Shambulio la Lissu kupigwa risasi: Polepole aibua mapya

Shambulio la Lissu kupigwa risasi: Polepole aibua mapya

Hajui mambo gani yanayoitaji siasa na yapi yasiyoitaji siasa huyu mpuuzi.
 
Upande mmoja unang'ang'ania cctv na upande mwengine unamtaka dereva, Trump ataendelea kututukana sana tu.
 
Kwa sasa mi naona vyama vyote sawa tu si ccm wala chadema. Sasa mfano CCM inalaumiwa sawa ila CHADEMA nao wakiguswa wanang'aka. Mfano kwa uelewa wangu naamini shahidi wa kwanza kwenye tukio la Lisu ni dereva wake huyo ndiye ambaye anaweza hadithia picha zima maana yeye ni almanusura,kwa hiyo kama uchunguzi unaanzia hapo. Sasa makamanda sijui hofu yao nini?
Naona Polepole yuko sahihi tuu.
 
polepole.jpg

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenenzi, Humphrey Polepole amefunguka na kuhoji kuhusu kitendo cha Chadema kumficha dereva aliyeshuhudia tukio zima la shambulio la risasi kwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na amewataka wananchi wa jimbo la Siha kumhoji Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aeleze sababu za kufanya hivyo.

Ametaka kuhoji siri iliyopo inayowafanya Chadema wamfiche dereva huyo wakati anahitajika kuisaidia Serikali kufumbua ukweli na kumjua aliyehusika katika shambulio hilo

Hivi huyu polepole yupo timamu kweli? Akipatikana dereva wa lissu hao watu wasiojulikana watapatikana baada ya kuhojiwa? Vipi dereva wa lissu angekufa ktk shambulio lile ina maana intelijensia ya jeshi la polisi ingekuwa nayo imekwisha?

Siasa za ccm kupitia huyu jamaa ni mufilisi kabisa.
Pole pole si mwendo.
 
Naona Polepole yuko sahihi tuu.
Kuwa kwenye tukio katika hali kama ile unadhani ameona kila kitu. Vipi akisema kama alivyokwisha kusema nini kitaongezeka. Kwenye tukio la Lissu kati ya Kamera za CCTV na huyo dereva wa Lissu mnayedai kwamba ni "shahidi muhimu" ushaidi wa hakika upo wapi, kwa dereva ama kwa hiyo CCTV iliyong'olewa?
 
Angeanza kwanza kueleza ni akina nani walio amuru:
1.kung'olewa kwa cctv camera pale area D.
2.kuondolewa kwa askari waliokuwa lindo siku ya tukio pale area D.
Pia aeleze je ni kweli watu wasiojulikana wana mkono mrefu kuliko serikali?
Kumsikiliza polepole kunahitaji busara.
 
kama dereva mmemficha mnashindwaje kuiba kamera za cctv
jibun swali aliyeshambuliwa tunamwona kwenye tv lakin dereva yupo wapi yeye ndio shahidi wa pekee
Camera za cctv zilinasa images za hao wahalifu wakiwa wameficha sura zao kwa kofia na miwani myeusi. Dreva wa Lissu anawafahamu vizuri sana wale waliokuwa wanamfuatilia Lissu huko Dar. Sasa kwa nini anakataa kwenda polisi kuziona hizo images zilizonaswa na camera za CCTV na kuona kama ni zile za watu waliokuwa wanawafuatilia kule Dar? Kwa nini anakataa kuambatana na polisi katika kuwasaka watu hao huko mitaani kwani yeye pekee ndiye anawafahamu kwa sura watu hawa. Kukataa kwake kunaitia doa chadema kama anavyolalamika mjane wa Wangwe! Chama kinapaswa kuondoa madoa doa haya kwa kuhakikisha dereva huyu anaenda kuisaidia polisi kwenye upelelezi wa suala hili. Polepole yuko sahihi ku point out madoa doa haya ya mpinzani wake.
 
Camera za cctv zilinasa images za hao wahalifu wakiwa wameficha sura zao kwa kofia na miwani myeusi. Dreva wa Lissu anawafahamu vizuri sana wale waliokuwa wanamfuatilia Lissu huko Dar. Sasa kwa nini anakataa kwenda polisi kuziona hizo images zilizonaswa na camera za CCTV na kuona kama ni zile za watu waliokuwa wanawafuatilia kule Dar? Kwa nini anakataa kuambatana na polisi katika kuwasaka watu hao huko mitaani kwani yeye pekee ndiye anawafahamu kwa sura watu hawa. Kukataa kwake kunaitia doa chadema kama anavyolalamika mjane wa Wange! Chama kinapaswa kuondoa madoa doa haya kwa kuhakikisha dereva huyu anaenda kuisaidia polisi kwenye upelelezi wa suala hili.
Umeingilia fani usiyoijua sasa unatoa pumba tu. Yaani akitoa maelezo au huo unaoita utambuzi ndo ataamriwa kuambatana na askari mtaani kuwasaka wahalifu? Akili za Madoctor Wa Tanzania ni za ajabu kweli. Kwa hiyo na wewe doctor!!?
 
Umeingilia fani usiyoijua sasa unatoa pumba tu. Yaani akitoa maelezo au huo unaoita utambuzi ndo ataamriwa kuambatana na askari mtaani kuwasaka wahalifu? Akili za Madoctor Wa Tanzania ni za ajabu kweli. Kwa hiyo na wewe doctor!!?
Bosi wake pia ni Dokta,ushuzi at its peak.
 
polepole.jpg

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenenzi, Humphrey Polepole amefunguka na kuhoji kuhusu kitendo cha Chadema kumficha dereva aliyeshuhudia tukio zima la shambulio la risasi kwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na amewataka wananchi wa jimbo la Siha kumhoji Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aeleze sababu za kufanya hivyo.

Ametaka kuhoji siri iliyopo inayowafanya Chadema wamfiche dereva huyo wakati anahitajika kuisaidia Serikali kufumbua ukweli na kumjua aliyehusika katika shambulio hilo

Hivi huyu polepole yupo timamu kweli? Akipatikana dereva wa lissu hao watu wasiojulikana watapatikana baada ya kuhojiwa? Vipi dereva wa lissu angekufa ktk shambulio lile ina maana intelijensia ya jeshi la polisi ingekuwa nayo imekwisha?

Siasa za ccm kupitia huyu jamaa ni mufilisi kabisa.

maswali mazuri, na kweli anaweza kuwa hana akili timamu! ila ndio kasema, wako watakao amini, wako ambao nao WANAJULIZA kama yeye!
 
Nikishapoteza imani na mtu huwa sitaki kumwongelea,wala hata kumsikia tu,kama huyu mkomao
 
Kwa hiyo ahadi kwa wana Siha ni kumtafuta Dereva wa Lisu

[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] mkuu nadhani wamemaliza hapo ndio sera na ndio ahadi
 
kama dereva mmemficha mnashindwaje kuiba kamera za cctv
jibun swali aliyeshambuliwa tunamwona kwenye tv lakin dereva yupo wapi yeye ndio shahidi wa pekee

Mkuu kinachozuia uchunguzi wa kupotea kwa Ben Saa Nane ni nini? N yule aliyemyooshea bastola Nape Nauye mbona amenaswa na media na kuanikwa kwenye mitandao mbona hajakamatwa? Au pia kikwazo ni wakina Mbowe. Alie vamia Clouds Media na watu wenye silaha mbona hajakamatwa wala kufikishwa mahakamani? Au pia kikwazo ni wakina Mbowe? Polepole anajua ngoma wameipiga wenyewe na wanaicheza wenyewe, si muda mrefu maaibika.
 
Huyu jamaa heshima aliyojijengea wakati wa kukusanya maoni ya katiba mpya kaivunja kabisa sasa hivi anaonekana ni boya tu kumbe jinga jinga
 
Back
Top Bottom