Mimi ni miongoni mwao so ujumbe umefika Mkuu. Inawezekana Kikwete ndio kiongozi wa hayo uliyoyataja hapo juuKatika watu waliochangia kuzorota kwa taifa hili kwa asilimia kubwa na ambao wanasababisha serikali ionekane hovyo zaidi ni watumishi wa Umma ambao miongoni mwao zaidi ya nusu ni fake! hawa qualify na hukuwengi wao wakiwa na vyeti vya ndugu na majirani!
Hawafai hata kulipwa mishara maana sijui wanachofanya, Mkapa alileta mpango wa OPRASS waliogopa sana na kumuomba Kikwete aondoe huo mpango maana walijua wengi wao wamefanya ofisi za serikali kama kijiwe cha kuangalia internet na kunywa kahawa bila tija.
Ndio kikwete aliwaijia juu na wakanywea hawana confidence wengi ni uzembe na ngono ofisi na kusinzia tu!
Sasa ni dhahiri, KIKWETE nchi imemshinda. Serikali yake imeshindwa kulipa watumishi stahili zao. Mishahara yashushwa, posho zapukutishwa na hakuna malipo kwa wafanyakazi wapya wanaoanza kazi. Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma (Standing Orders) zafanyiwa marekebisho.
Kwa mujibu wa Gazeti la Serikali Namba 10 vol. 92 la 11/3/2011 na Government Notice (GN) 104 ya 11/03/2011, Standing Orders za 2009 zimefanyiwa marekebisho ambapo pamoja na mambo mengine sasa mtumishi wa serikali anayeanza kazi HATALIPWA gharama za kuhamisha mizigo yake na posho yake ya kujikimu sasa itakuwa ni kwa siku saba (7) badala ya 14 kama ilivyokuwa kabla ya marekebisho hayo (tazama kif. L.6 na jedwali J/I kolamu ya [vi] na GN 104 ya 11/3/2011). Ikumbukwe kuwa ni mwaka jana tu yaani kuanzia Julai 1, 2010 ndipo (bila shaka ili kupata kura za wafanyakazi kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge 2010) Serikali ilipopandisha viwango vya posho kwa watumishi wapya na wale wanaohamia vituo vipya. Kabla ya Julai 1, 2010 mtumishi alipokuwa akihama alikuwa analipwa TSh 1,000/= kwa tani-km x tani 3 [kwa maafisa] (au tani 1.5 kwa watumishi wa kada ya chini) x km y (umbali kwenda kituo kipya); na posho ya kujikimu kwa mujibu wa stahili yake (siku 14 kwa kuhama na siku 7 kwa watumishi wapya). Lakini Serikali kuanzia Julai 1, 2010 ilipandisha pesa hizo kwa kuongeza tani kuwa 5 kwa maafisa na tani 3 kwa hao wengine (tazama Standing Orders za 2009 zilizoanza kutumia Julai 1, 2010) na posho ya kujikimu kuwa ya siku 14 kwa wote yaani watumishi wapya na wale wanaohamia vituo vipya vya kazi.
Kama hilo halitoshi Serikali tena imeshusha mishahara ya watumishi wa kada mbali2 ikiwa ni pamoja na kada ya afya kimya2 bila kutangazia umma kwa kuunganisha MADARAJA ya mishahara ambapo daraja la juu linateremshwa na kuunganishwa na daraja la chini yake. Kwa mfano kwa watumishi wa afya waliokuwa ktk ngazi ya mshahara TGHS B.1 (425,290/=) sasa wamerundikwa ktk TGHS A. 1 (260,400/=): haya ni maangamizi. Wafanyakazi mko wapi? Na viongozi wa wafanyakazi je, na nyie mko wapi? Nicolas Mgaya uko wapi? Ninamkumbuka mpanganaji marehemu RWEGASIRA wa TRAWU ... Cha ajabu ni kuwa wafanyakazi wa chini ndio wanaoguswa na makato haya. Wakubwa kama vile Wabunge, Mawaziri nk wanazidi kurundikiwa mihela tena pasipo kufanya kazi ya maana.
Wachambuzi wa mambo wanabaini kuwa haya ni matokeo dhahiri ya KIKWETE kushindwa kuongoza nchi na kwamba hajui la kufanya ili kuikwamua nchi kutoka hapa ilipo. Tungoje tuone, bila shaka kuna mengine mengi.
na wala huwasikii wakilalamika??? nchii hii!!!!!!!!!!! kazi ipo
we hujui?, Dr wa ukweli (hlf zikachakachuliwa),Komeni kulalamika kwani wakati wa uchaguzi mwaka jana mlimpigia kura nani?
sijasikia, eleza vizuri tafadhaliSi umesikia hata TRA wameshindwa kukusanya mapato wamewapa mafisadi;
Mbona sijawahi kusikia mshahara unashuswa tangu enzi za TANU, Sasa basi lowasa arudi serikalini.:A S 103:
Sasa ni dhahiri, KIKWETE nchi imemshinda. Serikali yake imeshindwa kulipa watumishi stahili zao. Mishahara yashushwa, posho zapukutishwa na hakuna malipo kwa wafanyakazi wapya wanaoanza kazi. Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma (Standing Orders) zafanyiwa marekebisho.
Kwa mujibu wa Gazeti la Serikali Namba 10 vol. 92 la 11/3/2011 na Government Notice (GN) 104 ya 11/03/2011, Standing Orders za 2009 zimefanyiwa marekebisho ambapo pamoja na mambo mengine sasa mtumishi wa serikali anayeanza kazi HATALIPWA gharama za kuhamisha mizigo yake na posho yake ya kujikimu sasa itakuwa ni kwa siku saba (7) badala ya 14 kama ilivyokuwa kabla ya marekebisho hayo (tazama kif. L.6 na jedwali J/I kolamu ya [vi] na GN 104 ya 11/3/2011). Ikumbukwe kuwa ni mwaka jana tu yaani kuanzia Julai 1, 2010 ndipo (bila shaka ili kupata kura za wafanyakazi kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge 2010) Serikali ilipopandisha viwango vya posho kwa watumishi wapya na wale wanaohamia vituo vipya. Kabla ya Julai 1, 2010 mtumishi alipokuwa akihama alikuwa analipwa TSh 1,000/= kwa tani-km x tani 3 [kwa maafisa] (au tani 1.5 kwa watumishi wa kada ya chini) x km y (umbali kwenda kituo kipya); na posho ya kujikimu kwa mujibu wa stahili yake (siku 14 kwa kuhama na siku 7 kwa watumishi wapya). Lakini Serikali kuanzia Julai 1, 2010 ilipandisha pesa hizo kwa kuongeza tani kuwa 5 kwa maafisa na tani 3 kwa hao wengine (tazama Standing Orders za 2009 zilizoanza kutumia Julai 1, 2010) na posho ya kujikimu kuwa ya siku 14 kwa wote yaani watumishi wapya na wale wanaohamia vituo vipya vya kazi.
Kama hilo halitoshi Serikali tena imeshusha mishahara ya watumishi wa kada mbali2 ikiwa ni pamoja na kada ya afya kimya2 bila kutangazia umma kwa kuunganisha MADARAJA ya mishahara ambapo daraja la juu linateremshwa na kuunganishwa na daraja la chini yake. Kwa mfano kwa watumishi wa afya waliokuwa ktk ngazi ya mshahara TGHS B.1 (425,290/=) sasa wamerundikwa ktk TGHS A. 1 (260,400/=): haya ni maangamizi. Wafanyakazi mko wapi? Na viongozi wa wafanyakazi je, na nyie mko wapi? Nicolas Mgaya uko wapi? Ninamkumbuka mpanganaji marehemu RWEGASIRA wa TRAWU ... Cha ajabu ni kuwa wafanyakazi wa chini ndio wanaoguswa na makato haya. Wakubwa kama vile Wabunge, Mawaziri nk wanazidi kurundikiwa mihela tena pasipo kufanya kazi ya maana.
Wachambuzi wa mambo wanabaini kuwa haya ni matokeo dhahiri ya KIKWETE kushindwa kuongoza nchi na kwamba hajui la kufanya ili kuikwamua nchi kutoka hapa ilipo. Tungoje tuone, bila shaka kuna mengine mengi.
sitaki kuamini mapema hii habari, na kama itakuwa kweli basi ile rushwa ya nigeria itakuwa ni cha mtoto, jk komaa na msimamo huo huo