BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Date::10/30/2008
Serikali yatetea mkataba wake na Tanzanite One, wabunge waupinga
Na Daniel Mjema, Dodoma
Mwananchi
SERIKALI imesema madini ya Tanzanite hayawezi kuisha ifikapo 2012 hivyo hakuna sababu ya kufuta mikataba ya uwekezaji na na kampuni ya Tanzanite One inayochimba madini hayo huko Mererani kwa kuhofia kumalizika kwa madini hayo adimu duniani.
Msimamo huo wa Serikali ulitolewa Bungeni juzi na waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wakati akijibu michango ya wabunge waliotoa ushauri wao juu ya taarifa ya kamati ya Rais ya kuishauri Serikali kuhusu usimamizi wa Sekta ya madini.
Kauli hiyo ya Waziri Ngeleja kuhusu kutovunjwa kwa mkataba huo ilionekana kujibu zaidi mchango wa Mbunge wa Same Mashariki,Anna Kilango Malecella aliyetaka Serikali ivunje mkataba na kampuni hiyo hata kabla ya kufikia mwaka 2012.
Kilango ambaye ni mmoja wa Wabunge wanaozungumza kwa hisia kali alisema wachimbaji wadogo wanao uwezo wa kuchimba madini ya vito kwa kutumia mitambo midogo ikiwamo Tanzanite.
Nimefanya utafiti wangu na kugundua kuwa leseni yao (Tanzanite One) inamalizika mwaka 2012 mimi naona huko ni mbali ukilinganisha na hasara tutakayopata tusitishe leseni yao sasaalisema Kilango.
Kilango alisema uchimbaji wa madini ya vito kwa kutumia mitambo mikubwa sio endelevu na kuonya kuwa kiasi cha madini kinachochimbwa na kuhifadhiwa Afrika Kusini ni kikubwa huku Tanzania ikiachiwa mashimo.
Alionya kwa vile kampuni hiyo sasa inafahamu uchimbaji wa madini ya Vito utafanywa na Watanzania kwa asilimia 100 wanaweza kuchimba kwa nguvu ili kufikia 2012 madini ya Tanzanite yawe yamekwisha.
siku zote kutoa maamuzi magumu ndio kuendelea na huu ni uamuzi mgumu lakini tumwambie Rais kuwa sisi Wabunge tunamuunga mkono na tuko tayari kuchangia fidia kusitisha mkataba huualisema.
Hata hivyo akijibu michango ya Wabunge, Ngeleja upo muda wa kutosha kurekebisha kasoro zilizojitokeza na kusema hakuna sababu kwa sasa kuwanyanganya wawekezaji hao migodi.
hatuwezi kuwanyanganya bado hatujafika huko kwa sababu tumeingia nao mikataba tukawapa na leseni hatujachelewa tutarekebisha hizo dosarialisema Ngeleja.
Waziri huyo alisema serikali itaifanyia kazi michango na ushauri wote uliotolewa na Serikali ikiwamo kufanya uchunguzi wa namna ilivyouza hisa zake kama ilivyopendekezwa na kamati ya kudumu ya Bunge la Madini na Nishati pamoja na Wabunge.
Alisema serikali inakubaliana na mapendekezo ya wabunge ya kutaka madini ya vito yasafishwe hapa nchini na kutoa wito kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuungana kwa ajili ya kuanzisha viwanda vya aina hiyo vitakavyotoa ajira kwa watanzania.
Wakati akichangia ripoti hiyo juzi jioni, Mbunge wa Kwela,Chrisant Mzindakaya(CCM) maarufu kama mzee wa mabomu jana aliipasha serikali kwa kuwakumbatia wawekezaji na kuwafanya kama Mungu wa duniani.
Mzindakaya alisema Tanzania inapaswa kuiga mfano wan chi ya Botswana ambayo imekuwa ikimiliki migodi nusu kwa nusu kati ya Serikali na makampuni yanayohitaji kuwekeza katika sekta hiyo.
Serikali isiogope kumiliki utajiri tulionao kwanini tunataka kila kitu raw material(malighafi) madini tunauza ghafi,kahawa tunauza ghafi kila kitu tunauza ghafi huu ni ugonjwa mbaya sanaalisema.
Mbunge huyo alitaka Shirika la madini nchini(STAMICO) liwezeshwe kusimamia uchimbaji madini na kusema Tanzania ina wataalamu wazuri wa madini bali kinachogomba ni vifaa.
Mzindakaya alisema madini sio bidhaa inayoharibika hivyo hakuna haraka ya kutafuta wawekezaji kabla ya kuwa na mazingira yanayoiwezesha nchi kunufaika na rasilimali zake.
Botswana wao wanamiliki 50-50, na wanachokifanya ni kwamba wakishaingia mkataba wa namna hii wanakwenda kukopa Benki na hapo sasa ndio unaajiri wataalamualisema Mzindakaya.
Kwa mujibu wa Mzindakaya,Tanzania ingeweza kuiga mfano huo na kumiliki migodi hii kwa ubia wa nusu kwa nusu badala ya kuwaachia wageni wamiliki migodi hiyo kwa asilimia 100.
Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene(CCM) alisema watanzania wa leo hawajatofautiana na wale wa kabla ya uhuru ambao waliletewa shanga na wazungu na wao kutoa almasi.
Alisema hivi sasa Watanzania wanadanganywa na Serikali kuwa imeamua kutafuta wawekezaji kwa sababu haifanyi biashara na kusema serikali zote duniani zinafanya biashara na kutoa mfano wa Dubai ambako Taxi zote zinamilikiwa na Serikali.
Hivi hii imani kwamba Serikali haifanyi biashara tunadanganywa na nani?...Tufike mahali Serikali yetu ikiri kuwa ilikosea halafu turudi nyuma kumiliki rasilimali zetualisisitiza.
Serikali yatetea mkataba wake na Tanzanite One, wabunge waupinga
Na Daniel Mjema, Dodoma
Mwananchi
SERIKALI imesema madini ya Tanzanite hayawezi kuisha ifikapo 2012 hivyo hakuna sababu ya kufuta mikataba ya uwekezaji na na kampuni ya Tanzanite One inayochimba madini hayo huko Mererani kwa kuhofia kumalizika kwa madini hayo adimu duniani.
Msimamo huo wa Serikali ulitolewa Bungeni juzi na waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wakati akijibu michango ya wabunge waliotoa ushauri wao juu ya taarifa ya kamati ya Rais ya kuishauri Serikali kuhusu usimamizi wa Sekta ya madini.
Kauli hiyo ya Waziri Ngeleja kuhusu kutovunjwa kwa mkataba huo ilionekana kujibu zaidi mchango wa Mbunge wa Same Mashariki,Anna Kilango Malecella aliyetaka Serikali ivunje mkataba na kampuni hiyo hata kabla ya kufikia mwaka 2012.
Kilango ambaye ni mmoja wa Wabunge wanaozungumza kwa hisia kali alisema wachimbaji wadogo wanao uwezo wa kuchimba madini ya vito kwa kutumia mitambo midogo ikiwamo Tanzanite.
Nimefanya utafiti wangu na kugundua kuwa leseni yao (Tanzanite One) inamalizika mwaka 2012 mimi naona huko ni mbali ukilinganisha na hasara tutakayopata tusitishe leseni yao sasaalisema Kilango.
Kilango alisema uchimbaji wa madini ya vito kwa kutumia mitambo mikubwa sio endelevu na kuonya kuwa kiasi cha madini kinachochimbwa na kuhifadhiwa Afrika Kusini ni kikubwa huku Tanzania ikiachiwa mashimo.
Alionya kwa vile kampuni hiyo sasa inafahamu uchimbaji wa madini ya Vito utafanywa na Watanzania kwa asilimia 100 wanaweza kuchimba kwa nguvu ili kufikia 2012 madini ya Tanzanite yawe yamekwisha.
siku zote kutoa maamuzi magumu ndio kuendelea na huu ni uamuzi mgumu lakini tumwambie Rais kuwa sisi Wabunge tunamuunga mkono na tuko tayari kuchangia fidia kusitisha mkataba huualisema.
Hata hivyo akijibu michango ya Wabunge, Ngeleja upo muda wa kutosha kurekebisha kasoro zilizojitokeza na kusema hakuna sababu kwa sasa kuwanyanganya wawekezaji hao migodi.
hatuwezi kuwanyanganya bado hatujafika huko kwa sababu tumeingia nao mikataba tukawapa na leseni hatujachelewa tutarekebisha hizo dosarialisema Ngeleja.
Waziri huyo alisema serikali itaifanyia kazi michango na ushauri wote uliotolewa na Serikali ikiwamo kufanya uchunguzi wa namna ilivyouza hisa zake kama ilivyopendekezwa na kamati ya kudumu ya Bunge la Madini na Nishati pamoja na Wabunge.
Alisema serikali inakubaliana na mapendekezo ya wabunge ya kutaka madini ya vito yasafishwe hapa nchini na kutoa wito kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuungana kwa ajili ya kuanzisha viwanda vya aina hiyo vitakavyotoa ajira kwa watanzania.
Wakati akichangia ripoti hiyo juzi jioni, Mbunge wa Kwela,Chrisant Mzindakaya(CCM) maarufu kama mzee wa mabomu jana aliipasha serikali kwa kuwakumbatia wawekezaji na kuwafanya kama Mungu wa duniani.
Mzindakaya alisema Tanzania inapaswa kuiga mfano wan chi ya Botswana ambayo imekuwa ikimiliki migodi nusu kwa nusu kati ya Serikali na makampuni yanayohitaji kuwekeza katika sekta hiyo.
Serikali isiogope kumiliki utajiri tulionao kwanini tunataka kila kitu raw material(malighafi) madini tunauza ghafi,kahawa tunauza ghafi kila kitu tunauza ghafi huu ni ugonjwa mbaya sanaalisema.
Mbunge huyo alitaka Shirika la madini nchini(STAMICO) liwezeshwe kusimamia uchimbaji madini na kusema Tanzania ina wataalamu wazuri wa madini bali kinachogomba ni vifaa.
Mzindakaya alisema madini sio bidhaa inayoharibika hivyo hakuna haraka ya kutafuta wawekezaji kabla ya kuwa na mazingira yanayoiwezesha nchi kunufaika na rasilimali zake.
Botswana wao wanamiliki 50-50, na wanachokifanya ni kwamba wakishaingia mkataba wa namna hii wanakwenda kukopa Benki na hapo sasa ndio unaajiri wataalamualisema Mzindakaya.
Kwa mujibu wa Mzindakaya,Tanzania ingeweza kuiga mfano huo na kumiliki migodi hii kwa ubia wa nusu kwa nusu badala ya kuwaachia wageni wamiliki migodi hiyo kwa asilimia 100.
Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene(CCM) alisema watanzania wa leo hawajatofautiana na wale wa kabla ya uhuru ambao waliletewa shanga na wazungu na wao kutoa almasi.
Alisema hivi sasa Watanzania wanadanganywa na Serikali kuwa imeamua kutafuta wawekezaji kwa sababu haifanyi biashara na kusema serikali zote duniani zinafanya biashara na kutoa mfano wa Dubai ambako Taxi zote zinamilikiwa na Serikali.
Hivi hii imani kwamba Serikali haifanyi biashara tunadanganywa na nani?...Tufike mahali Serikali yetu ikiri kuwa ilikosea halafu turudi nyuma kumiliki rasilimali zetualisisitiza.