Serikali yasitisha mafunzo ya JKT

Serikali yasitisha mafunzo ya JKT

kuna vijana wapo CCP wanaongeza nyota course yao iinakatishwa haraka sana kwasababu serikali imeishiwa na pesa.

Mr. Kikwete ataacha kovu la ukata lisilopona milele.
 
JKT ni muhimu tatizo labda kwa sababu huko makambini hawafanyi shughuli za uzalishaji.
muhimu wajue/waelezwe kwamba kupitia kwao JKT sio kupatiwa ajira ni kujengewa uwezo wa kujiamini na kujitegemea.
 
Serikali imesitisha mafunzo ya JKT kwa mwaka huu. Kwa hiyo wale vijana waliokua wanategemea kuanza mafunzo hayo mwezi wa pili mwaka,mafunzo hayo hayatakuwepo tena.

Sababu ya kusitisha mafunzo hayo ni ukata unaoikabili serikali,serikali haina hela.

MAONI YANGU. Mafunzo haya ya JKT yapigwe marufuku kabisa na yafutwe maana hayana faida yoyote wala tija katikaTaifa hili. Binafsi natamani serikali ifilisike kabisa ili isiweze kufadhili mafunzo hata tena.

Chanzo: Gazeti la Jamhuri.
Huu utumbo utupiliwe mbali moja kwa moja,ni upotevu wa muda wa watu na itaishia kutuandalia tu magaidi na majambazi watarajiwa.
 
Kuna faida na hasara za kupeleka vijana wengi JKT na kuwatupa uraini bila ajira... siku hawa wakiasi itakuwa ni mtafutano, iko wazi kwamba police hawataweza kupambana nao na hivyo kupekea kupambana na wanajeshi wenzao

Ni bora yasitishwe kwa mstakabali mwema wa taifa

Ni kweli.Hawa jamaa wakiwa wengi uraiani hata wizi wa Kura itakuwa taabu kwa sababu wanafundishwa uzalendo na kutoogopa Risasi wala vitisho.
 
walikuwa wanapewa mafunzo ya kujiajir na cyo kutegemea kuajiriwa
 
Na kama ni mandamano mbona hata leo CUF wameandamana????? kwani nao walikuwa JKT??????

Tofauti yao na CUF ni kwamba hawa wa Cuf ni wepesi kukamatwa na Polisi lakini waliotoka JKT ni vigumu kukamatwa na Polisi kwa sababu wana mbinu za Kivita.Kwa kweli ni ngumu kudhibiti Jeshi linalozurura mtaani bila uangalizi likiwa halina uhakika wa mlo wa siku.
 
Huyu sijui anazungumzia serikali gani tangu lini serikali ikafirisika?
 
Huyu sijui anazungumzia serikali gani tangu lini serikali ikafirisika?

Serikali ya ugiriki,cyprus,ureno na nyingi nyingine zinazotumia sarafu ya euro zilifilisika. Kampuni ya standard and poor mwaka juzi ilitangaza serikali ya ugiriki kufilisika.

Hata serikali ya Tanganyika iko mbioni kufilisika,ni madeni tu na kukopa.
 
Back
Top Bottom