Serikali yaanza rasmi Biashara ya kuuza mafuta nchini

Serikali yaanza rasmi Biashara ya kuuza mafuta nchini

Tukiwa na vituo vingi vya uuzaji wa mafuta manufa ni yetu walaji, naunga mkono hoja
 
Tukiwa na vituo vingi vya uuzaji wa mafuta manufa ni yetu walaji, naunga mkono hoja
 
vyanzo vya mapato kwa serikali vipo takribani vitatu na vipo kihalali kabisa I.e kodi,mikopo na misaada(grants).Serikali inapojiingiza directly kwenye business ni jambo ambalo halina afya kwa upande mmoja lakini nikiri kuwa faida ni kiduchu kwa last consumer.Serikali iweke mipango na mifumo mizuri ya kusimamia na kutengeneza mazingira mazuri kwa sekta binafsi ya ufanyaji biashara
Hapana.mimi naona ni jambo zuri.
Maana faida itaenda hazina..
waache kutegemea kodi.
Wawe na vyanzo vya mapato..
 
vyanzo vya mapato kwa serikali vipo takribani vitatu na vipo kihalali kabisa I.e kodi,mikopo na misaada(grants).Serikali inapojiingiza directly kwenye business ni jambo ambalo halina afya kwa upande mmoja lakini nikiri kuwa faida ni kiduchu kwa last consumer.Serikali iweke mipango na mifumo mizuri ya kusimamia na kutengeneza mazingira mazuri kwa sekta binafsi ya ufanyaji biashara
Unadhani ni kitu gani kitatokea kwa uchumi wa Tanzania kutokana na uwezo wetu wa kuhifadhi mafuta iwapo Iran ikifanikiwa kuzuia meli yoyote kukatiza strait of Hormuz kwa muda wa miezi mitatu tu?
 
Na sisi wa vijijini tusokuwa na vya moto watuletee maduka ya mitungi ya gesi na majiko yake kwa bei nafuu. Tumechoshwa kujitwisha mizigo ya kuni, kuharibiwa macho kwa moshi kishapo tutaepuka uharibifu wa mazingira, Biashara hii uwekezaji wake si mkubwa ki vile ukilinganisha na viituo vya mafuta. Inawezekana tena kwa muda mfupi. Kupanga ni kuchagua.
 
View attachment 1472096

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amezindua rasmi biashara ya kuuza na kusambaza mafuta nchini kwa kufungua kituo cha kwanza kuuza mafuta ya Petroli na Dizeli cha Serikali kitakachosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) kupitia Kampuni yake Tanzu ya Mafuta ( TANCOIL). Aidha Dkt. Kalemani alisema kuwa kuzinduliwa na kufunguliwa kwa biashara hiyo ni kutimiza azma na nia njema ya Serikali ya kuboresha shirika lake la TPDC,kuwapatia na kuwasogezea karibu wananchi wake huduma ya kupata mafuta yenye viwango vya ubora unaotakiwa, bei nafuu, na yatakayopatikana kwa wingi muda wote.

Dkt. Kalemani alifanya Uzinduzi huo pamoja na kufungua kituo hicho wilayani Musoma, mkoani Mara Juni 6, 2020, wakati wa ziara yake ya kikazi katika Mkoa huo, akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Zena Said pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Wizara hiyo na Taasisi zilizochini yake. Alisema baada ya kuanza rasmi kwa biashara hiyo, TPDC kupitia TANCOIL itashirikiana na Halmashauri zote nchini kuhakikisha inafanikisha azma ya Serikali ya kufungua na kuweka vituo vya kuuza na kusambaza mafuta katika kila halmashauri nchini pamoja na miundombinu ya kuhifadhi na kusafirisha mafuta.

Dkt. Kalemani aliwaeleza watanzania kuwa TPDC na TANOIL watashiriki katika biashara ya uagizaji na usambazaji mafuta kama zinavyofanya kampuni zingine za mafuta nchini ili kuongeza ushindani na kutanua wigo wa kampuni za kizalendo kushiriki katika biashara ya mafuta, ambayo kwa sasa inafanywa na makampuni kutoka nje ya nchi tu. Alisema kuwa serikali kupitia TPDC itajenga vituo 100 kwa kipindi cha miaka 5 ijayo, tayari baadhi ya Halmashauri zimeanza kutenga maeneo yatakayojengwa vituo hivyo: Aidha itahakikisha kuwa nusu ya mafuta yote yanayoingizwa nchini yanasimamiwa TPDC.
About time, ila bado viwanda kama Tanganyika Packers, Textiles, madini, vya kilimo n.k. Tutafika tu...
 
Nakubaliana na wewe lkn tatizo kubwa la baadhi ya makampuni yaliyo chini ya serikali ni kufanya kazi chini ya viwango ukilinganisha na makampuni ya sekta binafsi. Serikali inatakiwa kuyaacha makampuni haya kujiendesha yenyewe bila ya kuyaingilia ktk uendeshaji wake wa kila siku jambo la msingi yasimamiwe kwa karibu na yatengeneze faida na kuleta ushindani wa haki kwa walaji.
Kwenye biashara muhimu na nyeti kama umeme na nishati ya mafuta ni hatari ukategemea private companies kwa asilimia 100 na hasa kama kampuni hizo ni za nchi zingine. Tulishuhudia tulichokipata pale TANESCO na ATCL tulipowapa kampuni za Africa ya kusini na kadhalika. Tumeshuhudia licha ya bei ya mafuta ya petroli na dizeli kuteremka kwenye soko la dunia kwa sababu ya coronavirus kutoka USD 60 kwa pipa hadi USD 15 kwa pipa, sisi pamoja na EWURA yetu bei ya mafuta haya yalipungua kwa Tsh zisizozidi 100 tu kwa lita. Hii ni kwa sababu ya unyonyaji wa makampuni ya nje ya uagizaji na usambazaji wa mafuta haya hususani BP, Total, Camel etc. Sasa tutakuwa na TANOIL yetu wenyewe. Hatutaki kuchezewa chezewa tena.
 
Sio dalili nzuri uchumi kuendeshwa na mashirika ya umma, hapo awali tulishindwa, sasa tunatudia tena! Tutashindwa tena sababu kubwa ni usimamizi, kutakuwa na ufisadi, ubadhilifu, wizi,kuto wajibika hujuma.
Kwani sera ya serikali kutofanya biashara imeishia wapi?
 
Nafuu kwenye Monopoly? Unaijua Monopoly wewe?
Sioni vipi sekta binafsi inaweza shindana na serikali. Yale yale ya FastJet kujirudia.. but all in all kwetu walaji wa mwisho inaweza kuwa nafuu... let's wait and see
 
China yenyewe inamakampuni kibao ya serekal na Mambo yanaenda fresh tu
 
Tunajenga taifa hodhi la ajabu sana. Kupanga ni kuchagua, vituo vya mafuta ni pety buss kwa sasa wapo wajasiliamali wengi wadogo na wa kati. Endapo lipo swala la usalama bora serikali ingejipanga kuagiza bulk pekee.
Huna gari wewe ndio maana .........unapata wap ujasiri wa kuongea hakati huna gari
 
Hivi unajua kuwa SERIKALI ZA
1.uingereza
2.germany
3.saudia arabia n.k
Wana visima kabisa vya mafuta na makampuni ya mafuta unayajua haya?
vyanzo vya mapato kwa serikali vipo takribani vitatu na vipo kihalali kabisa I.e kodi,mikopo na misaada(grants).Serikali inapojiingiza directly kwenye business ni jambo ambalo halina afya kwa upande mmoja lakini nikiri kuwa faida ni kiduchu kwa last consumer.Serikali iweke mipango na mifumo mizuri ya kusimamia na kutengeneza mazingira mazuri kwa sekta binafsi ya ufanyaji biashara
 
Hawa jamaa hawashauriwi vizuri. Mtu akiamka na mke wake ana wazo flani basi linatekekezwa. Wanahisi sekta binafsi inafaidi sana.
 
Sio kweli labda haujui.
Nchi nyingi duniani Zina makampuni ya mafuta na visima pia.
Tena wanachimba wenyewe.au wanaingia mkataba na kampuni nyingine lakini faida wana gawana sawa au serikali inazidi.
Acheni kututisha.
Serikali nyingi za uarabuni zimetajirika kwa sababu ya biashara ya mafuta.
Ndo maana hata serikali zao hazitegemei sanaa KODI ZA WANANCHI.
Ni ujinga serikali kujiingiza kwenye vibiashara
 
Back
Top Bottom