Kitila,
Haya unayosema ni kweli na ninaamini kina mtatiro na wenzao wanasoma hapa. Migomo sio lazima itumike hata kwenye mambo ambayo yanaweza kuwa solved kwa mawasiliano mazuri. Kama nimeleewa story yako, angalau wewe serikali ilikuheshimu na kuahidi kukopa pesa toka NBC. Katika hii case sioni kama uongozi wa chuo ulikuwa na nia ya kupata suluhu na wanafunzi na msimamo ulikuwa ni kuwa chuo lazima kiamue nani awe kiongozi.
swali dogo kwako,
Je kipindi chenu uongozi wa chuo ulikuwa unaingilia chaguzi za wanafunzi kama Mkandara anavyotaka kufanya hapa?
Maghembe mnamuonea bure tu. Hata ingekuwa wewe tatizo hili lingekuwepo. Kuweni fair kidogo ktk ukosoaji wenu
hayo ndio madhara ya mgomo usio na akili...
Unajua wanafunzi wameshazoeshwa kwamba matatizo yao hayawezi kutatuliwa hadi wagome. Na ni kweli mara nyingi wakigoma hupata walichokuwa wakikitaka. So, it is the question of attitudes. Ndio yale yale tunayoongelea hapa kila siku: respect to the rule of law na ustaarabu. Ongeza na cha tatu sasa: ustahimilivu.
Jamii yetu imekuwa jamii isiyo na ustahimilivu. Hakuna patience kabisa. Wanafunzi wetu hawawezi kusibiri hata kidogo.
Na kuna udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa wanafunzi. Kuna faslafa ya kijinga kwamba ukiwa kiongozi wa wanafunzi unafuata wanachosema wanafunzi. Hii ni weakness kubwa na sio maana ya uongozi. Ukiwa kiongozi unakuwa na taarifa nyingi zaidi kuliko unaowaongoza kwa hiyo lazima uonyeshe njia.
Mimi nikakataa, nikawaambia sipo tayari kuongoza mgomo kwa sababu hatuwezi kuvumilia siku tatu wakati kuna watanzania wanashinda njaa kila siku. Nikawaambia wakati sisi tukisema hatuwezi kusubiri siku tatu, kuna watanzania walikuwa wamekufa na njaa kule Gairo. Nikawaambia wanafunzi wenzangu kuwa watanzania wangetudharau kwa kushindwa kuvumilia siku tatu tena tukisubiri utaratibu wa kawaida wa kibenki. Tukalumbana sana na mwisho nikwaambia kama mnaona ni lazima tuandame twende wizarani saa hiyohiyo, basi sikuwa tayari kuongoza huo mgomo na kwamba ningejiuzulu ili wachague kiongozi mwingine.
Baada ya hapo wanafunzi wakapoa, wakatawanyika wakabaki wachache kama 20. Nikawaambia wanafunzi walio wengi wameshanielewa. Ilipofika Jumanne wanafunzi wakapapata pesa zao na mambo yakaendelea kama mdundo. Ndio walinidharau sana siku hiyo Nkrumah na kuniona mimi ni traitor, lakini wengi walinishukuru baada ya siku tatu baada ya kutulia na ku-reflect.
Tunafahamu ya kuwa wap ambao wana sifa ulizotaja hapo juu lakini kushabikia vijana wetu kupigwa, kuwekwa rumande na kutolewa mimba, si sahihi! Pia naomba nikuulize ni kwa nini wanafunzi wa Chuo kikuu ni Vialza kama unavyodai? Who are they and how did they become like that? They were NOT born like that. Ni mazingira. Sasa kama mfano wanaoona ni kwamba viongozi wetu wa nchi wanaiba na kutufilisi, na ni vihiyo na wababe, unafikiri what type of role models do they have to look up to? Acha kumwaga propaganda hapa!
Hili la uchaguzi nimeshasema tangu jana kwamba hapa utawala umechemsha sana. Enzi zetu mambo ya DARUSO elections yalikuwa ya kwetu na utawala ulikuwa haugusi zaidi ya kumtuma Dean of Students kama observer tu. Ndio nasema wanafunzi sio watoto wadogo, waachwe wafanye mambo yao na wawajibike nayo. Ndio wanajifunza kujitegemea hivyo. Katika hili mbona tupo page moja kabisa.
Tatizo lingine kubwa hapa ni lack of clarity juu ya sababu hasa za mgomo. Sasa wote tuna-struggle kutafuta sababu, lakini ni jukumu la wagomaji: (i) kueleza kwa uwazi kabisa sababu za kugoma (ii) kushawishi jamii kwamba mgomo wao ni muhimu na kwamba wametumia njia zote imeshindikana na imebidi wagome (iii) mgomo wao sio kwa ajili ya maslahi yao leo tu bali pia ni katika kudai mambo ya msingi yatakayosaidia hata kizazi kijacho.
Principle moja tuliokuwa tunatumia sisi ni kwamba tulikuwa hatupo tayari kufanya mgomo (i) bila kueleza sababu vizuri za kugoma na zikaeleweka (ii) tulikuwa tunahakikisha kwamba katika kila mgomo tunakuwa na agenda inayogusa jamii ili tupate sympathy ya kutosha ndio maana utakuta kwamba tuliweza kwenda kupeleka msaada wa unga kwa wale wananchi waliobomolewa nyumba kule Kwamzungwi-Pugu. Na kuna kipindi tuligoma kwa ajili ya pesa za chakula lakini ndani yake tukaweka agenda kwamba tunadai nyongeza ya bajeti katika waizara ya elimu na kila mtu akatuunga mkono. Lengo ilikuwa ni kuonyesha kwamba DARUSO ni chombo cha kuwasemea wasio na sauti (voice of the voiceless)na wala sio chombo cha kutetea mambo ya mkate na bluebend za wanafunzi tu.
Tatizo la wanafunzi wetu leo sababu za migomo (i) hazieleweki kwa hiyo kila mtu anabaki kubuni (ii) hazigusi jamii na hivyo inakuwa rahisi kwa serikali kushinda maana wanaishia kuzomewa na wananchi walio wengi.
Nakuhakikishia serikali haiwezi kufunga chuo kwa sababu ya mgomo ikijua wanafunzi wana sympathy ya wananchi katika mgomo wao. Kila mara serikali kabla haijafunga chuo huwa inasoma kwanza maoni ya wananchi; wakiona wananchi wengi hawaungi mkono mgomo wanafunga, wakigundua wanafunzi wana sympathy ya wananchi hawafungi. Hili ni jambo ambalo viongozi wa wanafunzi ni muhimu wakilijua. Always make sure your agenda is relevant to the people's problems, otherwise mtabaki peke yenu na wananchi wa Manzese watawazomea!
Hili la uchaguzi nimeshasema tangu jana kwamba hapa utawala umechemsha sana. Enzi zetu mambo ya DARUSO elections yalikuwa ya kwetu na utawala ulikuwa haugusi zaidi ya kumtuma Dean of Students kama observer tu. Ndio nasema wanafunzi sio watoto wadogo, waachwe wafanye mambo yao na wawajibike nayo. Ndio wanajifunza kujitegemea hivyo. Katika hili mbona tupo page moja kabisa.
Tatizo lingine kubwa hapa ni lack of clarity juu ya sababu hasa za mgomo. Sasa wote tuna-struggle kutafuta sababu, lakini ni jukumu la wagomaji: (i) kueleza kwa uwazi kabisa sababu za kugoma (ii) kushawishi jamii kwamba mgomo wao ni muhimu na kwamba wametumia njia zote imeshindikana na imebidi wagome (iii) mgomo wao sio kwa ajili ya maslahi yao leo tu bali pia ni katika kudai mambo ya msingi yatakayosaidia hata kizazi kijacho.
Principle moja tuliokuwa tunatumia sisi ni kwamba tulikuwa hatupo tayari kufanya mgomo (i) bila kueleza sababu vizuri za kugoma na zikaeleweka (ii) tulikuwa tunahakikisha kwamba katika kila mgomo tunakuwa na agenda inayogusa jamii ili tupate sympathy ya kutosha ndio maana utakuta kwamba tuliweza kwenda kupeleka msaada wa unga kwa wale wananchi waliobomolewa nyumba kule Kwamzungwi-Pugu. Na kuna kipindi tuligoma kwa ajili ya pesa za chakula lakini ndani yake tukaweka agenda kwamba tunadai nyongeza ya bajeti katika waizara ya elimu na kila mtu akatuunga mkono. Lengo ilikuwa ni kuonyesha kwamba DARUSO ni chombo cha kuwasemea wasio na sauti (voice of the voiceless)na wala sio chombo cha kutetea mambo ya mkate na bluebend za wanafunzi tu.
Tatizo la wanafunzi wetu leo sababu za migomo (i) hazieleweki kwa hiyo kila mtu anabaki kubuni (ii) hazigusi jamii na hivyo inakuwa rahisi kwa serikali kushinda maana wanaishia kuzomewa na wananchi walio wengi.
Nakuhakikishia serikali haiwezi kufunga chuo kwa sababu ya mgomo ikijua wanafunzi wana sympathy ya wananchi katika mgomo wao. Kila mara serikali kabla haijafunga chuo huwa inasoma kwanza maoni ya wananchi; wakiona wananchi wengi hawaungi mkono mgomo wanafunga, wakigundua wanafunzi wana sympathy ya wananchi hawafungi. Hili ni jambo ambalo viongozi wa wanafunzi ni muhimu wakilijua. Always make sure your agenda is relevant to the people's problems, otherwise mtabaki peke yenu na wananchi wa Manzese watawazomea!
ni yale yale ya utawala wa Msolla! hivi kweli Tanzania hatuna watu wenye akili timamu ambao wanaweza kukaa chini na kutatua matatizo ya Mlimani? Tuombe wawekezaji waje kutuonesha jinsi ya kuendesha Chuo Kikuu cha Taifa...?
Kitila
Hebu tafuta mwanausalama yoyote akauleze kwa kina yanayofanyika mlango wa nyuma hapo UDSM. Una bahati katika kipindi chako hukukuwa na matukio makubwa ya kitaifa ambayo yangepelekea serikali kufanya propaganda dhidi ya wanafunzi kama ilivyokuwa wakati wa Nyerere na yale matukio ya wakati wa Mwinyi. Unafahamu jinsi ambavyo wanausalama walisuka ule mpango mzima wa kinachoitwa "kisa cha kubakwa kwa Levina Mukasa?".
Ukweli ni kuwa hawa wanafunzi wameingia mtego wa propaganda za serikali. Walikuwa na madai ya msingi ya ufisadi, sasa wameshatolewa kabisa katika mstari- sasa wanaonekana kuwa wanagomea uchaguzi, na wametolewa zaidi kwenye mstari, sasa wanaonekana wanagombea wenzao waliosimamishwa warudi. Kila kukicha wanazidi kuondolewa katika mstari. Kesho utakuta chuo chote kinafungwa na sababu zinazotolewa zitafanya wanafunzi waonekani wajinga kabisa.
Ukweli ni kuwa chini ya ufisadi wa EPA, RICHMOND nk- serikali imeiona kuna vuguvugu linafukuta UDSM kama lile la mageuzi ya 1990. Vijana wameamua kuunga mkono upinzani. Na ukitaka ushahidi wa haya ninayoyasema soma Ripoti ya Kamati ya Ulinzi na Usalama iliyowasilishwa kikao cha NEC ya CCM Butiama. Ripoti hiyo imesema wazi kwamba wanafunzi wa UDSM wamekuwa upinzani haswa CHADEMA na kwamba hali hiyo ni tishio kwa serikali. Maelekezo yalitolewa kwamba wote wenye mwelekeo wa upinzani watafutiwe sababu na kwa ujumla UDSM ichonganishwe kwa wananchi ili wanafunzi na jumuia yote ya wasomi pale ionekane hamnazo. Yale maelezo yaliyoandikwa ukweli ni huu niliyoyaweka hapa ni maelezo ambayo nimeyapata toka kwa mwanausalama mmoja. Ni sehemu tu ya maelezo ya wanafunzi ambayo inaelekea waliyaandika kwa kambi ya upinzani bungeni kueleza tukio zima lilivyo.
Binafsi siwapendi CHADEMA wanavyofanya siasa yao, lakini hili limenigusa kwa sababu najua chuo kikifungwa waathirika ni pamoja na mwanangu aliyeko pale UDSM mwaka wa mwisho. Hivyo, watanzania tuungane pamoja kuhakikisha chuo hakifungwi. Na hatua ya kwanza ni kujua ukweli wa yote yanayoendelea pale UDSM
The propaganda machinery of the state is now full at play, angalia trick ndogo tu kwa mfano- Mukandala ametumia muda mrefu kueleza jinsi ambavyo wanafunzi ni wavuta bangi, lakini ukiangalia katika ile orodha ya kina mtatatiro na wenzake wanaotajwa kuwa vinara wa mgomo- yale majina ya wanaoitwa wavuta bangi watano si sehemu ya majina yao kabisa. This are pure propagandas and distortions!
PM
kulaumu wanafunzi na kuseherekea kupigwa kwao na kupelekwa mahakamani wakati kina Balali, Mkapa, Lowasa, Vijisenti(Chenge ) na wenzao wanatesa mitaani japo wamefisadi kiasi kikubwa cha mali zetu ni kuwa na ujauzito wa mawazo au utindio wa ubongo
Rwekaza Mukandala ni fisadi, dikiteta na muuaji. Nimemweka kwenye notice hapa JF. Nitamfuatilia kama Chenge na sitampa breki kama mkoloni na mwizi mwenye uraia wa utata ROstam Azizi
Wameingilia uchaguzi, wamefukuza viongozi, wamepiga mabomu wanafunzi bila sababu yoyote, kuna habari kuwa wameua mwanafunzi mjamzito, wamekamata wanafunzi usiku wa manane, hii ni hitimisho la udikiteta, ufisadi na "uuaji" wa Mkandara (ambaye ni mshauri wa Kikwete wa masuala ya siasa).
kama kawaida yako... maumivu ya kichwa huanza polepole....
Mwizraeli ameshindwa kufaulu kwa kutumia mabavu ya kila aina kule Palestina: mauaji, mateso, kila mbinu, lakini binadamu anaonekana hawezi kufugika kama kuku. mabavu hayatatua matatizo ya msingi
Kweli kabisa PM,
Habari za kiusalama kwenye suala la wanafunzi hawa zinatisha. Kwanza alianza Magembe kwa kuwaonya wanafunzi wasiteue viongozi wenye msimamo, na kisha ni juhudi ya serikali ya kudhibiti kazi na utendaji kazi wa viongozi wa wanafunzi.
Kuanzia ile siku ambayo Mtatiro na wenzake walitoa tamko la kukemea ufisadi, Mukandala amekuwa anamfuatilia sana huyu Mtatiro na wenzake. Huu ni udikiteta, ufisadi na uuaji wa hali ya juu kabisa unaonyeshwa hapa na Mukandala (ambaye ni mshauri wa Kikwete)
Naona wanataka kuingilia siasa za vyuoni kama vile ambavyo Republicans hapa Marekani wameanza mikakati ya kuingilia vyuo vikuu ili kupunguza influence ya Demokrats vyuoni.
CCM wanaweza kudhani kuwa wanawakomoa CHADEMA kwenye hii issue lakini nina hakika kabisa kuwa wanacreate radicals ambao siku moja watajuta kwanini waliingilia uendeshaji wa serikali za wanafunzi vyuo vikuu
Rwekaza Mukandala ni fisadi, dikiteta na muuaji. Nimemweka kwenye notice hapa JF. Nitamfuatilia kama Chenge na sitampa breki kama mkoloni na mwizi mwenye uraia wa utata ROstam Azizi