Mokes Junior
Member
- Aug 20, 2022
- 7
- 0
CHINI YA MPARACHICHI.
1 Kivuli chake kitamu, mfaidi hafaidi
parachichi zake tamu, wengine wanafaidi
matunda yake ni sumu, tiba yao makuadi
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
2 Matunda yakikomaa, mzee huwa mkali
unaweza kulemaa, ukimwambia ukweli
maisha ya ujamaa, yalishakwenda na meli
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
3 Sifa zake naskia, matunda wakisifia
wanadai yavutia, matamu kuyabugia
mdomoni kuyatia, sijawahi ambulia
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
4 Majaniye kudondoka, taka taka kuongeza
fagio wenye mashaka, kusafisha naumiza
maneno nayo sadaka, ukweli unajiweza
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
5 Anajali marafiki, wanae kutudhihaki
hataki tukate keki, rafiki hababaiki
watoto twalia dhiki, lawama hazikwepeki
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
6 Mkweli hawezi dumu, daima kumdhulumu
ukweli hatari sumu, darasa bila kalamu
kushindia vuta ndumu, daima kosa nidhamu
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
7 Urithi wetu shakani, hatuoni ahueni
uhuru wetu shambani, unasubiri hisani
hakuna kwenda sokoni, mfadhili mlangoni
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
8 Barafu siyo kinywaji, hata ukila hushibi
tunataabika maji, nyumbani shamba la bibi
tunashindwa pata uji, kelele zenu kinubi
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
1 Kivuli chake kitamu, mfaidi hafaidi
parachichi zake tamu, wengine wanafaidi
matunda yake ni sumu, tiba yao makuadi
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
2 Matunda yakikomaa, mzee huwa mkali
unaweza kulemaa, ukimwambia ukweli
maisha ya ujamaa, yalishakwenda na meli
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
3 Sifa zake naskia, matunda wakisifia
wanadai yavutia, matamu kuyabugia
mdomoni kuyatia, sijawahi ambulia
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
4 Majaniye kudondoka, taka taka kuongeza
fagio wenye mashaka, kusafisha naumiza
maneno nayo sadaka, ukweli unajiweza
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
5 Anajali marafiki, wanae kutudhihaki
hataki tukate keki, rafiki hababaiki
watoto twalia dhiki, lawama hazikwepeki
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
6 Mkweli hawezi dumu, daima kumdhulumu
ukweli hatari sumu, darasa bila kalamu
kushindia vuta ndumu, daima kosa nidhamu
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
7 Urithi wetu shakani, hatuoni ahueni
uhuru wetu shambani, unasubiri hisani
hakuna kwenda sokoni, mfadhili mlangoni
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.
8 Barafu siyo kinywaji, hata ukila hushibi
tunataabika maji, nyumbani shamba la bibi
tunashindwa pata uji, kelele zenu kinubi
Chini ya mparachichi, nadondokewa na mawe.