Imamu Kortini Kwa Uchochezi

Status
Not open for further replies.

babalao 2

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
5,398
3,243
IMAM wa Msikiti wa Thaqi B,Hamza Omary (37) maarufu kama Mohamed amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza,akikabiliwa na mashitaka mawili ya uchochezi.

Alifikishwa mahakamani hapo jana mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Godfrey Mwambapa.Wakili wa Serikali, Felista Lelo alidai kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo kati ya Desemba mwaka jana na Februari mwaka huu katika Msikiti wa Thaqi B wilayani
Nyamagana jijini Mwanza.

Katika shitaka la uchochezi,Wakili alidai Imam huyo anadaiwa kuchochea chuki kwa nia ovu chini ya Kifungu Namba 63 B (i) (ii) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alidai katika kipindi cha miezi hiyo, mshitakiwa akiwa katika mkutano wa kidini kwenye Msikiti wa Thaqi B, alitamka maneno ya uchochezi yaliyosema: "Ardhi yetu inaelekea pazuri kwenda kuchinjana na makafiri, kwa hali hii kuchinja ni halali".

Alidai kuwa maneno hayo yalichochea chuki miongoni mwa Watanzania. Katika shitaka hilo, Imam huyo hakutakiwa kujibu lolote,kutokana na mahakana hiyo kutokuwa na mamlaka hadi hapo itakapopata ridhaa kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP).

Katika shitaka la pili, Lelo alidai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na shitaka la kuchochea uhalifu chini ya Kifungu 390 na 35 cha Sheria
ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alidai kuwa katika kipindi hicho cha Desemba mwaka jana hadi Februari mwaka huu katika Msikiti wa Thaqi B,akihutubia mkutano wa kidini,aliwachochea wasikilizaji kufanya uhalifu wa mauaji,ambao ni kosa chini ya Kifungu 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Alidai kuwa katika mkutano huo, mshitakiwa alitamka maneno "Ardhi yetu inaelekea pazuri kwenda kuchinjana na makafiri, kwa hali hii
kuchinjana ni halali". Mshtakiwa alikana shitaka hilo na kupelekwa rumande baada ya wakili wa Serikali, kuiomba Mahakama isimpatie dhamana.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 13, mwaka huu,ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa pingamizi la dhamana.

Wakati huo huo Polisi inaendelea kumsaka Mkurugenzi wa Kituo cha Redio cha Kwa Neema Fm,Askofu Augustino Mpemba pamoja na Shehe, Ilunga Kapunga wakituhumiwa kuchochea chuki za kidini.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alisema viongozi hao wa dini hawajapatikana. Alisema baada ya kufuatilia, Polisi ilibaini kuwa Shehe Ilunga yupo India kwa matibabu.

Kwa upande wa Mpemba ambaye ni Askofu wa Kanisa la Tanzania Field Evangelism,alisema hajulikani alipo.Aliwaomba raia wema wenye taarifa za askofu huyo, kutoa ushirikiano kwa polisi kueleza alipo.

Source. Habari leo.

Kwa mwendo huu Wachochezi watahubiria kutokea mapangoni.
 
  • Thanks
Reactions: ADK
sERIKALI NDIO INAAMKA SASA BAADA YA MAUAJI NA UHARIBIfu


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
mbona mtaani kwetu kuna jamaa anaweka hizo cd tena kwa sauti kubwa na hajafanywa kitu?
 
Askoff hana tatizo lolote wanataka kumkamata ili ku balance na shehe ilunga,wameona wakimkamata ilunga pekee inaweza amsha hasira za waislaam
 
Hakimu ni Mkristo hawezi kuhukumu kwa kuzingatia sheria! ni lazima atawadhulumu watuhumiwa wa Kiislamu hivyo panahitajika mahakimu 2 Muislamu na Mkiristo ili kuleta balance! Mashehe wote waliokamatwa hawana budi kugoma kuhukumiwa na Mahakimu wakristo pekee!
 
Hakimu ni Mkristo hawezi kuhukumu kwa kuzingatia sheria! ni lazima atawadhulumu watuhumiwa wa Kiislamu hivyo panahitajika mahakimu 2 Muislamu na Mkiristo ili kuleta balance! Mashehe wote waliokamatwa hawana budi kugoma kuhukumiwa na Mahakimu wakristo pekee!

mkuu Tanzania Kwanza,hahukumiwi na hakimu bali sheria ndio inamhukumu,nijuavyo mimi hakimu yuko pale kuitafsiri sheria,hivyo km wakipatikana na hatia watahukumiwa kwa mujibu wa sheria na sio kwa mujibu wa utashi wa hakimu.
 
Last edited by a moderator:
Sawa japo mamlaka imechewa kudhibiti hadi roho a watu zimepotea. La kujiuliza ni kwa nini mamlaka imewaachia waislamu wachache kukejeli ukristo kwa muda mrefu bila kuchukuliwa hatua hadi baadhi ya wakristo kuanza kujibisha. Hili jambo la dini kustahimiliana na kuheshimiana si la pande moja. Hakuna dini yenye hati miliki na mungu, lazima kabisa kuheshimiana. Imani za dini zinaahidi pepo ya milele, hakuna atakayekubali njozi yake ya pepo ya milele eti ni fake.
 
Then kipindi hiki wakiandamana FFU tumieni kitimoto kuwapoza njaa then kamateni na pelekeni ndani wakaungane na ponda.
 
Huyo Imamu achunguzwe jee huwa anafadhiliwa na nani kufanya shughuli zake za uchochezi akiwa hapo Mwanza?maana wakati mwingine hawa watu wenye uwezo wao kifedha ndio wanaoleta mambo hayo wakiwa nyuma ya pazia.
 
Inatia huruma kwa watu kutoa kauli bila kujua madhara yake
 
mkuu Tanzania Kwanza,hahukumiwi na hakimu bali sheria ndio inamhukumu,nijuavyo mimi hakimu yuko pale kuitafsiri sheria,hivyo km wakipatikana na hatia watahukumiwa kwa mujibu wa sheria na sio kwa mujibu wa utashi wa hakimu.

You are playing a guitar to a goat mkuu. Huyo jamaa ni taahira No. 1 hapa J4, we all know so.
 
Last edited by a moderator:
Wao hudai hupata thawabu kwa alah.

Hudai hivyo kwakuwa hawajui nini hasa hutokea baada ya kifo .Ingependeza kama dini zote zingekuwa zinafundisha watu wake kupenda watu wote bila kujali imani zao nasiyo ilivyo baadhi wanajiona dini fulani ni safi kuliko zote
 
Hakimu ni Mkristo hawezi kuhukumu kwa kuzingatia sheria! ni lazima atawadhulumu watuhumiwa wa Kiislamu hivyo panahitajika mahakimu 2 Muislamu na Mkiristo ili kuleta balance! Mashehe wote waliokamatwa hawana budi kugoma kuhukumiwa na Mahakimu wakristo pekee!

Kalagabaho wee!!, Na mgome kusoma shule zilizojengwa na kanisa na kutibiwa kwenye hospitali za kanisa.
 
Haaah haaah haaaah !
Askofu wa KWA NEEMA FM - Mwanza, hajulikani alipoo.....

Nimeipenda hiiyooo
 
Kalagabaho wee!!, Na mgome kusoma shule zilizojengwa na kanisa na kutibiwa kwenye hospitali za kanisa.

Nimeanza kugundua uwezo wa akili zako kumbe unatumia " masaburi " kwani hizo huduma wanapata bure ?

Kwani kama Waislam nao wangekuwa wanapewa fedha na Serikali katika kuendesha shughuli zake kama MKATABA WA MOU unavyosema wasingekuwa na Hospital zao ?

Think BIG !
 
Hakimu ni Mkristo hawezi kuhukumu kwa kuzingatia sheria! ni lazi
ma atawadhulumu watuhumiwa wa Kiislamu hivyo panahitajika mahakimu 2 Muislamu na Mkiristo ili kuleta balance! Mashehe wote waliokamatwa hawana budi kugoma kuhukumiwa na Mahakimu wakristo pekee!

kwa kuzingatia sharia au sheria.!
 
Hawa ndugu zetu wana matatizo gani kwani?
Hawawezi kuifanya hii nchi kuwa mahala safi pa kuishi bila vurugu na chuki za kidini?
kila kukicha hili ndo limekua gumzo sasa.
Aaaaaarrrggghhhhhh......

IMAM wa Msikiti wa Thaqi B,Hamza Omary (37) maarufu kama Mohamed amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza,akikabiliwa na mashitaka mawili ya uchochezi.

Alifikishwa mahakamani hapo jana mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Godfrey Mwambapa.Wakili wa Serikali, Felista Lelo alidai kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo kati ya Desemba mwaka jana na Februari mwaka huu katika Msikiti wa Thaqi B wilayani
Nyamagana jijini Mwanza.

Katika shitaka la uchochezi,Wakili alidai Imam huyo anadaiwa kuchochea chuki kwa nia ovu chini ya Kifungu Namba 63 B (i) (ii) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alidai katika kipindi cha miezi hiyo, mshitakiwa akiwa katika mkutano wa kidini kwenye Msikiti wa Thaqi B, alitamka maneno ya uchochezi yaliyosema: "Ardhi yetu inaelekea pazuri kwenda kuchinjana na makafiri, kwa hali hii kuchinja ni halali".

Alidai kuwa maneno hayo yalichochea chuki miongoni mwa Watanzania. Katika shitaka hilo, Imam huyo hakutakiwa kujibu lolote,kutokana na mahakana hiyo kutokuwa na mamlaka hadi hapo itakapopata ridhaa kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP).

Katika shitaka la pili, Lelo alidai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na shitaka la kuchochea uhalifu chini ya Kifungu 390 na 35 cha Sheria
ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alidai kuwa katika kipindi hicho cha Desemba mwaka jana hadi Februari mwaka huu katika Msikiti wa Thaqi B,akihutubia mkutano wa kidini,aliwachochea wasikilizaji kufanya uhalifu wa mauaji,ambao ni kosa chini ya Kifungu 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Alidai kuwa katika mkutano huo, mshitakiwa alitamka maneno "Ardhi yetu inaelekea pazuri kwenda kuchinjana na makafiri, kwa hali hii
kuchinjana ni halali". Mshtakiwa alikana shitaka hilo na kupelekwa rumande baada ya wakili wa Serikali, kuiomba Mahakama isimpatie dhamana.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 13, mwaka huu,ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa pingamizi la dhamana.

Wakati huo huo Polisi inaendelea kumsaka Mkurugenzi wa Kituo cha Redio cha Kwa Neema Fm,Askofu Augustino Mpemba pamoja na Shehe, Ilunga Kapunga wakituhumiwa kuchochea chuki za kidini.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alisema viongozi hao wa dini hawajapatikana. Alisema baada ya kufuatilia, Polisi ilibaini kuwa Shehe Ilunga yupo India kwa matibabu.

Kwa upande wa Mpemba ambaye ni Askofu wa Kanisa la Tanzania Field Evangelism,alisema hajulikani alipo.Aliwaomba raia wema wenye taarifa za askofu huyo, kutoa ushirikiano kwa polisi kueleza alipo.

Source. Habari leo.

Kwa mwendo huu Wachochezi watahubiria kutokea mapangoni.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom