Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,818
- 62,030
Masheikh wa BAKWATA wamekuwa hawajali kwa kina maslahi ya waislamu nchini. Wao wamekuwa kama rear guards wa kulinda mfumo, kutetea serikali, kuwalaza waislamu usingizi pindi joto la haki nchini likipanda.
Hivi karibuni Maaskofu wamekuwa msitari wa mbele kulaani matendo ya kitekaji na uuaji yanayoyendelea nchini, cha ajabu Masheikh wa BAKWATA badala ya kukemea na kulaani mambo hayo, wao wamekuwa msitari wa mbele kuitetea serikali kwa kuleta hoja za "whataboutism", hoja zao dhidi ya maaskofu ni mbona mtawala alipokuwa fulani hamkusema. Japo hiyo hoja yao si kweli kwa sababu maaskofu kipindi cha utawala wa Magufuli wamewahi kutoa waraka mzito wa Kwaresma kulaani ukandamizaji nchini, lakini ni Masheikh ndo waliokaa kimya huku dhulma kwa wafanyabiashara, wanasiasa na watu wengine zikifanyika.
Tumeona jinsi maaskofu walivyosimama kumkatakia Magufuli katakata alipodai eti nchini COVID haipo. Wakasema wanaoumia na COVID ni watawa wao pamoja na waumini wao, lazima serikali ichukue hatua. Wakati maaskofu wakifanya hayo Masheikh wa BAKWATA kimyaa.
Maaskofu walipolalamika kuumizwa kwa padri wao, Father Kitima, Masheikh wa BAKWATA wanang'aka eti mbona maaskofi hawakuwatetea masheikh walipowekwa ndani. Badala ya Masheikh wa BAKWATA wawe msitari wa mbele kuwatetea masheikh wenzao, wao wanaoiga kimya, kisha wanangoja maaskofu wazungumze jambo la manufaa halafu wao wapinge!. Ajabu sana hii.
Juzi kauawa Sheikh Jabir huko Zsnzibar. Alitekwa na watu, Jioni yake mwili ukaokotwa pembezoni mwa barabara. Lakini huwasikii Masheikh wa BAKWATA wakikemea hili.
Kwa kweli hili ni tatizo kubwa, ni shida kubwa kwa Waislamu.
Angalau Sheikh Ponda na shura ya maimamu huongea, lakini siyo hawa masheikh wa BAKWATA ambao ni chombo kikubwa nchini.
Hebu tazama hapa chini video ya mazishi ya Sheikh Jabir, na mahojiano ya Sheikh Ponda ( Siyo BAKWATA huyu)
Hivi karibuni Maaskofu wamekuwa msitari wa mbele kulaani matendo ya kitekaji na uuaji yanayoyendelea nchini, cha ajabu Masheikh wa BAKWATA badala ya kukemea na kulaani mambo hayo, wao wamekuwa msitari wa mbele kuitetea serikali kwa kuleta hoja za "whataboutism", hoja zao dhidi ya maaskofu ni mbona mtawala alipokuwa fulani hamkusema. Japo hiyo hoja yao si kweli kwa sababu maaskofu kipindi cha utawala wa Magufuli wamewahi kutoa waraka mzito wa Kwaresma kulaani ukandamizaji nchini, lakini ni Masheikh ndo waliokaa kimya huku dhulma kwa wafanyabiashara, wanasiasa na watu wengine zikifanyika.
Tumeona jinsi maaskofu walivyosimama kumkatakia Magufuli katakata alipodai eti nchini COVID haipo. Wakasema wanaoumia na COVID ni watawa wao pamoja na waumini wao, lazima serikali ichukue hatua. Wakati maaskofu wakifanya hayo Masheikh wa BAKWATA kimyaa.
Maaskofu walipolalamika kuumizwa kwa padri wao, Father Kitima, Masheikh wa BAKWATA wanang'aka eti mbona maaskofi hawakuwatetea masheikh walipowekwa ndani. Badala ya Masheikh wa BAKWATA wawe msitari wa mbele kuwatetea masheikh wenzao, wao wanaoiga kimya, kisha wanangoja maaskofu wazungumze jambo la manufaa halafu wao wapinge!. Ajabu sana hii.
Juzi kauawa Sheikh Jabir huko Zsnzibar. Alitekwa na watu, Jioni yake mwili ukaokotwa pembezoni mwa barabara. Lakini huwasikii Masheikh wa BAKWATA wakikemea hili.
Kwa kweli hili ni tatizo kubwa, ni shida kubwa kwa Waislamu.
Angalau Sheikh Ponda na shura ya maimamu huongea, lakini siyo hawa masheikh wa BAKWATA ambao ni chombo kikubwa nchini.
Hebu tazama hapa chini video ya mazishi ya Sheikh Jabir, na mahojiano ya Sheikh Ponda ( Siyo BAKWATA huyu)