Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 242
Wana-JF:
Hii ni sehemu ya mwisho ya stori ya Dr Slaa atabiriwa kifo katika Tanzania daima ya leo.
.Wakati huo huo Makama Kuu jijini Dar es Salaam imeombwa kumkamata na kumshitaki mnajimu Sheikh Yahya Hussein kwa kutoa kauli ya kitisho kwamba yeyote ambaye angeshindana na Rais Kikwete katika kinyanganyiro cha kura ya maoni ya urais ndani ya CCM angefariki dunia ghafla.
Taarifa za kuaminika zilizolifikia gazeti hili jana zilisema Paul Mhozya, ambaye ni mwalimu mstaafu wa taasisi ya elimu nchini, ndiye aliyewasilisha ombi hilo Mahaka Kuu akitaka Sheikh Yahya ahukumiwe kwa kukiuka sheria ya makosa ya ushirikina na uchawi Witchcraft Act aliyodai inakataza kitendo cha mtu kutumia uwezo wake katika mambo ya kishirikina kutisha wengine.
Ibara ya tatu ya sheria hiyo inasema: Mtu yeyote ambaye, kwa kauli au kwa matendo anajipambanua kuwa na nguvu ya uchawi au kutishia kuitumia au kuegemea katika matumizi ya kichawi juu ya kitu chchote cha kichawiu au dhidi ya mtu yeyote, amefanya kosa.
Kesi hii inayogusa suala lililogubikwa na utata mkubwa ni ya pili kufunguliwa na Mhozya, baada ya kufungua kesi nyingine mwezi Julai mwaka huu akitaka jina la Rais Jakaya Kikwete liondolewe katika orodha ya wagombea urais kwa madai ya kukiuka matumizi mabaya ya madaraka na Katiba ya nchi.
Kwa ombi hilo Sheikh Yahya ikiwa anaweza kupatikana na hatia anaweza kufungwa miaka saba jela au kulipa faini isiyopungua sh elfu moja.