Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda leo Alhamisi, Juni 5, 2025 ametangazwa kujiunga na Chama cha ACT-Wazalendo.
===
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda leo Alhamisi, Juni 5, 2025 anatarajiwa kutangaza kujiunga na Chama cha ACT-Wazalendo.
Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya ACT-Wazalendo, Sheikh Ponda atatangaza uamuzi huo mbele ya viongozi waandamizi wa chama hicho katika mkutano na waandishi wa habari utakaofanyikia makao makuu yake, Magomeni jijini Dar es Salaam.
Tayari ACT-Wazalendo imetoa matangazo ya kuonesha kuna ‘mwamba’ ambaye atajiunga nao. Kumekuwa na maswali mengi ni kiongozi gani huyo?
Sheikh Ponda anatarajia kujiunga pamoja na watu wengine wanaomuunga mkono na huenda akawa miongoni mwa wale watakaoomba ridhaa ya kuwania ubunge katika moja ya majimbo jijini Dar es Salaam.
Chanzo Mwananchi
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda leo Alhamisi, Juni 5, 2025 anatarajiwa kutangaza kujiunga na Chama cha ACT-Wazalendo.
Tayari ACT-Wazalendo imetoa matangazo ya kuonesha kuna ‘mwamba’ ambaye atajiunga nao. Kumekuwa na maswali mengi ni kiongozi gani huyo?
Sheikh Ponda anatarajia kujiunga pamoja na watu wengine wanaomuunga mkono na huenda akawa miongoni mwa wale watakaoomba ridhaa ya kuwania ubunge katika moja ya majimbo jijini Dar es Salaam.
Chanzo Mwananchi