Sheikh Katimba: Makonda achunguzwe

Sheikh Katimba: Makonda achunguzwe

Na vyeti vyake pia vihakikiwe.watu wametumbuliwa kisa vyeti feki.yeye mbona hajitokezi kujisafisha..Ndalichako nayeye hizi sauti hazisikii??
Yule jamaa ukimsikiliza utajua tu kuwa anaelimu ya kutiliwa shaka. siyo ya kusoma hasa na kufaulu. Shida ya nchi hii hatua zinachukuliwa haraka ikiwa ni kiongozi wa uponzani. Kuna mtu walikuwa wahoji udokta wake hata haijulikani waliokuwa wanahoji wako wapi
 
Huyo ni yule sheikh ambaye siku zote ana vita na BAKWATA.Wivu umemjaa kuona Makonda ni rafiki wa BAKWATA na mfalme wa moroco anawajengea msikiti mkubwa pale .Huyu ni sheikh wa UKAWA .mASHEIKH wao ni wale WA answar sunna wagomvi wa bakwata.

hapa chini ni meya wa jiji la dar es salaam akisalimiana na DARWESHI DUME kwenye maulidi aliyoalikwa ADA ESTATE mikocheni kama mgeni rasmi.Hao ndio masheikh wa UKAWA


1.JPG
Jadili hoja usijadili mtu.
 
sheikh-300x199.jpg

JUMUIYA na Taasisi za Kiislamu nchini imevitaka vyombo vya kisheria na uchunguzi kuacha kupuuza kauli zilizotolewa na wabunge zilizomtuhumu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kumiliki mali zisizoendana na kipato chake halali.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Msemaji wa Jumuiya hiyo Sheikh Rajabu Katimba, alisema wakati wa mkutano wa Bunge lililopita baadhi ya wabunge walimtuhumu Makonda hivyo tuhuma hizo zinapaswa kufanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria.

Alisema vyombo vyenye mamlaka ya uchunguzi vinapaswa kufanya uhakiki wa mali za Makonda ili kuondoa shaka katika umiliki wa mali aliyonayo na uhalali wa misaada ya kifedha zinazotolewa kwake na taasisi rafiki.

Sheikh Katimba alisema kifungu cha (11) cha sheria ya maadili ya viongozi wa umma inamtaka kiongozi kutaja hadharani mali zake ikiwemo zawadi anazopewa.

Hivi karibuni, Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) wakati akichangia taarifa za Kamati ya Bunge na Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama alisema Makonda amenunua jengo ‘(Apartment ) lenye thamani ya shilingi mil 600 jijini Dar es Salaam.

Selesini aliliambia Bunge kuwa Makonda amempa gari mkewe aina ya Mercedez Benzi lenye thamani ya Dola 250,000 za Marekani ambazo ni sawa na Sh milioni 550.

Mbali na Selesini, Mbunge mwingine aliyemtuhumu Makonda kujilimbikizia mali ni Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma (CCM) ambaye naye wakati akizungumza bungeni alihoji ni wapi Makonda alipata fedha za kusafiri kwenye ndege daraja la juu kwenda Marekani.

Wakati huo huo, Sheikh Katimba alisema vita dhidi ya dawa za kulevya inaweza kwenda vibaya iwapo itasimamiwa na wanasiasa.

Alisema ili kuepuka hilo vyombo vya dola vyenye mamlaka ya kisheria vinapaswa kuifanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa.

Sheikh Katimba alisema taasisi za kiislamu zinaunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali kupambana na biashara hiyo na kusisitiza kuwa vyombo vyenye mamlaka kuisimamia kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana Dawa za Kulevya nchini ya mwaka 2014.

‘’Hatuoni ni kwa mantiki ipi watumiaji wengine washitakiwe kwa kutumia dawa na wengine waachiwe huku zitumike na fedha za kuwatibia nje ya nchi.

‘’Wasanii kama Rehema Chalamila, maarufu kwa jina la Ray C’ msanii TID nao pia walipaswa kushitakiwa kama walivyofanywa wengine na vilevile watumiaji walioko mitaani na kwenye vituo vya daladala wote wasombwe wakapimwe na kisha washitakiwe.

“Pamoja na nia ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuongoza na kuendesha vita hiyo lakini vita isimamiwe na vyombo vyenye weledi na si wateule wa kisiasa au wanasiasa,’’ alisema.

Aidha, alizungumza kesi za ugaidi inawakabili baadhi ya viongozi wa dini kwa kueleza kuwa haitakuwa na tija wala heshima iwapo viongozi hao wataendelea kushikiliwa gerezani.

“Ni kweli serikali inatutaka tuiunge mkono kwenye vita hiyo nasi tuko tayari lakini ni vuziri jitihada hii ikawa kwa watu wote, tunaiona serikali inashindwa kutenda haki kwa viongozi wa dini yetu na ni kesi gani isiyokwisha? inatia aibu masheikh kufungwa bila hatia miaka mitatu ni sawa na kufungwa bila hatia,’’ alisema Sheikh Katimba.


Source: Mtanzania
 
Ukweli unajitenga na unafiki. Haipendezi kwa hii serikali kuwashikilia watu bia sababu. Hivi wangekuwa viongozi wa dini nyingine hili lingewezekana? Tuache unafiki ifike mahala ionekana kila mtu anazo haki zake!
sawa kabisa mkuu wangu
 
HII NDO ILE JUMUIA YA SH.PONDA HATUWASHANGAI KUPINGA VITA DHIDI YA UNGA. WAO KAMA CDM VILE KILA JAMBO LA SERIKALI NI BAYA .
Sijui nani kapotosha hapa....bandiko linatetea vita ya madawa ila kusiwe na siasa ndani yake....
LuSilk unasema huwashangai kupinga vita dhidi ya unga...
Napata ukakasi kidogo kuelewa...
Nani kapotosha...???
 
Subiri kauli ya yule sheik wa ccm sheikh wa mkoa hadi mussa lazima atakuja kupinga haya kwa kutetea watawala, viongozi wa dini wote wangekuwa wanatumikia waumini wao basi nchi ingekuwa na maana sana kuishi,
Lakini wengi wao ni wanafiki sana, hongera sana Sheikh wangu Ponda wewe huwa huna unafiki
Na huyo Katimba ni sheikh wa mzee white hair....
Tafuta record za ziara za white hair....hakosekani pembenI....
 
Mali zake wameambiwa waliotuhumu bungeni wapeleke ushahidi tume ya maadili wafuatilie wamekataa kupeleka.Wewe utasemaje zipo wakati waliotuhumu wamekataa kupeleka ushahidi kwenye vyombo husika wakati bungeni walidai ushahidi wanao.Huyu shehe uhakika kautoa wapi wakati waliotoa tuhuma hawana ushahidi wa kutoa?
Heeh,!hv ni lini wameambiwa wapeleke ushahidi wakakataa,kwani ofisi yake si ni moja ya tuhuma,si wameshataja zawadi ya gari,na apartment aliyonunua si wameeleza ipo wapi,safari ya first class ulaya wakati mzee alikataza watumishi kusafiri safari za nje mpaka kwa kibali cha jengo jeupe,magari anayomiliki,!? Na kwani si anatakiwa yeye ndo aende mjengoni dodoma kwanza kwenye kamati yao kwanza,. Kwani wabunge walimtuhumu kwa mikataba au bank account ambazo unaweza ukasumbuka kuzipata,!? Hivyo si tangiable thing, vinaonekana kwa macho sa unataka ushahidi gani mwingine,!? Sa nyingine kabla ya kupost vitu kwa ajili ya uchama fikiria kwanza unachotaka kucoment, sio unakurupukakurupuka kimakondakta
 
Hawa masheikh wa siku hizi wanajiingiza kwny mambo ya siasa sana
 
Sheikh mkuu wa Dar kalegea na pesa za GSM
Halafu hawa washkaji kuna kashfa za mabati wanapitisha kimya kimya bandarini kutoka China lakini mijitu inakaa kimya tu,simply Makonda ni mshkaji wao.
Kwa mfano.
Wanaleta makontena 14 wanalipa manne (4)
Halafu kumi.... nawanukuu...wanajilipua.STUPID.
 
Huyo ni yule sheikh ambaye siku zote ana vita na BAKWATA.Wivu umemjaa kuona Makonda ni rafiki wa BAKWATA na mfalme wa moroco anawajengea msikiti mkubwa pale .Huyu ni sheikh wa UKAWA .mASHEIKH wao ni wale WA answar sunna wagomvi wa bakwata.

hapa chini ni meya wa jiji la dar es salaam akisalimiana na DARWESHI DUME kwenye maulidi aliyoalikwa ADA ESTATE mikocheni kama mgeni rasmi.Hao ndio masheikh wa UKAWA


1.JPG
mbona huyu unasema daruwesh dume alikuwepo maulid ya msikiti wa manyema kariakoo nahuo msikiti maarufu wa ccm
 
Hawa watu ni wanafik sana aiseeeeeee.......
Juzikati walimpigia makofi na kumshangilia pale Paul alipo ahidi kuwajengea Nyumba ya sala...... .
Ebu ngoja niishie hapa, maana nimesha kasirika
sasa ukiwepa zawadi na konda ya kupanda daldala bure hutafurahia? na je huyo konda akijamba hutamwambia?? we ndo mnafiki sasa...
 
Back
Top Bottom