Serikali yagoma kuwepo kwa uchunguzi huru juu ya Tundu Lissu, wadai kwani kibiti walikuja wazungu?

hadi leo hatujasikia kama walinzi wa getini wamehojiwa,sijui dodoma nzima haina cctv hata route waliyopita hao wasiojulikana waonekane?ndiyo maana watu wanaamini madai ya mange kwamba hadi ndani ya TRA wafanyakazi wanshindwa ku access information kuhusu ile premio aliyoitaja lissu inamfatilia na hii ya juzi ya dodoma?kwa nini hata wamiliki hawajulikani?
kisingizio ni eti tunataka dereva wa lissu atusaidie...jamani kwa hiyo angekufa ndo basi,hakuna upelelezi tena...agh jamani mbona hawa watu wanajiabisha.
 
Baada ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kusikika wakidai vyombo vya usalama kutoka nje ya nchi vije kufanya uchunguzi wa shambulio la MbungeTundu Lissu, Msemaji mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbaas amefunguka na kuhoji




Dkt%20abbasi.jpg

watu wangapi wamekufa na wazungu hawakuja.

Kupitia ukurasa wake wa twitter Dkt. Abbas amehoji kwa kuandika "Waje wazungu? Wamekufa watu wangapi Kibiti hatukuita wazungu?Lakini hatujui pia hata hao wazungu kwao makosa ya jinai pia yamewazidi nguvu?

Hata hivyo Dkt Abbas ameongeza kwamba tabia ya kutuhumiana kunapotokea kosa la jinai ambalo limetendwa kwa mtu yoyote au mwanasiasa siyo vizuri kwani kufanya hivyo kunakufanya uwe mshukiwa namba moja wa tukio.

Ameongeza kwamba kwamba ni "busara vyombo vya dola vikaachwa vifanye kazi yake kwanza na siyo kutuhumu".

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kupitia viongozi wake wamekuwa wakitaka serikali iruhusu vyombo vya kimataifa waje nchini kufanya uchunguzi juu ya shambulio la Tundu Lissu aliyepigwa risasi na waru wasiojulikana Septemba 7 akiwa nje ya nyumba yake Area D' Dodoma alipokuwa akitokea bungeni mchana.

msemaji%20wa%20serikali....._0.JPG
Dah! Huyo Abbas naye ana phd? Kaazi kweli kweli. Anavyoongea lazima utilie mashaka hiyo elimu yake.
 
Wachunguzi huru? Tukumbushane, wachunguzi hawa hawa wa Bongo ndio walifuatilia kifo cha Chacha Wangwe. Leo Mbowe anawakataa... vipi?

Mbowe yupo kimewashinda nini kumfunga kwa kifo cha Wangwe? Safari hii mtatafuta mpaka propaganda za kwenye Archive lakini hamtoki. Mzalendo academia jicho limemtoka haamini kwamba picha limeharibika kiasi hiki. Hata wale waliokuwa wanaimbishwa uzalendo uchwara sasa hivi akigeuka watu wanamng'ong'a. Ni hofu tu ndio inawafanya watu wasifunguke. Lakini kwenye hadithi za hapa na pale kila mtu kaipata picha, hivyo mkiwaimbisha watu uzalendo uchwara wanawasanifu tu wanajua mna uchu wa madaraka. Na ile single ya miaka 7 ndio kabisa heshima imetoweka.
 
Kwakweli mnatutia mashaka hata sie tuliokuwa hatutaki muhusishwe na hili. Tutaanzaje kutoa kauli kuwakinga kwa mambo kama haya ya watu na PhD zenu kujikanyaga kama darasa la 5C?
 
Hawezi seme vingine Dr. Abbas kumuudhi boss wake acha atete ugali wake. Asante Mungu kuendelea kumtetea Lissu mkono wako tumeuona.
 
Wanaogopa kuumbuka maana jamaa wa Scotland Yard ama FSB wangegonga hadi Magogoni
Sasa it's official waliotaka kumuua Lisu ni hao wanao zuia uchunguzi huru

Hongereni kwa precedent nzuri mliyo iweka ya kuwapiga risasi mchana kweupe wanao wakosoa haita waacha salama

Lisu anapigwa risasi karibu na Bunge, Polisi, Makao makuu ya nchi halafu mpaka leo hamna aliye kamatwa mnaona jambo dogo sio?

Hivi pattern ya mauaji ya Kibiti ni sawa kabisa na hili la Lisu?
Mbona mnajidhalilisha kiasi hiki?

Hili la kuunganisha tukio la Lisu na Kibiti tayari mmeonyesha ulimbukeni mkubwa hata uchunguzi wa ndani hauna maana yoyote kwa kushindwa kutofautisha kitu kidogo hivi ndio mna weledi wa kuwachunguza watesi wa Lisu?

Kwa hiyo leo kiongozi wa nchi mkubwa akiuwawa tutasema mbona Kibiti wazungu hawakuja?

Majibu marahisi kwenye maswali magumu

Ninani aliyekataa uchunguzi huru kwa swala la Kibiti?

Mnara wa babeli unaanguka naona kila mtu ananena kwa lugha yake

Hofu zimewajaa Mungu anawaumbua tu

Get well soon Undisputed Tundu Lisu
 
Mkuu kama kusoma hujui,hata picha kuona huoni???

Na wanazidi kuthibitisha kuwa wahusika ni wenyewe kama mh.mbowe alivosema.
Sijui wanaogopa nini just kutoa tu kibali kuruhusu watu wafanye uchunguzi....think big.!!!!!!
 
Chezea washamba, si unajua hata smg kupiga ni shida japo ndio wanazotumia wakishindwa hoja?
Kwa hiyo majambazi na wanyang'anyi wote wanaoua au kujeruhi kwa kutumia silaha ikiwemo hiyo SMG uliyoitaja wanatumwa na serikali au vyombo vya usalama? Halafu nani kakuambia silaha iliyotumika kumshambulia Lissu ni SMG?
 
Ni wendawazimu kila mara kufanya reference ya Kibiti. Kibiti mauaji yalikuwa yanafanyika vijijini. Wauaji tuliambiwa walikuwa wanakimbilia kwenye msitu mnene. Kibiti hakuna mtu aliyelalamika kuwa alikuwa akiwindwa na watu wa usalama wa Taifa. Sasa mazingira hayo ni ya kulinganisha na ya Lisu.

Nosense. Sijui hawa watu huwa wanaokotwa wapi!
 
Back
Top Bottom