MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Na Magdalena Mkwama, MSHITAKIWA Mohamedi Shehe (20), mkazi wa Buguruni Malapa, amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo Buguruni kujibu mashitaka ya wizi wa amplifaya. Mshitakiwa amesomewa mashitaka na karani Edwin Wandawanda mbele ya Hakimu Adelf Sachore wa Mahakama hiyo. Amedai kuwa, mshitakiwa aliingia msikitini na kuiba amplifaya ya mlalamikaji Swalehe Hassan ambaye ni Imamu wa Msikiti wa Vingunguti na huku mshitakiwa naye akiwa ni mtoto wa Imamu wa Msikiti wa Buguruni Madenge. Mshitakiwa amekana mashitaka na kesi itatajwa tena Desemba 22, mwaka huu. Habari imetoka DL |