Shelukindo: Namuunga mkono Lowassa kumrithi Kikwete

Shelukindo: Namuunga mkono Lowassa kumrithi Kikwete

Naunga mkono Lowasa kuwa Rais, lakini sio rais wa Tanzania yetu hii, labda awe rais wa chama cha mafisadi, kwa hiyo wajemeni tusimlaumu sana huyu mama, labda alimaanisha kuwa jamaa atakuwa rais wa Ngumi, si nayo inahitaji maamuzi magumu. But this man cant be, and will never be the president of our Nation. Huyo jamaa ni mwizi!!!!!!!
 
Piga uwa,lazima rais ajeye atoke mkoani Arusha,kati ya Dr W.P SLAA au mkuu wa Richmond.riz 1,nape na chogo chemba kama hamtaki mjinyonge.
 
Huyu mama anajua anachokisema. Hapigi mayowe bure. Naamini ana watu wako nyuma yake kwa kuwa yeye hana cha kupoteza kwa sasa hata kama akitolewa kafara.

Kwa staili ya uongozi wa mwenyekiti sitoshangaa kuwa hata mwenyekiti anajua kinachoendelea na amekibariki ila kama kawaida yake ni mtu wa kula matendo yake mwenyewe pale mambo yanakwendea ndivyo sivyo. Ni mangapi ameyakana hadharani? Tutakuja kuona mambo mengi tusubiri tu muda utaamua, huu ni mwanzo tu.

Lowassa ameshasema serikali imara ni ile inayochukua "maamuzi magumu!" Maamuzi magumu mfano: kumfukuza kwenye chama kwa kuwa ni fisadi ili kitakachofuata apewe uwanja wa kutoa yaliyo moyoni mwake.

Mwenyekiti anajua fika kuwa, Lowasa akiwa ndani hawezi kusema jambo lakini akitoka kwa staili ya Nape (ambayo hawathubutu na wameshaonywa mapema) atapata nafasi ya kusema na kwa vyovyote ataaminika anachokisema na atachafua hali ya ndani kiasi kwamba walio nje wote wataonekana safi (ambavyo ndivyo ilivyo) suala ni kuwaweka upenuni tu.

Mimi naamini mgombea urais wa CCM alitangazwa monduli siku hiyo. Na sherehe hiyo iliandaliwa kwa makusudi maalum si bure. Kwa mwanasiasa yeyote nguli anafahamu fika kuwa kutoka 2013 hadi 2015 ni muda mfupi sana kwa yeyote anayetaka kujiandaa kwa uprezidaa!! Tusubiri tuone!!
 
Mh Betrice Shelukindo ameamua kuvunja ukimya baada ya kutangaza kumuunga mkono Edward Lowassa kumrithi Mh. Rais Kikwete.Kazi kwako Nape na Mangula, je bado siku 90 hazijafika?

chanzo: mwananchi
watu wengine mko nyuma kihabari sana aisee yani unalishangaa hili limama leo!mbona lilishanyea kambi muda mrefu sana baada tu ya uchaguzi mkuu uliopita kisa lowassa alifadhili chakula cha hisani kwa ajili ya kumpigia debe apate kacheo gani sijui mjengoni,mama akamsaliti hadi mumewe mzee shelukindo,sasa hivi ni yeye na bashe ndio pekee waliobaki kumpigania mzee,maana hamis mgeja nasikia uzalendo umemshinda,kaachana nae,mi nilidhani labda ana kilango ndio ingekua news sio beatrice anaeamini lowassa ni mwanamme wa shoka
 
Hata mimi nitamuunga mkono lowasa. anayo kura yangu tayari. Tunahitaji mtu mwenye maamuzi magumu, hata akiwa dictator kama kagame lakini analeta maendeleo hamna shida. hata akila kidogo lakini analeta maendeleo hamna shida, kuliko kutokula kabisa halafu hata maendeleo haleti.

Hakuna mtakatifu duniani, kila mmoja alishawahi kutenda kosa mara moja au zaidi, sema tu wengine hata wale wanaowanyoshea wenzao vidole hawajawekwa peupe tu, cha muhimu ni kwamba, mtu akifanya kosa huwa kuna mazingira ya kujirekebisha. kosa si kosa bali kurudia kosa.

Hata hivyo, suala la lowasa na kashfa yake, inasemekana anazo njia za kujieleza ambazo ameweka fumbo, kuna siku wakati wa kampeni atakuja kujieleza na watu watashangaa kwamba walikuwa wanapiga mayowe ya bure kwa mtu asiyehusika.

Yapo mengi yamejificha mle kwenye ile kashfa, na inawezekana lowasa akawa kafara tu. na wapo wengi waliokuwa juu ya lowasa wamefichwa, lowasa kachukua msalama wa wengi pale.

Mteteeni mnavyotaka ila lowassa ni MWIZI period! Tunabyojadili hapa ameshirikiana na askofu Laizer kuifilisi hotel ya KKKT Arusha ili ajiuzie kwa bei ya kutupa. Huyu hatosheki hata kidogo, tukifanya kosa la kumpa urais tutalia na kusaga meno.
 
kama Mungu akitoa kibali kura nitampigia dr. w. slaa asipogombea nitampa EL.
 
Huyo mama anastahili kuchekiwa afya yake kuanzia miguuni mpaka kichwani,she is a disaster kwa wanaomjua..
 
Mh!hii kali inachochea mgawanyiko ndani ya CCM!Secretariat ya CCM fanyeni kazi yenu!


Hii ndio tofauti ya CCM na CHADEMA, atleast ndani ya CCM mwanachama ana uhuru wa mawazo,hakuna kikao chochote kitakachopoteza muda kujadili kwanini mwanachama anaamini fulani ndio anafaa kuwa Rais na sio fulani.
 
Mh Betrice Shelukindo ameamua kuvunja ukimya baada ya kutangaza kumuunga mkono Edward Lowassa kumrithi Mh. Rais Kikwete.Kazi kwako Nape na Mangula, je bado siku 90 hazijafika?

chanzo: mwananchi

Huyo maza anajulikana yupo kamba ya Lowassa siku mingi................................... na kuwepo kwake bungeni ilitokana na support ya Mr. whitehead
 
Raha ya siri ni kutoisema.

Huyu mama ana mambo kama ni siri yake si angekaa nayo na kuiwakilisha kwenye vikao halali vya chama?????
 
Kila mwanaCCM akiamua kwa wakati wake kutaja kambi anayounga mkono chama kitakuwa salama?
 
Nyinyi watoto wa mama sikilizeni lowassa ni jembe
 
Watu wenye akili vizuri kama bado wapo ccm hawawezi kubali huo upuzi. Huyu bwana hana jipya tena alikuwa kwenye mfumo muda mrefu lakini hana alichofanya.
Bungeni ndio usiseme kule kawa bubu sasa tumpe urais mtu kama huyu ili tulie tena miaka 10? Apewe cheo cha MZEE WA MICHANGO HIYO ATAWEZA.



Mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe, lakn ukubali ukae anafaa kuwa prezidenti
 
God Bless Tanzania, God bless Lowassa appointed as the president who art in 2015
 
Hii ndio tofauti ya CCM na CHADEMA, atleast ndani ya CCM mwanachama ana uhuru wa mawazo,hakuna kikao chochote kitakachopoteza muda kujadili kwanini mwanachama anaamini fulani ndio anafaa kuwa Rais na sio fulani.

kikao gani ndani ya ccm kinachoweza kumjadili Lowasa..si kikwete, kinana, mangula na mavuvuzela wao kama Nape
 
Tunaitaji raisi mwenye maamuzi magumu kama lowasa.raisi ambae anamsimamo kwa sasa ssm ni lowasa tu.
Yaan ameshavuliwa lile gamba kwa hiyo tunafukiza marashi ili lile la richmond lisahaulikekweli shelukindo umebugi, kama ndivyo hata Rostam anafaa kuwa rais!
 
Mh Betrice Shelukindo ameamua kuvunja ukimya baada ya kutangaza kumuunga mkono Edward Lowassa kumrithi Mh. Rais Kikwete.Kazi kwako Nape na Mangula, je bado siku 90 hazijafika?

chanzo: mwananchi

Hayo ni matokeo ya New Year party ya Monduli!!
 
Back
Top Bottom