She is not special

Kama hayo maneno uliyoweka quote ameongea jamaa,basi nakubaliana nae asilimia 100.

Kuna wanawake ili uwapate basi inabidi ujiupgrade wewe mwanaume ili ufikie viwango vyake. Hapa nazungumzia katika level ya kiuchumi kama amekuzidi.

Mwanamke akishakuwa na uchumi mkubwa ,gari Kali,nyumba ya mamilioni na mwonekano wa HD( mrembo aliyepita viwango vya uzuri wa kawaida) automatically anapunguza wanaume kumfuatilia.

Yaani anakuwa kama mlimani city ilivyopunguza au kuchuja masikini,kwa sababu masikini wanaogopa vioo (uzuri na gharama ) na mambo kama hayo.

Mfano kwenye story ya Member INSIDER MAN ,jamaa mmoja Ambae alikuwa ni Mwarabu ana Mali za mafuta Dubai, na Bongo ana biashara pamoja na utajiri wote alikuwa anamgwaya mwanamke main character wa kwenye ile story.

Kwa sababu alipotaka kwenda kwa gia ya Hela/ ukwasi akashauriwa na jamaa kuwa huyo Binti hata umuonge milioni mia hawezi kukukubali kwa hiko kigezo maana yeye mwenyewe ana Hela chafu Mwarabu akagwaya na mihela yake.

Nakubaliana na wewe kuwa hakuna mwanamke special ila kwanza hakikisha mwanaume uwe umeinuka kiuchumia maradufu(pesa inaleta security na authority) kumzidi huyo manzi. Vinginevyo akupende yeye bila kuzingatia uchumi wako.

Mfano yule jamaa wa Arusha anayetrend mitandaoni kupendwsa na ile pisi Kali muuza nguo. Jamaa kaangukiwa tu na zali la mentally.
 
1. Katika maisha ogopa sana kitu kinaitwa HISIA,- HISIA haina class wala speciality yoyote
-ndiyo maana waweza kuta mwanaume imara, lakini ana mwanamke anafanana na ufunguo wa magereza
-au unakuta mwanamke yupo vizuri lakini anabeba mwanaume hana pesa(wakati mwingne anatunzwa) na ana sura haieleweki kama namba za four figure ya form two...hisia hisia ni kitu ambacho kinaweza kukuuwa au kukuhuisha katika mapenzi.

2. kinachosabbisha umuone ni special ni kutokana na umbali wa kumfikia, lakini ukiwa karibu hana uspecial wowote na analika vizuri

3. umaskini wetu wanaume ni janga letu
-huwezi kuwa unashindia mawashio(furu na dagaa) upate akili ya kuwazia mademu wengne zaid ya kuwaza pesa ya kununua nyama.

4.mwanamke special ni yule

-uliye naye kwenye ndoa (hakika mjali)

-aliyekuzalia au aliyetayari kukuzalia kiumbe

-anayekupenda, kusamehe mnapokosea, kukujali, anayekubebea madhaifu, anayekutunzia siri

hapa kwenye bikra, busara inanituma kunyamaza, nisije kosea hawa viumbe.
 
Sasa hao waliojipata ndio wazuri kuwapata maana yeye anakuelewa kikweli kidume

Manzi masikini hata akikuambia anakupenda unashindwa kuelewa anamaanisha au ni njaa inamsumbua
 
Hivi ni kwanini ukiwa unatembea, njiani kukiwa na mavi/kinyesi ni lazima ukione na usipokiona ni lazima ukikanyage?

Yani hakiwezi kukuacha salama
Au mtu akiziba pua na kutema mate,unajua kabisa huyu ameona mavi au ameona kitu kibaya kilichooza na kinanuka vibaya mno na wewe harufu unaiskia na huipendi.

Ila cha ajabu moyo unakuwa hautulii hadi macho yatafute hayo mavi au mzoga kisha na wewe uone ndiyo ulidhike.

Saikolojia ya binadamu ni ya ajabu.
 
Sasa hao waliojipata ndio wazuri kuwapata maana yeye anakuelewa kikweli kidume

Manzi masikini hata akikuambia anakupenda unashindwa kuelewa anamaanisha au ni njaa inamsumbua
Lakini itakuwa haujaelewa context yangu Wala ya makaveli10 .

Nakubaliana na wewe katika hoja yako ila ukweli ni kuwa wapo wanawake ni level ambazo kuwapata inakuwa mtiti.

Maana kigezo kikuu cha kumpata mwanamke ni Hela,gari kali na cheo.

Sasa unakuta huyo mwanamke ana Kila kitu Tena pengine amekuzidi. Yaani amekuzidi hadi exposure ya maisha. Mwanaume automatically unakuwa unafeel inferiority complex.

Hakuna mwanamke anapenda awe namwanamke aliyemzidi.
 
Katika mfumo wa ubepari lazima utafute class yako, ukikata utaendelea kuishi kwenye "life of denial", we mkilima wa vitunguu Sigida kijijini, ni ngumu kupata mazingira ya kumpata mtoto wa bakhresa au Kikwete umtongoze na atimae umoe ni vigumu sana. ni rahisi kua Nabii wa walokole kuliko wewe kuoa mtoto wa Raisi kwa mfumo hu wa capitalism.
 
Sasa unakuta huyo mwanamke ana Kila kitu Tena pengine amekuzidi. Yaani amekuzidi hadi exposure ya maisha. Mwanaume automatically unakuwa unafeel inferiority complex.
Hii ni wewe tu mkuu usiwazungumzie wanaume wote wanaofeel inferiority complex kwa aina hiyo ya wanawake

Mbona tuna mifano mingi ya wanawake waliotokea familia za high class na wao mamanzi wamejipata

Na bado wanafanya maisha na wana kutoka life la kawaida
 
Wanaume tunajifelisha sana, inakuwaje mwanaume kutoka familia za kitajiri wanaoa mademu kutoka familia za kawaida kiuchumi na hata status?

Mapenzi hisia
 
Very nice observation
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…