Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,462
- 154,332
WAZIRI Mwadini (38), mkazi wa Oysterbay, amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni kujibu shitaka la kumshambulia askari na kumtukana matusi ya nguoni.
Imedaiwa na Karani Fatma Khatibu Mbele ya Hakimu Mary Matoi kuwa Januari 1, mwaka huu, mshitakiwa alimshambulia askari namba G 789 Konstebo Alfred na kumsababishia maumivu.
Mshitakiwa amekana mashitaka na kesi hiyo itatajwa tena Februari 18, mwaka huu.
Pia, Marco Maiko (31), mkazi wa Masaki amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni kujibu mashitaka ya shambulio.
Mbele ya Hakimu Mariamu Masamalo imedaiwa na Karani Emakulatha Philipo kuwa Novemba 24, mwaka jana, mshitakiwa alimshambulia mlalamikajiMusa Abdallah na kumsababishia maumivu.
Mshitakiwa amekana mashitakana kesi hiyo itatajwa tena Februari 16, mwaka huu.
Imedaiwa na Karani Fatma Khatibu Mbele ya Hakimu Mary Matoi kuwa Januari 1, mwaka huu, mshitakiwa alimshambulia askari namba G 789 Konstebo Alfred na kumsababishia maumivu.
Mshitakiwa amekana mashitaka na kesi hiyo itatajwa tena Februari 18, mwaka huu.
Pia, Marco Maiko (31), mkazi wa Masaki amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni kujibu mashitaka ya shambulio.
Mbele ya Hakimu Mariamu Masamalo imedaiwa na Karani Emakulatha Philipo kuwa Novemba 24, mwaka jana, mshitakiwa alimshambulia mlalamikajiMusa Abdallah na kumsababishia maumivu.
Mshitakiwa amekana mashitakana kesi hiyo itatajwa tena Februari 16, mwaka huu.