Serikali ya Magufuli inatia shaka

Serikali ya Magufuli inatia shaka

rosemarie

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2011
Posts
6,887
Reaction score
3,439
Waziri wa elimu ameulizwa swali ni kwanini walimu wanadai hawajashirikishwa suala la elimu bure anapaniki.Jamani hawa watu wanajua wanachokifanya?

Suala la elimu bure ni mchakato unaotakiwa kujengewa msingi imara na ikiwezekana lipelekwe bungeni kutungiwa sheria,sasa pesa zinazotakiwa ni b30 lakini zimepelekwa b11.

Halafu kama ni kweli waalimu wanalalamika hawajashirikishwa, je hatuoni kama kuna tatizo hapa?

Nchi haiwezi kuedeshwa kienyeji au kibabe au kwa amri amri,suala la elimu bure ambalo ni Sera ya CHADEMA linahitaji kufanyiwa kazi na wadau wote wakiwemo walimu wahusishwe,huyu rais anaweza kutupeleka shimoni.
 
Wewe unaongea sera ya CHADEMA kwenye makaratasi wakati wengine wanaitenda kwa vitendo.

Kwani hao CHADEMA waliwashirikisha walimu kwenye kutunga hii unadai ni sera ya CHADEMA?.

Eti zinahitajika billion 30. Hizo billion 30 zinahitajika kwa siku au kwa saa?

Kama wewe ni mwelewa lazima utafamu kasoro haziwezi kukosekana kwa sababu sera hii ni mpya pamoja na kwamba ilikuwepo kwenye awamu ya kwanza ya uongozi nchini.

Feedback ya changamoto ndiyo itaifanya sera ikamilike kivitendo.

Hata software au machine zikitengenezwa kwa mara ya kwanza huwa zinakuwa na mapungufu ya hapa na pale.

Hata Kubenea anasema elimu yake niya hapa na pale!
 
magufuli alikuwa mwalimu mama magufuli mwalimu sasa nini zaidi wanachodai ambacho hata mama magufuli hajui
 
Waziri wa elimu ameulizwa swali ni kwanini walimu wanadai hawajashirikishwa suala la elimu bure anapaniki.Jamani hawa watu wanajua wanachokifanya?

Suala la elimu bure ni mchakato unaotakiwa kujengewa msingi imara na ikiwezekana lipelekwe bungeni kutungiwa sheria,sasa pesa zinazotakiwa ni b30 lakini zimepelekwa b11.

Halafu kama ni kweli waalimu wanalalamika hawajashirikishwa, je hatuoni kama kuna tatizo hapa?

Nchi haiwezi kuedeshwa kienyeji au kibabe au kwa amri amri,suala la elimu bure ambalo ni Sera ya CHADEMA linahitaji kufanyiwa kazi na wadau wote wakiwemo walimu wahusishwe,huyu rais anaweza kutupeleka shimoni.

Wewe binti umelewa kilevi gani? Magufuli ametokana na CCM na anatekeleza sera ya CCM. Kwa kukusaidia tu, hoja za CHADEMA wapelekee wenyewe CHADEMA ambao kwa siku kadhaa viongozi wakuu pamoja na wale wawekezaji wake wa ndani walikuwa Protea Machame (hotel ya Mbowe).
 
Mm naona haina haja ya kushirikisha waalimu coz hawagusi moja kwa moja kazi yao ni kufundisha tu.
 
Chadema asingekurupuka kupeleka bill. 11 wakati zinatakiwa 30 ndio maana tunasema Sera in mchakato wadau wahusishwe Chadema angewahusisha wadau akatengeneza Sheria akaipeleka bungeni sio kukurupuka Kwa CCM
 
JF katika ubora wake, hii nayo ni topic ya kujadili. Bure kabisa, imekaa kinafiki tu kutoka kwa wanaokula na kurambaramba peremende. You guys you need to grow up!
 
Walimu ni waajiriwa, na Mwajiri anataka huduma yake kwa wateja wake iwe bure, sasa hao walimu wanataka nini?
Kama Ualimu umewashinda wakafanye kazi nyingine. Wao wanatakiwa kupigania maslahi yao siyo kupinga elimu kutolewa bure.
 
Hivi Magufuli anaona shida gani kumteua Mh. Mbatia kushika wizara ya Elimu ili amsaidie mawazo kuhusu utekelezaji wa hii sera? Kipindi cha M.kwere wakajidai ku-copy katiba mpya ikawadodea mpaka Mkwe.re ameenda kwao hakuna cha katiba mpya. Huyu naye muda si mrefu atafungulia walimu kuchangisha fedha, wewe fikria shule inahitaji 650,000 kwa mwezi inapewa 250,000 wataweza wapi kujiendesha hawa? Elimu bure kwa CCM haiwezekani!!
 
Walimu wanataka washirikishwe wana mchango gani kwenye Sera ya kutoa elimu bure? Wanataka kuchangia gharama? Kazi yao ni kufundisha kama wanalipwa mshahara watulie wachape kazi.mambo ya kisera hayawahusu
 
Walimu wana hasira na deal zao za kuchangisha wazazi kukatizwa,

Mlolongo wa michango mfano.

Mafyekeo, madawati, rim moja ya karatasi, jembe, hela ya mlinzi, hela ya taaluma nk nk.

Sasa ukiwauliza watowe records za miaka iliyopita ikiwemo na sehemu vilipo vifaa vya akiba kwa mwaka uliopita inakuwa ubabaishaji tupu.
Na bado jipu la tuition kila wiki mtoto atadaiwa ikiambatana na hela ya kuchapishia mitihani wakati wao wa nakula deal la photocopy.

Hakika wewe Mleta Mada ulikuwa mnufaika wa mfumo tulioukataa wacheni tingatinga awatinge
 
Inawezekana kweli CDM wangeweza kutoa mchango mzuri kuhusu hoja ya elimu bure. Naomba wachangiaji mnisaidie kuelewa, CDM ipi tuiombe mchango wa mawazo yao hii ya Lowasa au iliyokufa ya Dr. Slaa. Kwa mtazamamo wangu hizi mbili zinatofautiana mno. Ni kama ninavyoliona Mawio na Mwanahalisi kabla na baada ya Ujio wa Lowasa CDM.
 
Inawezekana kweli CDM wangeweza kutoa mchango mzuri kuhusu hoja ya elimu bure. Naomba wachangiaji mnisaidie kuelewa, CDM ipi tuiombe mchango wa mawazo yao hii ya Lowasa au iliyokufa ya Dr. Slaa. Kwa mtazamamo wangu hizi mbili zinatofautiana mno. Ni kama ninavyoliona Mawio na Mwanahalisi kabla na baada ya Ujio wa Lowasa CDM.
UKWELI daima ni UKWELI, na wewe nimekukubali KWELI NI MKWELI, hata kubenea wa kabla ya Lowassa sio huyu wa sasa anayemuandama Zuberi zitto kabwe na kumuacha Freeman aikaeli Mbowe aliyetorosha mabilioni ya shilingi kwenda nje ya nchi kinyemela. 😀😱
 
Back
Top Bottom