DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mwalimu wa masuala ya dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Rusaganya, amewajia juu viongozi wa dini nyingine kwa kutoa matamko kuhusu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Amesema kuwa Rais Samia anatukanwa sana, hivyo ni vyema viongozi wa dini nyingine wakaacha kutoa matamko yasiyo na adabu dhidi yake. Sheikh Rusaganya amehoji kwa nini kila mara Rais anapokuwa Muislamu, maneno na matamko mengi huibuka.
Aliyasema hayo Oktoba 23, 2025, wakati akihutubia msikitini na kuwaonya vijana kushiriki kwenye maandamano.
Amesema kuwa Rais Samia anatukanwa sana, hivyo ni vyema viongozi wa dini nyingine wakaacha kutoa matamko yasiyo na adabu dhidi yake. Sheikh Rusaganya amehoji kwa nini kila mara Rais anapokuwa Muislamu, maneno na matamko mengi huibuka.
Aliyasema hayo Oktoba 23, 2025, wakati akihutubia msikitini na kuwaonya vijana kushiriki kwenye maandamano.