SGR vs BMW x3 F25

SGR vs BMW x3 F25

Hiyo 160 km/h itapatikana on average au zaidi. Bmw x3 inakwenda mpaka 260 km/h. Na kufikia 160 km/h kwa Bmw x3 ni kugusa tu ambapo SGR inachukua muda kidogo kufikia hiyo speed

hiyo siyo ishu, nafikiri mada inahusu mazingira ya tanzagiza kama yalivyo sasa hivi hauwezi kuendesha gari 160 km/h kwa zaidi ya 100 km constantly kwa maana tanzagiza hakuna 4-lane highway system kwanza max. speed allowed by law in tanzagiza ni 100km/h vs sgr inaweza kwenda hiyo speed 160km/h +/- labda itasimama stesheni tu na baada ya hapo mwendo ni ule ule

bottomline: kwa gari hauwezi kuwa faster klk sgr kwa tanzagiza na haijalishi aina ya gari ...
 
Hiyo 160 km/h itapatikana on average au zaidi. Bmw x3 inakwenda mpaka 260 km/h. Na kufikia 160 km/h kwa Bmw x3 ni kugusa tu ambapo SGR inachukua muda kidogo kufikia hiyo speed
Mkuu ushapanda SGR train? Haichujui muda kugusa 160kph. Umeme huo ni kusukuma throttle tu. Hio BMW tatizo ni barabara na mazingira yake. Wataishia nyuma ya Lori wakifanya mchezo.
 
Hahaha. Hapana mkuu. Akili kisoda hao. Labda ingekua straight line, ndio wangesema wajaribu ila ukiangalia matuta, foleni, trafiki, barabara mbovu, kona, hainamke sense.. ata ukijitahidi sana ukatumia 8 hours wewe umeendesha vibaya sana na risk ni kubwa sana..
Masaa 8 dodoma Dar kwa mkimbiaji??hapana mengi sana....Mimi sio mtu wa mashindano ila kama mtu Ana kibunda tubet,hayo masaa natoboa...
 
Naijua vizuri sana. Ilichangia kunifilisi. Ikikuwashia taa nyekundu kwenye dashboard kama Christmas tree ndiyo utajua hujui mpaka uje kuzizima. Nilimiliki hiyo ndinga ndani ya miezi saba nikafilisika na kuiuza kwa bei ya hasara. Wanaozijua wengi hawanunui hata bei ushushe kiasi gani.
Ila kwa speed ni balaa aisee
Ulimiliki ya mwaka gani mkuu ya 2025 Tanzania zipo chache sana na pia ya 2025 diesel inanusa mkuu inatumia sana umeme ni kama Ford ranger tu..sema bmw za kitambo mafuta uwe na kisima nyumbani..
 
Ulimiliki ya mwaka gani mkuu ya 2025 Tanzania zipo chache sana na pia ya 2025 diesel inanusa mkuu inatumia sana umeme ni kama Ford ranger tu..sema bmw za kitambo mafuta uwe na kisima nyumbani..
Mkuu ya mwaka 2025 ntaiwezea wapi, hahaha huu utani sasa. Kweli mafuta na spare si mchezo, ni ghari sana. Hizi gari ni kwa wale ndani ana gari mbili au tatu za kuchagua. Nilinunua kama showoff tu.
 
Mkuu ya mwaka 2025 ntaiwezea wapi, hahaha huu utani sasa. Kweli mafuta na spare si mchezo, ni ghari sana. Hizi gari ni kwa wale ndani ana gari mbili au tatu za kuchagua. Nilinunua kama showoff tu.
Hiyo gari ya mwaka jana parts utaanza kununua baada ya miaka minne sio leo wala kesho sio gari za kuulizia vipuri hizi ikianza kuharibika parts zishakua za kumwaga..
 
Masaa 8 dodoma Dar kwa mkimbiaji??hapana mengi sana....Mimi sio mtu wa mashindano ila kama mtu Ana kibunda tubet,hayo masaa natoboa...
Wewe huwa unatumia muda gani Dar Dodoma? Watu wanatumia muda mrefu kwasababu ya malori na ubovu wa barabara sasa hivi. Kutoka Moro kwenda Dodoma kuna mashimo mengi sana. Ukienda zaidi ya 100kph utapiga mashimo hadi akili ikukae sawa.
 
Wewe huwa unatumia muda gani Dar Dodoma? Watu wanatumia muda mrefu kwasababu ya malori na ubovu wa barabara sasa hivi. Kutoka Moro kwenda Dodoma kuna mashimo mengi sana. Ukienda zaidi ya 100kph utapiga mashimo hadi akili ikukae sawa.
Sijawahi ku drive dar to dodoma but last month dar to arusha kama nakuna nazi...na Toyota crown
 
Sijawahi ku drive dar to dodoma but last month dar to arusha kama nakuna nazi...na Toyota crown
Dar to Arusha njia haina malori mengi. Njia ta Dar Moro Dom unaweza kukutana na malori yameongozana 5km mbele yako.
 
Inawezekana wanachotakiwa kufanya ni kutafuta barabara ambazo hazipo bize kama vile za mikoani huko ambazo wanajitengea km zao ambazo zitakuwa na umbali Sawa wa Dsm to Dom starting time ziwe Sawa afu gari wanipe mimi niwe dereva kudadadeki sgr inakaa ni kama Kimi Antonelli on the Wheel
 
Masaa 8 dodoma Dar kwa mkimbiaji??hapana mengi sana....Mimi sio mtu wa mashindano ila kama mtu Ana kibunda tubet,hayo masaa natoboa...

Dar Dom kwa mwendo wa ngiri ni masaa 5 hapo...

Nilishwahi fanya hivyo na Vanguard, safari ilianza alfajiri saa 10 na madakika yake kabla ya mabasi ya mikoani, saa 12 na hivi ilinikuta Dumila huko...

Saa 3 kasoro asubuhi nilikuwa viunga vya Dodoma...

Siku hiyo niliacha "Kilimo kwanza" ikae mbele kuondoa longolongo ya kunguru weupe...
 
SGR muda mwingi linakua kwenye 160/hr hadi 170/hr

Barabara zetu hizi ku maintain 150/ kwa kilometa moja tu ni utata kabla hujakutana na Semi zinanyata, kidogo tuta, mara Najimunisa limetanua, mara msafara usio rasmi wa STL umetanua na full lights…….. utakuja kujikuta umetembea wastani wa 70/hr dhidi ya 160/ hr ya SGR
 
Back
Top Bottom