Sherehe inapogeuka msiba

Daisy Llilies

JF-Expert Member
Apr 19, 2019
1,017
2,154
Kaka mmoja alikuja mkoani kwetu kwa barua kutoka Wizarani, aliletwa pale kama Ofisa wa Serikali. Ule mkoa una neema sana, ndani ya miaka miwili yule kaka aliweza kujenga ghorofa pale mjini.

Siku ya ufunguzi wa ghorofa lile, alitualika watumishi wenzake, viongozi wa dini na mama yake mzazi tuliambiwa atafika na basi la saa saba mchana hivyo dua zimsubiri mgeni huyu muhimu.

Tulifika saa 12 asubuhi kusaidia shughuli, tulikata vitunguu na kupika pilau, tulikata kachumbari na tulitengeneza salad ya matunda. Wali maharage na wali kuku havikukosekana.

Basi la saa saba likawasili, mwenye sherehe akaenda kumpokea mgeni wa muhimu. Kufika kule wanamkuta mama amekauka kwenye kiti cha basi. Alifariki saa ngapi ni siri ya Mungu. Basi chakula cha sherehe kiligeuka kuwa cha msiba.
 
Umenikumbusha andiko fulani katika Biblia takatifu !

Imeandikwa:

“Baraka ya Bwana haichangamani na huzuni”

Kama sijakosea!

Sasa huwa huwa najiuliza,

Je inamaana ikitokea jambo jema la mafanikio linachangamana na jambo la huzuni inamaana itakuwa lile jema litakuwa halikutokana na Mungu au inakuwaje?

Naomba kusaidiwa tafadhali wasomaji wa Biblia na wenye Roho Mtakatifu Naomba mnisaidie!
 
Kaka mmoja alikuja mkoani kwetu kwa barua kutoka Wizarani, aliletwa pale kama Ofisa wa Serikali. Ule mkoa una neema sana, ndani ya miaka miwili yule kaka aliweza kujenga ghorofa pale mjini.

Siku ya ufunguzi wa ghorofa lile, alitualika watumishi wenzake, viongozi wa dini na mama yake mzazi tuliambiwa atafika na basi la saa saba mchana hivyo dua zimsubiri mgeni huyu muhimu.

Tulifika saa 12 asubuhi kusaidia shughuli, tulikata vitunguu na kupika pilau, tulikata kachumbari na tulitengeneza salad ya matunda. Wali maharage na wali kuku havikukosekana.

Basi la saa saba likawasili, mwenye sherehe akaenda kumpokea mgeni wa muhimu. Kufika kule wanamkuta mama amekauka kwenye kiti cha basi. Alifariki saa ngapi ni siri ya Mungu. Basi chakula cha sherehe kiligeuka kuwa cha msiba.
Daisy, hili ni fumbo? Changamsha genge? Chai ? Au jambo lililotokea kweli?
 
Hadithi hii inatufundisha nini?
Hahaha nimeona funzo, ni kwamba;

Mosi, ukila ukashiba usidhani ndio mwisho wa njaa.

Pili unapokula jaribu ku share na wengine hicho chakula, ukishiba peke yako wenye njaa husononeka kwamba ama umekula sana au wewe mbinafsi na mchoyo.

Tatu usialike masikini wenye njaa kwenye sherehe za walioshiba matajiri.

Mwisho endelea kujifunza kupitia tafakuri tofauti.
 
Kwa iyo unataka kushauri kina mama wasisafiri na basi za mkoa tuwatafutie usafiri mwingine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom