Serikali yanawa mikono Al-Shabab Mtanzania

Serikali yanawa mikono Al-Shabab Mtanzania

Huyo maza ni mbugila tu asiyejitambua! Si ajabu hata hao al shabaab amewajua baada ya mwanae kuhusishwa! Nahisi huyo ni aina ya wazazi wanaoona sifa kuwa na watoto wengi wakt kuwatunza hawezi! Hapo msaada kwake ni VIBAO tu afunge bakuli lake!
 

paul-chagonja1-300x225.jpg



WAKATI mama mzazi wa Mtanzania Rashid Mberesero anayetuhumiwa kuwa kati ya wafuasi wa Al-Shabaab walioua wanafunzi 148 wa Chuo Kikuu cha Garissa nchini Kenya akitaka msaada wa Serikali ili akamwone mwanawe huyo, Jeshi la Polisi limesema halina uwezo wa kumsaidia.

Jeshi hilo limesema halina uwezo wa kumsaidia mama huyo, Fatma Ally kutokana na sheria mpya za ugaidi zilizopitishwa nchini Kenya hivi karibuni na kuwekewa pingamizi mahakamani.

Aidha limesema hadi sasa bado halijafuatilia tukio la kukamatwa kwa kijana huyo na kuwa habari zake linazifuatilia kwenye vyombo vya habari tu.

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Paul Chagonja, ameliambia MTANZANIA kuwa hajui msimamo wa Kenya ukoje kuhusu tukio hilo.

Alisema suala hilo ni la kisheria zaidi na sheria zinatofautiana baina ya nchi na nchi ikiwamo utaratibu wa kumwona mtu akiwa mahabusu.

“Jeshi la Polisi hatujui chochote kuhusu mtuhumiwa huyo zaidi ya kusoma kwenye magazeti, kwa hiyo ni ngumu kusema kama mama yake ataweza kumwona au la kutokana na sheria mpya za ugaidi walizopitisha wenzetu hivi karibuni.

“Sijazipitia vizuri sheria hizo, lakini baadhi yake zina makali zaidi, kwa hiyo siwezi kutia neno, tuwaachie uhuru wa sheria zao wenzetu waamue,” alisema.

Aidha alipoulizwa kuhusu taarifa za utaratibu wa kijana huyo kuwepo nchini Kenya, alisema hawana taarifa zake zaidi ya kusoma kwenye magazeti kwamba alitoweka nyumbani na shuleni.
Kutokana na hali hiyo, alisema Serikali sasa inategemea huruma ya Kenya katika kumponya ama kumwadhibu kijana huyo kwa mujibu wa sheria zake.

Kwa mujibu wa Fatma alikuwa anajua mtoto wake yupo shuleni Bihawana mkoani Dodoma alipokuwa akisoma kidato cha tano huku uongozi wa shule ukisema alitoroka tangu Novemba mwaka jana,
Sheria mpya ya ugaidi nchini Kenya, ambayo baadhi ya vipengele nane vilipingwa mahakamani inatoa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela na faini ya dola 55,000 kwa uchapishaji bila ruhusa wa makala au kutafuta habari amzazo zitatatiza uchunguzi ao operesheni ya kupambana dhidi ya ugadi.

CHANZO: Mtanzania

Mwambie huyo mama aache kiherehere na kutuchanganya sisi. Alishindwa kumtembelea alipokuwa bihawana anataka akamtembelee Kenya? Amesahau ule msemo wa asiyefunzwa na ***** hufunzwa na ulimwengu? Mwambie atulie tu "Mwiba hutokea pale ulipoingilia"
 
Huyu mama anataka asaidiwe kwenda kumfariji mwanae kwa lipi? Mwanae kaua watu wote hao wasio na hatia halafu jeshi limsaidie mamake kwenda kumsalimia gaidi? Hata kama uchungu wa mwana aujua mzazi lakini kwa hili hapana. Huyu mama ahojiwe ana kitu anajua maana nasikia hawa vijana wanapewa pesa kusaidia familia zao. Labda anataka kujua dogo kaweka wapi huo mzigo.
 
Uchungu wa mwana (mtoto) aujuae MAMA.... lakini liBaba halina hata habari !! POLE mama !! Magazetini@dragoon@The Bleiz@mcharo son
 
Last edited by a moderator:
Serikali ifuatilie utakuta walitoroka wengi.

Rekodi ziangaliwe za wote ambao hawakufanya mitihani ya form 2,4,6.Taarifa za Baraza la mitihani la taifa zaweza saidia hasa za wenye majina ya kiislamu.

Lakini pia walimu wakuu waweza ombwa peleka majina na taarifa za watoro wote wizara ya elimu kwa kipindi mfano cha miaka 10 hasa wenye majina ya kiislamu

Iundwe task force ya kuweka mkakati na namna ya kuwafuatilia hao watoro wako wapi.
Pia serikali yaweza fuatilia wale walioenda kusoma nje ya nchi nchi kama sudan,misri,libya na nchi za kiarabu ambao hawakurudi nchini wako wapi?

Na kwa wale ambao ndugu zao hawajui wako wapi ni vizuri polisi wahamasishe watu kuwapelekea majina ya watoto au ndugu ambao hawajulikani wako wapi.

Wazazi na ndugu wasaidie kutoa ushirikiano.
 
Uchungu wa mwana (mtoto) aujuae MAMA.... lakini liBaba halina hata habari !! POLE mama !! Magazetini@dragoon@The Bleiz@mcharo son

Baba kafanya la maana zaidi kuliko huyu anayemlilia muuaji. Anataka atumie rasilimali za umma kusaidia kwenda kumuona mtoa roho za watu? Na wewe unampa pole kwa maana unamuhurumia badala ya kumuhoji?
 
MAMA ATULIE MWANAE AFUNZWE
Yaan akikutwa na hatia akatwe pingili pingili kama kitimoto afu achomwe adi awe majivu afu mama yake akachikue majivu aje kuzika..........

Maana haiwezekani wazazi wa waliofariki wachomeke na jua kutafuta namna ya kukuza watoto wao na wengine wameweka hati za nyumba bank ili watoto wasome... mzazi huyo huyo ndo mtoto wa pekee aliyefariki plus madeni ya bank kwa ajili ya kumsomesha ......yeye aende kuchinja kirahis rahisi bila kujua wanafunzi wale wanategemewa kiasi gani na familia zao..........KAMA ANA HATIA NITASHANGAA SANA SEREKALI YA KENYA KAMA IMEMUACHA HAI MPAKA LEO
 
Huyu mama ahojiwe vizuri.dizaini kama ana details zaidi za dogo na genge lake.kuna kitu hapa mama atakuwa ana dondoo mbili tatu
 
Haitoshi tu kumjibu mama asiende Kenya. Polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama wamepata chanzo kizuri cha kuwatafuta magaidi watarajiwa nchini na waanze na huyo mama awaongoze machimbo na vijiwe vyote alivyokuwa anashinda mwanae ili watunusuru tuliobaki. Isitoshe wakamhoji na dogo awape taarifa za kina na ramani zote huko aliko ili kuwadhibiti waliobaki makambini. Huenda dogo ni tunda la wale watoto waliokutwa wamefichwa kwenye majumba ya waendesha madrasa kule Mkoani Kilimanjaro. Ni wazo tu.
 

paul-chagonja1-300x225.jpg



WAKATI mama mzazi wa Mtanzania Rashid Mberesero anayetuhumiwa kuwa kati ya wafuasi wa Al-Shabaab walioua wanafunzi 148 wa Chuo Kikuu cha Garissa nchini Kenya akitaka msaada wa Serikali ili akamwone mwanawe huyo, Jeshi la Polisi limesema halina uwezo wa kumsaidia.

Jeshi hilo limesema halina uwezo wa kumsaidia mama huyo, Fatma Ally kutokana na sheria mpya za ugaidi zilizopitishwa nchini Kenya hivi karibuni na kuwekewa pingamizi mahakamani.

Aidha limesema hadi sasa bado halijafuatilia tukio la kukamatwa kwa kijana huyo na kuwa habari zake linazifuatilia kwenye vyombo vya habari tu.

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Paul Chagonja, ameliambia MTANZANIA kuwa hajui msimamo wa Kenya ukoje kuhusu tukio hilo.

Alisema suala hilo ni la kisheria zaidi na sheria zinatofautiana baina ya nchi na nchi ikiwamo utaratibu wa kumwona mtu akiwa mahabusu.

“Jeshi la Polisi hatujui chochote kuhusu mtuhumiwa huyo zaidi ya kusoma kwenye magazeti, kwa hiyo ni ngumu kusema kama mama yake ataweza kumwona au la kutokana na sheria mpya za ugaidi walizopitisha wenzetu hivi karibuni.

“Sijazipitia vizuri sheria hizo, lakini baadhi yake zina makali zaidi, kwa hiyo siwezi kutia neno, tuwaachie uhuru wa sheria zao wenzetu waamue,” alisema.

Aidha alipoulizwa kuhusu taarifa za utaratibu wa kijana huyo kuwepo nchini Kenya, alisema hawana taarifa zake zaidi ya kusoma kwenye magazeti kwamba alitoweka nyumbani na shuleni.
Kutokana na hali hiyo, alisema Serikali sasa inategemea huruma ya Kenya katika kumponya ama kumwadhibu kijana huyo kwa mujibu wa sheria zake.

Kwa mujibu wa Fatma alikuwa anajua mtoto wake yupo shuleni Bihawana mkoani Dodoma alipokuwa akisoma kidato cha tano huku uongozi wa shule ukisema alitoroka tangu Novemba mwaka jana,
Sheria mpya ya ugaidi nchini Kenya, ambayo baadhi ya vipengele nane vilipingwa mahakamani inatoa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela na faini ya dola 55,000 kwa uchapishaji bila ruhusa wa makala au kutafuta habari amzazo zitatatiza uchunguzi ao operesheni ya kupambana dhidi ya ugadi.

CHANZO: Mtanzania

Huyu Chagonja mwongo, Polisi wa Interpol na wa TZ wamefika mpaka pale shule alikuwa anasoma na kukusanya taarifa za Rashid ikiwemo kumhoji Headmaster Mr. Mbilinyi yeye anasema hawajui lolote zaidi ya kusoma kwenye magazeti? that is an irresponsible leader.
 
Baba kafanya la maana zaidi kuliko huyu anayemlilia muuaji. Anataka atumie rasilimali za umma kusaidia kwenda kumuona mtoa roho za watu? Na wewe unampa pole kwa maana unamuhurumia badala ya kumuhoji?
WEWE acha kuchukua hukumu na kutoa judgment kabla ya uhakika wa mambo MAHAKAMA ndo yataHOJI na mahaka ndo yatatoa hukumu...!!! Hadi prove guilty ndo useme, Wee unajua maana ya MAMA au kuwa MZAZI !!
Mie sina haki ya kumhoji mzazi wa mhalifu ..mimi ntamsaidia kwa kupooza nafsi yake na kuridhisha amuone mwanae uso kwa uso!! Ooh God msaidie mama fatuma amuone mwanae kwa njia yeyote iliyo bora. AMIN
 
WEWE acha kuchukua hukumu na kutoa judgment kabla ya uhakika wa mambo MAHAKAMA ndo yataHOJI na mahaka ndo yatatoa hukumu...!!! Hadi prove guilty ndo useme, Wee unajua maana ya MAMA au kuwa MZAZI !!
Mie sina haki ya kumhoji mzazi wa mhalifu ..mimi ntamsaidia kwa kupooza nafsi yake na kuridhisha amuone mwanae uso kwa uso!! Ooh God msaidie mama fatuma amuone mwanae kwa njia yeyote iliyo bora. AMIN

We kama unauchungu nenda kamsaidie huyu mama.
 
WEWE acha kuchukua hukumu na kutoa judgment kabla ya uhakika wa mambo MAHAKAMA ndo yataHOJI na mahaka ndo yatatoa hukumu...!!! Hadi prove guilty ndo useme, Wee unajua maana ya MAMA au kuwa MZAZI !!
Mie sina haki ya kumhoji mzazi wa mhalifu ..mimi ntamsaidia kwa kupooza nafsi yake na kuridhisha amuone mwanae uso kwa uso!! Ooh God msaidie mama fatuma amuone mwanae kwa njia yeyote iliyo bora. AMIN

Huyo mtoto mwenyewe amekiri kuhusika na aliogopa kujilipua dakika za mwisho we ni nani hadi umtetee
 
Huyu Chagonja mwongo, Polisi wa Interpol na wa TZ wamefika mpaka pale shule alikuwa anasoma na kukusanya taarifa za Rashid ikiwemo kumhoji Headmaster Mr. Mbilinyi yeye anasema hawajui lolote zaidi ya kusoma kwenye magazeti? that is an irresponsible leader.

Upelelezi ukifanywa si lazima kuufanya public!!!

Anyway Haya tupe ushahidi wewe ulio nao unaokuthibitishia kuwa walihojiwa na interpol. Na aliyekwambia hao waliomhoji ni interpol sio usalama wa taifa au kikosi cha kupambana na ugaidi au kikosi maalumu cha kupambana na wahalifu cha JWTZ ni nani?
 
We kama unauchungu nenda kamsaidie huyu mama.
Wee umekurupuka, Mie nina uchungu na huzuni pande zote (waliokutwa na mauti,ndugu wafiwa,wahanga wa majeruhi na huyu mzazi)nimeshamfariji na kumombea wepesi wa kumtembelea mwanae, nikionana nae nampa nauli !! (dhambi yake nini?) kuwa muungwana....
 
Kamishina chagonja amejitahidi sana kujibu kwa busara nahisi huko akiwa peke yake anaweza akaongea maneno makali zaidi,huyo mama aache uchokozi ...
 
Ndg zake wote waliokuwa wanamtetea hapo awali wako kimya kama wamesafiri waje basi wamsaidie huyu mama
Baba yake mzazi alishanawa mikono mara baada ya tukio.
Nikimsikiliza BBC/DW alisema 'sheria ichukue mkondo wake'.
 
Huyo mtoto mwenyewe amekiri kuhusika na aliogopa kujilipua dakika za mwisho we ni nani hadi umtetee
Stunna !! soma vizuri mie siyo mjinga kumtetea Gaidi !! NIMEMTETEA MAMA (mzazi wake asiyekuwa na dhambi) alikuwa nyumbani masikini akilea familia yake!! Mama mtu dhambi yake nini..?!! Mfano tu dereva akiua katika ajali mama mtu abebe lawama kuwa ndiye aliyemzaa?????????????????????????????????!
@Simanyane
 
Back
Top Bottom