekaa kitaarifa zaid kuliko ulivyoelewa wewe! Ok,by the way mi ni mmoja wa watakao athirika na hii sheria ya kinyonyaji kama itapitishwa..
 
Nawaambia tu kama huo ndio mpango wao ni bora ukafie private sector kuliko huo unyonyaji wanaotaka kuuleta.
 
Hii ni zaidi ya ufisadi, kwanini malipo yasitishwe pindi mstaafu anapofariki!!?
Kwanini familia yake isiendelee kulipwa?
Baada ya mstaafu kufariki, mafao yake yanaenda wapi?

Nina wasiwasi fedha za mifuko ya jamii zimeshachotwa kwa shughuli nyingine.
 
Tetesi ni kwamba serikali inachukua fedha kwenye mifuko na kufanyia miradi hivyo mifuko iko hoi. Suluhisho sasa ni kulipa robo robo kwa wastaafu. Wafanyakazi hawawezi kukubali unyonyaji wa ajabu namna hii. Mishahara yenyewe inayolipwa ni kidogo halafu tena anaibiwa uzeeni. HAIKUBALIKI.
 
Huo ni unyonyaji unaotakiwa kupingwa kwa nguvu zote!!!

Safi kabisa, I support you, pokea hii quote poa ya mpambanaji:

"My blood will nourish the tree that will bear the fruits of freedom. Tell my people that I love them. They must continue the fight." - Solomon Mahlangu, 6 April 1979.
 
Anaye jua atuwekee hapa formula ya sasa na formula inayopendekezwa ili tujue. Maana haya maelezo ya jumla jumla yanatufanya tushindwe kujua ni kiasi gani formula mpya itatukandamiza.
 
Wanamaliza makaratasi bure kuandika kitu ambacho hata mfanyakazi awe mtiifu kiasi gani hawezi kukubaliana nacho.
 
Kama ndoto vile ila jamaa walivyo na roho ngumu na mbaya wanaweza wakalazimisha upite maana pesa ni tamu na ni wao tu ndio wanaiihitaji
 
Watajuaje kama mtu amekufa? Kuna watu hapo wataishi hadi miaka 200 wakipokea hiyo posho...ni ngumu sana kufanya follow-up ya vifo esp' kwa wale wanaoishi vijijini...
 
Mbwa akikaribia kufa hujisogeza mwenyewe barabarani ili agongwe! Iacheni ccm itapetape kwani huo ndio mwisho wao na nina uhakika kuwa wafanyakazi wataizika rasmi.
 
Kama ndoto vile ila jamaa walivyo na roho ngumu na mbaya wanaweza wakalazimisha upite maana pesa ni tamu na ni wao tu ndio wanaiihitaji

Mkuu umenifanya nicheke kama nimeferahi kumbe hapana,

Lakini wacha wapeleke huo mswada ili tupate cha kuongezea kwenye kampeni tupate kuwang'o hadi mizizi iliyobaki
 
Back
Top Bottom