Nipe Maji
JF-Expert Member
- Mar 25, 2025
- 335
- 190
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema Serikali imejipanga kuongeza wigo wa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya kati vinavyotoa stashahada lengo ni kuongeza idadi ya wataalamu.
Utoaji wa mikopo katika ngazi za stashahada kwa wanafunzi wa ngazi hiyo ya elimu ulianza mwaka 2023/24, kwa fani sita za kipaumbele ambazo zina uhitaji mkubwa wa wataalamu ambazo ni afya na sayansi shirikishi, ualimu wa hisabati.
Fani nyingine ni fizikia na mafunzo ya amali, uhandisi na nishati, madini na sayansi ya ardhi, kilimo na mifugo ambapo Sh48 bilioni zilitengwa kwa ajili ya wanafunzi 8,000.
Pia soma Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
Akizungumza Jumanne Aprili 29,2025 wakati wa kufungua mkutano mkuu wa Shirika la Mtetezi wa Mama, Profesa Mkenda amesema Serikali ya awamu ya sita, imefanya mapinduzi makubwa kwenye sekta ya elimu ikiwamo ya kutoa mikopo kwa ngazi ya stashahada.
Amesema katika kuzalisha vijana wenye ujuzi, Serikali iliamua kuanza kutoa mikopo ngazi ya stashahada kwa kozi za kipaumbele na mpango wa sasa ni kuongeza wigo wa kozi zitakazonufaika na mpango huo.
Utoaji wa mikopo katika ngazi za stashahada kwa wanafunzi wa ngazi hiyo ya elimu ulianza mwaka 2023/24, kwa fani sita za kipaumbele ambazo zina uhitaji mkubwa wa wataalamu ambazo ni afya na sayansi shirikishi, ualimu wa hisabati.
Fani nyingine ni fizikia na mafunzo ya amali, uhandisi na nishati, madini na sayansi ya ardhi, kilimo na mifugo ambapo Sh48 bilioni zilitengwa kwa ajili ya wanafunzi 8,000.
Pia soma Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
Akizungumza Jumanne Aprili 29,2025 wakati wa kufungua mkutano mkuu wa Shirika la Mtetezi wa Mama, Profesa Mkenda amesema Serikali ya awamu ya sita, imefanya mapinduzi makubwa kwenye sekta ya elimu ikiwamo ya kutoa mikopo kwa ngazi ya stashahada.
Amesema katika kuzalisha vijana wenye ujuzi, Serikali iliamua kuanza kutoa mikopo ngazi ya stashahada kwa kozi za kipaumbele na mpango wa sasa ni kuongeza wigo wa kozi zitakazonufaika na mpango huo.