VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Ndugu zangu watanzania, mimi si msemaji wa Dr. Kigoda wala familia yake wala serikali. Lakini, nataka kudokeza ninachokijua. Ni kweli kuwa Dr. Kigoda yuko nchini India kwa matibabu. Kwa siku za hivi karibuni,amekuwa akilazwa ICU.
Anasumbuliwa na matatizo makubwa ya figo na ini. Tuzipuuze habari za kifo ingawa zaweza kuthibitishwa na wahusika kama ni za kweli kwa wakati na namna inayopasa. Nijuavyo, Dr. Kigoda anaendelea na matibabu ingawa hali yake si njema. Tumuombee Dr. Kigoda apate nafuu na aungane nasi kujenga Tanzania yetu.
Get well soon Comrade Abdallah Kigoda!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
======
Updates:
Anasumbuliwa na matatizo makubwa ya figo na ini. Tuzipuuze habari za kifo ingawa zaweza kuthibitishwa na wahusika kama ni za kweli kwa wakati na namna inayopasa. Nijuavyo, Dr. Kigoda anaendelea na matibabu ingawa hali yake si njema. Tumuombee Dr. Kigoda apate nafuu na aungane nasi kujenga Tanzania yetu.
Get well soon Comrade Abdallah Kigoda!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
======
Updates:
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Serikali inapenda kukanusha taarifa kutoka Kwenye baadhi ya Mitandao ya Kijamii ikidai kwamba, Mhe. Dkt. Abdallah Kigoda, Waziri wa Viwanda na Biashara amefariki dunia nchini India alikokuwa anatibiwa.
Taarifa Rasmi ya serikali ni kwamba taarifa hizo ni za uongo na hazina hata Chembe ya ukweli. Mhe. Dkt. Kigoda bado yupo nchini India Katika Hospitali ya Apollo katika Jiji la New Delhi anakoendelea kupatiwa matibabu.
Mhe. Dkt. Kigoda alikwenda India kwa matibabu tarehe 18 Septemba, 2015 na tangu kipindi hicho ameendeleaa kupata matibabu katika hospitali Hiyo ya Apollo.
Serikali inapenda kuvionya vyombo vya habari na Mitandao ya kijamii kuacha kusambaza taarifa za uongo kuhusu viongozi wa serikali.
Imetolewa na Assah Mwambene, Msemaji Mkuu wa serikali.