Shelukindo katikisa Taifa kwa dakika 10 tu.

Shelukindo katikisa Taifa kwa dakika 10 tu.

akide

Member
Joined
Jun 5, 2012
Posts
11
Reaction score
1
Mama huo ndio ukomavu wa kisiasa na usomi,utapita 2015,maana wabunge hao wanaohangaika kuwajibu wapinzani,kweli hawaelewi maana ya upinzani,maana umeongea dakika kumi tu,na umekuna taifa zima,kwa maneno ya kujenga nchi,we ni mzalendo,endelea hivyo mama achana na hao wanaoshinda kujibu upinzani na kupiga makofi,machozi ya watanzania watayalipa siku moja kwa unafiki na uovu wanaoufanya.
 
Mama huo ndio ukomavu wa kisiasa na usomi,utapita 2015,maana wabunge hao wanaohangaika kuwajibu wapinzani,kweli hawaelewi maana ya upinzani,maana umeongea dakika kumi tu,na umekuna taifa zima,kwa maneno ya kujenga nchi,we ni mzalendo,endelea hivyo mama achana na hao wanaoshinda kujibu upinzani na kupiga makofi,machozi ya watanzania watayalipa siku moja kwa unafiki na uovu wanaoufanya.
 
Hadi sasa, ni wabunge Filikunjombe, Mkono, Sendeka na huyu mama kambi ya CCM ambao wameonakana kujifungua toka kwenye minyororo ya u-chama. Kanifurahisha sana alipowashangaa wabunge wa CCM wanaotarajia CDM isifanye kazi yake ya kuwakosoa watawala.
 
Mleta mada uwe msomi basi na sio msomaji wakilisha mada kama grt thinker bana.Wengne hatuwa na acces ya tv
 
Nimesikilza kidogo nilichopata kazungumzia umuhimu wa wapinzani katka mfumo wa vyama vingi na kasema wanaopoteza muda kupambana bungeni na kambi ya upinzani ni wasioelewa maana ya upinzani.Hoja zianzotakiwa kujadiliwa bungeni ni taarifa ya mzee wa gombe, hotuba ya waziri wa fedha na mpango wa maendeleo 5yrs kwisha.Mambo ya kujadili hotuba ya kambi ya upinzani huo ni uzezeta ni nje ya mada.AMEWATAKA WAPINZANI WAONGEZE NGUVU KUIPINGA NA KUIKOSOA SERIKALI YA CCM ILI IENDELEEE KUTAWALA.Mama kapinga mwenendo wa wabunge wa ccm kushambulia upinzani
 
Huyu mleta maada hajatulia au hajui wengi tupo ofcini tunajenga mataifa ya Ulaya!!!!! Siyo wote tunaangalia au kusikiliza TV. Please njoo tena
 
Hadi sasa, ni wabunge Filikunjombe, Mkono, Sendeka na huyu mama kambi ya CCM ambao wameonakana kujifungua toka kwenye minyororo ya u-chama. Kanifurahisha sana alipowashangaa wabunge wa CCM wanaotarajia CDM isifanye kazi yake ya kuwakosoa watawala.

Unajua watakaorudi bungeni 2015 kutoka upande wa CCM ni wachache sana. Muulize mama kilango aliona nini kule Kiwira.
 
Kwa kifupi, Beatrice Shellukindo kawaambia wabunge wa CCM kuwa wanachofanya wabunge wa upinzani ni sahihi kabisa, wako hapo kukosoa chama tawala na ndivyo wanatakiwa kufanya kama wabunge wa upinzani. Badala ya kukwashambulia wangechukuwa yale mazuri wanayoambiwa na upinzani.

Pia kasema wabunge wa upinzani wanapenda sana chama tawala na wanachofanya ni kukosoa ili chama tawala kijirekebishe na hivyo kuendelea kubaki madarakani.

Kwa maoni yangu Beatrice Shellukindo ameonesha uelewa mzuri sana wa siasa za vyama vingi ndani ya bunge. Ameonesha kuwa na ngozi mungu jambo ambalo ni muhimu kwenye ulingo wa siasa. Wabunge wa CCM wanaoshambulia wapinzani ni kutoelewa nini kazi za ya wapinzani. Kuna utoto wa hali ya juu CCM!
 
Si bora hao ungejadili wewe na mpenzi wako kisha sisi ukatutaarifu alichosema huyu mama. Ina maana gani sasa kutuwekea mawazo yako hapa,usiwe na akili kama za mwigulu Nchemba
 
Hadi sasa, ni wabunge Filikunjombe, Mkono, Sendeka na huyu mama kambi ya CCM ambao wameonakana kujifungua toka kwenye minyororo ya u-chama. Kanifurahisha sana alipowashangaa wabunge wa CCM wanaotarajia CDM isifanye kazi yake ya kuwakosoa watawala.

Sendeka na Kilango huwa wanageuka na wanarudi kwenye magamba.
 
wameongea nini,

pipa naungana na muyaka binhaji.... sidhani kama tunataka kutikisana, tunachohitaji ni mambo ya mbolea kuboresha taifa

hayo ya kuwasha moto, kutema cheche, kutikisha, kufuka moshi, kuvurumisha vumbi nk.. hayana tija katika jamii
 
sendeka na kilango wana issues na personalities zao wenyewe
 
Si bora hao ungejadili wewe na mpenzi wako kisha sisi ukatutaarifu alichosema huyu mama. Ina maana gani sasa kutuwekea mawazo yako hapa,usiwe na akili kama za mwigulu Nchemba

Kazi kweli kweli!
 
Back
Top Bottom