Serikali yafyeka mishahara ya watumishi

Serikali yafyeka mishahara ya watumishi

Great Thinkers,
Kuna malalamiko kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi wa serikali ya Tanzania kuhusu mishahara yao ya mwezi Juni 2025. Inaripotiwa kuwa baadhi ya watumishi wamekumbwa na makato yasiyoeleweka ya takribani asilimia 3% kutoka kwenye mishahara yao. Hali hii imezua taharuki na maswali mengi miongoni mwa watumishi wa umma.
Kwa dhati kabisa, poleni sana watumishi wa umma. Tunatambua mchango wenu mkubwa katika kuendesha shughuli za serikali na kutoa huduma muhimu kwa wananchi. Ni wazi kuwa kila senti inayokatwa ina athari kwa maisha ya kila siku, hasa kwa wale waliokuwa tayari wamepanga matumizi ya mishahara hiyo kwa uangalifu mkubwa.
Ni matumaini yetu kuwa mamlaka husika kama Hazina, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Ndani (CAG) watatoa ufafanuzi wa kina kuhusu makato haya:
  • Je, ni marekebisho ya kodi au michango ya hifadhi ya jamii?
  • Au ni makato ya marekebisho ya mfumo wa mishahara?
  • Je, kuna ucheleweshaji wa malipo ya baadhi ya posho au marupurupu?
Ni muhimu kwa serikali kuweka uwazi na kutoa taarifa mapema kwa watumishi wake, kwani mshahara wa mtumishi ni mtegemeo wa familia nyingi.

Kwa mara nyingine, poleni sana watumishi wa serikali. Tunaamini serikali itasikiliza kilio chenu na kuchukua hatua stahiki. Endeleeni kuwa wavumilivu huku tukisubiri ufafanuzi rasmi.
Kila senti inayozidi sh 500,000/= inastahili kukatwa kodi. FULL STOP.
 
Ngoja waangalie watakuja kwenye ule uzi ,mtu uko ughaibuni unaleta taarifa wakati wahusika wako kimya .
 
Inaripotiwa kuwa baadhi ya watumishi wamekumbwa na makato yasiyoeleweka ya takribani asilimia 3% kutoka kwenye mishahara yao.

Na bado wakienda mashine za ATM miamala yao inatozwa tozo hivyo mshahara halisi ni pungufu sana.

Mitano mingine kwa Mama, Oktoba wafanyakazi mtiki

N.B
No Reforms No Election 2025
 
Double Taxation katika mshahara wenu ?

1750603972862.png
 
Back
Top Bottom