voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Nimemsikiliza huyu aliyewahi Kuwa sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, almaarufu Alhad Mussa Salum.
Amekuja na tamko la hiyo wanayojiita kamati ya maridhiano na amani. Anaongea kinafiki, akiomba viongozi wa Dini kutorushiana maneno kutokana na kadhia ya mkataba wa DP-WORLD.
Ameenda mbali na kusema sasa yete na kamati yake,wanaufunga mjadala na anaomba tuiachie serikali itimize wajibu wake kutokana na maoni ya wananchi kutosha sasa.
Sasa nikashindwa kumuelewa. Kwa sababu mpaka sasa hakuna viongozi wa Dini waliorushia maneno wenzao, zaidi ya masheikh kadhaa wanaoibuka na taasisi zao tofauti za kiislamu toka huko watokako.
TEC walikwishamaliza kazi yao na sasa waraka unatembea kwa kasi ya 5G.
Yeye Sheikh Alhad angeacha kuzunguka mbuyu na awaambie wenzake waache upotoshaji bali waujadili mkataba husika na waseme vifungu wanavyoviunga mkono ili jamii iwaelewe.Badala ya kuja na hoja za Udini bila mkataba mkononi kama walivyofanya wenzao wasomi wa TEC.
Nguvu inayotumika inaiaibisha serikali.
Sasa Serikali imefikia hatua mnatuletea hadi Masheikh walioondolewa madarakani kwa kashfa za kuingilia ndoa za kina Dk Mwaka?
Masheikh ambao walikuwa wakijibizana na kina Mange Kimambi?
Kweli Deep World?
Mungu inusuru Tanzania