Serikali ya Tanzania haithamini uhai wa raia wake. Watu wanauliwa na tembo mara kwa mara, familia zinaishia kupewa millioni 1

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,705
36,158
Baada ya kuweka juhudi za kuzuia ujangiri awamu ya Kikwete mpaka utawala wa Magufuli tembo waliongezeka sana kwenye pori la akiba la Selous na mapori mengine hapa nchini.

Juhudi za kuzuia na kupambana na ujangiri zinaendelea kuimarika hata Sasa. Tembo wameongezeka mara dufu. Wilaya ya Tunduru, Liwale na wilaya zingine za kusini tembo mpaka mjini wanafika. Wijijini Sasa wamekuwa kama mbuzi, wanazurura tu.

Watu wanakufa sana, hata leo kazikwa mjomba wangu huko Liwale Kijiji cha Mtawango kauliwa na tembo. Kwanini serikali isiwavune na kuuza nyama zao au hata kugawa Bure? Walaji tuko wengi mbona. Au iwauze nje, itangaze mnada kupunguza hili wimbi.

Miaka inaenda watu wanakufa, mazao yao yanaliwa na kuishia kupewa fidia za kiwendawazimu. Mtu auawe kwa uzembe wa serikali kisha familia yake muitulize kwa millioni 1. Hii ni sawa? Mbona mtu akikutwa na meno ya tembo anapigiwa thamani kubwa sana. Anafungwa m3ka mpaka 50 na faini juu?

Mtanzania maskini hana thamani kiasi hichi?
 
Kama tembo wanakuwa tishio kwa watu ni kuwatandika risasi tu wakafie mbali. Inaudhi sana mamlaka ya wanyamapori kushindwa kudhibiti wanyama wao wasilete madhara kwa binadamu. Kama ndio binadamu waliwafuata katika maeneo yao ya kutamba hapo ingeonekana binadamu ni wamewafuata huko porini na mbugani. Tembo wanazurura hovyo mpaka kwenye makazi ya watu, kwani askari wa wanyamapori wanafanya kazi gani?
 
Baada ya kuweka juhudi za kuzuia ujangiri awamu ya Kikwete mpaka utawala wa Magufuli tembo waliongezeka sana kwenye pori la akiba la Selous na mapori mengine hapa nchini.

Juhudi za kuzuia na kupambana na ujangiri zinaendelea kuimarika hata Sasa. Tembo wameongezeka mara dufu. Wilaya ya Tunduru, Liwale na wilaya zingine za kusini tembo mpaka mjini wanafika. Wijijini Sasa wamekuwa kama mbuzi, wanazurura tu.

Watu wanakufa sana, hata leo kazikwa mjomba wangu huko Liwale Kijiji cha Mtawango kauliwa na tembo. Kwanini serikali isiwavune na kuuza nyama zao au hata kugawa Bure? Walaji tuko wengi mbona. Au iwauze nje, itangaze mnada kupunguza hili wimbi.

Miaka inaenda watu wanakufa, mazao yao yanaliwa na kuishia kupewa fidia za kiwendawazimu. Mtu auawe kwa uzembe wa serikali kisha familia yake muitulize kwa millioni 1. Hii ni sawa? Mbona mtu akikutwa na meno ya tembo anapigiwa thamani kubwa sana. Anafungwa m3ka mpaka 50 na faini juu?

Mtanzania maskini hana thamani kiasi hichi?
Ukiua tembo utatozwa zaidi ya Shilingi 30 milioni. Tembo akikuua warithi wako hupewa hiyo milioni moja. Kwa hesabu hii tembo anathaminiwa zaidi kuliko binadamu.
 
Back
Top Bottom