Shamba langu. Bustani ya ndoto zangu

Shamba langu. Bustani ya ndoto zangu

FB_IMG_1758171408467.jpg
 
Je wajua ya kwamba ndoto zaweza kuwa kweli? Wazungu wanasema dreams can come true...

Fanya yote maishani.. Pambana sana lakini usiache kumwomba Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema zote akujaalie mwisho mwema, uzee uliojaa fanaka na baraka.. Tele.. Wanazengo wanasema fainali uzeeni.. Basi Mwombe sana Manani akutunuku fainali ya ushindi.. Sio ya kutoa suluhu wala kufungwa..!

Pamoja na yote utakayojaaliwa pata walau hekari moja ukikosa kabisa basi walau nusu yake .. Kishapo
Jenga kajumba kako kazuri sana.. Huhitaji ghorofa wala nyumba kubwa utafuga majini na mashetani bila

kutaka na bila kujua
Fuga mifugo yako michache
1. Ng'ombe wa maziwa mmoja wakizidi wawili
2. Kuku wawili watatu wa mayai wa kienyeji
3. Ukiweza na ukipenda fuga na bata au sungura
4. Bwawa dogo la samaki
5. Fuga njiwa ukiweza na kasuku na ndege wengine wa leisure
Hii mifugo yote
Hawa wote watakusaidia sana kwenye ishu ya mbole
Kuzunguka nyumba una bustani zako za maua, garden na miti ya vivuli
Huko shambani sasa unatenga eneo la shamba dogo mazao mixer miti ya matunda.. Eneo lililobaki bustani za mbogamboga..
Utahitaji kisima pia
Pengine utahitaji vijana wawili watatu wa kukusaidia
Utahitaji chumba/ghala lenye vitendea kazi vyote...
Eat well.. Eat fresh.. Na kamnywesho kidogo😀😀😀View attachment 3261641View attachment 3261642View attachment 3261643View attachment 3261644
Mkuu hizo hizo Jack Daniels zipo nnavotoka mdaula kabla sijafika bagamoyo nishukie hapo nijipoze kidogo
 
Sawa Mkuu hope next time muda ukipatikana walau tutakaa tukinywa na kujadili mwelekeo wa Taifa na sisi watu wake
Amina mkuu tuombeane afya na sifa njema! Nitakuja na kitu ya Mao ste Tungu 56%😂
 
Back
Top Bottom