Shamba la Sumaye kufutiwa hati

Shamba la Sumaye kufutiwa hati

Francis12

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2016
Posts
7,533
Reaction score
22,285
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imenza rasmi mchakato wa kumnyang’anya shamba Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye kwa kulimiliki muda mrefu bila kuliendeleza.

Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri mwenye dhamana, William Lukuvi alisema kuwa tayari wameshampa notisi kisheria na kinachosubiriwa ni sahihi ya Rais John Magufuli kuhalalisha uamuzi huo.

”Kama wewe ulifikiri kwa sababu ni Waziri Mkuu hatutachukua hatua, sasa umejibiwa kwamba tumechukua na Ofisa aliyechukua hatua yule pale,” alisema Waziri Lukuvi. ”Sisi katika utendaji wetu hatuangalii sura ya mtu,” aliongeza.

Shamba hilo linaloingia mikononi mwa Serikali, ni lile liliko katika eneo la Mwabwepande jijini Dar es Salaam ambalo mwishoni mwaka jana, wananchi waliobomolewa nyumba zao walilivamia na kujenga.

Aidha, Waziri Lukuvi aliwataka wananchi kutojichukulia hatua ya kuvamia maeneo yaliyokaa muda mrefu bila kuendelezwa badala yake watoe taarifa wizarani ili hatua za kisheiria zifuatwe.

Alisema kwa kawaida notisi hiyo hutolewa kwa mhusika na baada ya siku 90 hupelekwa wizarani kwa ajili ya kuiwasilisha kwa Rais ambaye atachukua uamuzi kwa kushauriwa na wizara hiyo.

Sumaye aliwahi kueleza kuwa ameliacha eneo kwani lengo lake ni kujenga chuo kikuu na sio vinginevyo. Aliweka wazi nia yake ya kufika mahakamani endapo atanyang’anywa eneo hilo.


Chanzo: Dar 24
 
Viongozi wengi sana walijitwalia Mashamba, au wanaanza kwanza na Sumaye kama alivyosema wanaanza kwanza na Mbowe japo wapo wengi, lakini mpaka leo sijasikia yoyote mkubwa akitolewa vitu vyake National Housing. We need to think big.
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Lukuvi amesema, shamba hilo lipo kwenye hatua ya kufutwa hati yake na kusisitiza, serikali haitavumilia watu wanaomiliki mashamba bila kuyafanyia kazi.
“Shamba la Sumaye hati yake iko katika hatua za kufutiwa,” amesema Lukuvi na kusisitiza “serikali haitofumbia macho watu wanaomiliki ardhi pia mashamba ambayo hawayaendelezi.”
Tayari Rehema Mwinuka, Ofisa Ardhi wa wilaya hiyo ameandika barua ya notisi kuelekea kutekeleza kutwaa eneo hilo la Sumaye.
Hata hivyo, Lukuvi amewataka watu wanaomiliki ardhi kwa kuwa na karatasi za ofa halali, wazibadilishie ili wapewe hati halali.
Amesema, kuwa kinachoonekana kwa sasa ni kuwa, asilimia 60 ya migogoro ya ardhi, chanzo chake ni karatasi za ofa za Halmashauri jiji na manispaa na kwamba, wametoa miezi mitatu kwa wenye karatasi za ofa kubadilishwa.
Chanzo Mwanahalisi

Mhhhh hii kali ulitaka kusemaje?
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Lukuvi amesema, shamba hilo lipo kwenye hatua ya kufutwa hati yake na kusisitiza, serikali haitavumilia watu wanaomiliki mashamba bila kuyafanyia kazi.
“Shamba la Sumaye hati yake iko katika hatua za kufutiwa,” amesema Lukuvi na kusisitiza “serikali haitofumbia macho watu wanaomiliki ardhi pia mashamba ambayo hawayaendelezi.”
Tayari Rehema Mwinuka, Ofisa Ardhi wa wilaya hiyo ameandika barua ya notisi kuelekea kutekeleza kutwaa eneo hilo la Sumaye.
Hata hivyo, Lukuvi amewataka watu wanaomiliki ardhi kwa kuwa na karatasi za ofa halali, wazibadilishie ili wapewe hati halali.
Amesema, kuwa kinachoonekana kwa sasa ni kuwa, asilimia 60 ya migogoro ya ardhi, chanzo chake ni karatasi za ofa za Halmashauri jiji na manispaa na kwamba, wametoa miezi mitatu kwa wenye karatasi za ofa kubadilishwa.
Chanzo Mwanahalisi

Please tell Lukuvi kuwa right of occupancy is created after issuance of an offer and acceptance of the same and conditions such as paying fees etc. by the offeree. Certificate of occupancy is a document merely for registration purpose but ownership is created once a letter of offer is accepted by offeree and fulfillment of conditionalities
 
->kisa yupo upinzani/ poor poor poor/ don't do that make a compromise first followed with warning letters on developing the area.//
 
Hivi serikali imeliona Shamba la Sumaye tu kule Mabwepande? Mbona kuna watu wana maeneo makubwa wamepima viwanja havijaendelezwa ni mapori wanasubiri kuviuza lakini hawanyang'anywi Kwa kuwa wako CCM?
 
Back
Top Bottom