Shekhe kundecha apongeza elimu ya dini katka mtaala mpya

Shekhe kundecha apongeza elimu ya dini katka mtaala mpya

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
781
Reaction score
1,831
Katika eneo la elimu kumekuwa na utata mkubwa wa uelewa nchi yetu imekuwa ikihangaishwa sana na tatizo la maadili lakini iko nyuma sana kwenye mafunzo ya dini, tulikuwa tunasema sasa nchi yetu inataka maadili gani ambayo hayatokani na dini?"

"Lakini kupitia uongozi wako (Rais Samia Suluhu) hapa tunashuhudia katika mtaala mpya sasa masomo ya dini ni rasmi na sasa kazi imebaki kwa Watanzania kuandaa walimu bora wanaoweza kufundisha lugha ya kiarabu”

“Wanaoweza kufundisha maarifa ya kiislamu na pia watapata ajira ya Serikali kwa kufanya kazi hiyo hiyo ambayo kwa kipindi chote tulikuwa tukifanya waislamu bila ya msaada wowote hili ni jambo kubwa sana la kushuru"

"Mheshimiwa Rais umetupa faraja kubwa sana kutuwekea mazingira mazuri ya kuwafundisha vijana wetu na Watanzania kwa ujumla misingi mizuri ya imani na dini zao katika mfumo wa nchi unaotambulika tunaamini ukipata kipindi kingine tutapata makubwa zaidi”-Shekhe Mussa Kundecha akizungumza katika kongamano la amani katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
 
Haya Sasa kumeanza kuchangamka. Nchi ni ya wote. Maendeleo hayana vyama. Kazi na utu tusonge mbele.
 
Maadili yanayotokana na mafundisho ya vitisho ya dini hukuza watoto waoga na wanafiki.
Ona washika dini wasivyo na maadili; ni wezi, waongo, mafisadi, wavivu, wauaji na kadhalika.

Kisha hapo, tazama nchi wanazofundisha maadili kwa kuelewesha watoto logic nyuma ya hayo maadili wanayofundishwa walivyo na utu, uadilifu, heshima n.k.

Bado tuna safari ndefu kama mwaka 2025, tunategemea vitisho vya biblia na kurani kufundisha watoto maadili.
 
Serikali haipaswi kuweka mambo ya dini katika elimu.

Niwe mkweli tu kwa upande wangu siamini kabsa hizo dini ila naamini MUNGU yupo.

Hizo gharama zakugharamia masomo ya dini wangewekeza kwa walimu waliopo na kuongeza wengine ili elimu yetu iwe bora zaidi.
 
Back
Top Bottom