Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
I see, ni mara ya kwanza naleta tatizo langu kwenu wakuu.
Nina matatizo ambayo nahitaji ushauri wa haraka au wa kina ikiwezekana,.
Najisikia uchovu wa hali ya juu... Najisikia kucha kila aina ya kazi... Natamani kupumzika japo siku tatu tu niweze kurejea katika hali yangu ya kawaida.
Ugumu:
Nahitaji kuzima simu, kuwa mbali na pc kuwa mbali na familia yangu kabisa na kukaa alone kwa muda huo.
Si rahisi kuwambia familia kuwa nawaacha kwa muda huo, nahisi watajisikia vibaya.
Si rahisi kukaa mbali na JF, nikifanya hivyo nafsi inakuwa inanisuta all the times.
Si rahisi kuwaacha kwenye mataa makampuni manne ambao wameniajiri na kazi zao kulala siku moja kwao wanaona kama ndo mwisho wa makampuni yao (ilhali kuna wataalam wengi lakini wananikomalia).
Sina hamu na pesa zao hata kama wanasema wanavunja mkataba nami kwani mwili hauwezi kuvumilia hali niliyo nayo kwa sasa... Yani niko tayari kuacha na kupumzika liwalo na liwe.
Mbaya zaidi:
Nikiwa naendesha gari natamani kutokanyaga hata mafuta wala breki kwani nahisi vinanichosha mwili tu, nikiwa mbele kwenye foleni ya magari najikuta nimekuwa mwingi wa mawazo hata taa zikiruhusu nisipopigiwa kelele na wenzangu kushtukia inakuwa tatizo.
Je, wakuu nifanye nini???
Nina matatizo ambayo nahitaji ushauri wa haraka au wa kina ikiwezekana,.
Najisikia uchovu wa hali ya juu... Najisikia kucha kila aina ya kazi... Natamani kupumzika japo siku tatu tu niweze kurejea katika hali yangu ya kawaida.
Ugumu:
Nahitaji kuzima simu, kuwa mbali na pc kuwa mbali na familia yangu kabisa na kukaa alone kwa muda huo.
Si rahisi kuwambia familia kuwa nawaacha kwa muda huo, nahisi watajisikia vibaya.
Si rahisi kukaa mbali na JF, nikifanya hivyo nafsi inakuwa inanisuta all the times.
Si rahisi kuwaacha kwenye mataa makampuni manne ambao wameniajiri na kazi zao kulala siku moja kwao wanaona kama ndo mwisho wa makampuni yao (ilhali kuna wataalam wengi lakini wananikomalia).
Sina hamu na pesa zao hata kama wanasema wanavunja mkataba nami kwani mwili hauwezi kuvumilia hali niliyo nayo kwa sasa... Yani niko tayari kuacha na kupumzika liwalo na liwe.
Mbaya zaidi:
Nikiwa naendesha gari natamani kutokanyaga hata mafuta wala breki kwani nahisi vinanichosha mwili tu, nikiwa mbele kwenye foleni ya magari najikuta nimekuwa mwingi wa mawazo hata taa zikiruhusu nisipopigiwa kelele na wenzangu kushtukia inakuwa tatizo.
Je, wakuu nifanye nini???