Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Hivi sasa serikali ya CCM imekuja na mpango wake mpya uliobatizwa jina la kizungu la Big Results Now. Binafsi aliyeaanza kunifanya nitazame kwa macho mawili kuhusiana na mpango huu ni Waziri wa Nishati na Madini ambaye amekuwa kwa kiasi kikubwa kama mbunifu mwenyewe wa mpango huo.Mara kadhaa amekuwa akionekana akitoa matangazo ya wito huu wa Tanzania kuja na matokeo makubwa sasa.
Pengine wote kwa pamoja lazima tuulizane huu mpango wa matokeo makubwa sasa una maanisha nini.Mimi sijajua kabisa kuwa malengo makuu ya haya mambo ni nini, lakini nimebahatika kuona kile kinachoendelea katika idara ya elimu.Sijui idara zingine za serikali kama vile Nishati na Madini wao wamepanga kutuonesha nini, lakini niseme tu kama huko nako kuna mpango kama huu wa sekta ya elimu basi tumepotea kabisa katika kubuni matokeo makubwa sasa.
Labda niwashirikishe yanayoendelea sasa kwenye elimu ya sekondari.Baada ya mwaka huu serikali kupata aibu ya matokeo mabaya ya kidato cha nne 2012 na baada ya malalamiko mengi kutoka kwa wadau na wananchi wa kawaida juu ya matokeo hayo, serikali iliamua kubatilisha na kuja na matokeo mapya. Hivi sasa serikali imepanga kuondoa aibu hiyo katika mtihani ujao utakaofanyika Novemba 2013, japo haijatamka rasmi lakini kwa macho maangavu utaona ni kama wanataka kujinasua na aibu hiyo.
Serikali hivi sasa imewakusanya baadhi ya walimu wa masomo manne ya kidato cha nne kila wilaya na kila shule ya sekondari, na kuwapa semina elekezi juu umuhimu wa masomo hayo kufundishwa kwa umakini katika kipindi hiki kilichobaki kabla ya mtihani wa kidato cha nne Novemba 2013. Serikali inataka kuondoa aibu ya mwaka huu isijitokeze tena mwakani.Masomo hayo ni Hisabati, Sayansi(Physics and Chemistry) na Kiingereza. Katika masomo hayo zimechukuliwa mada nne ambazo walimu hawa wanafundishwa. Tukumbuke kuwa walimu hawa wanafundisha haya masomo mashuleni, lakini kwa mujibu wa waelekezi wanasema serikali imesisitiza topics hizo zilizopendekezwa , walimu wafundishwe tena.
Walimu hawa kila baada ya kumalizika kwa topics wanafanyishwa mtihani. Na kituko kikubwa ni kuwa wakufunzi wanasema wazi kuwa maswali ambayo yanaulizwa ndio hayo hayo wakawafundishe wanafunzi wao kwani ndio yatakayotoka kwenye mtihani wa mwisho Novemba 2013.Usisahau kuwa walimu pia katika siku hizi 5 wanazofundishwa wanalipwa posho ya siku shilingi 15,000/=.
Labda kuna mwerevu mwingine anaweza kuuliza kwanini masomo manne tu wakati ufaulu wa mwanafunzi unaanza na masomo 7. Jibu toka kwa wakufunzi ni hili kuwa haya masomo manne ndio yanayoongoza kwa kufelisha wanafunzi.Lakini pia kama mwanafunzi atafaulu masomo haya 4 basi idadi ya sifuri na daraja la nne zitapungua na hivyo kuongeza asilimia ya ufaulu badala ya kila mwaka kushuka.Lakini pia kuna jibu la ziada toka kwa wakufunzi ni kuwa mtu akifaulu somo la hesabu na Kiingereza basi mengine kama historian a civics anaweza kufaulu. Haya ndio matokeo makubwa sasa tunayoyasubiria mwakani. Je huu ndio mpango wa kuzalisha matokeo makubwa sasa?Je sekta zingine kam afya nako wamebuni nini?
Lakini la mwisho ambalo walimu wamepewa kama motisha ya kuipenda CCM baada ya mahusiano yao kudorora ni kuwa serikali imeamua kubadilisha madaraja ya walimu na kuwapandisha na kuwapa mshahara mkubwa.Anasema utafiti uliofanywa na serikali ni kuwa walimu wanaichukia sana CCM na serikali yake.Na hivyo wamemwaga sumu sana kwa wanafunzi pamoja na wanachi wengine.Hivyo kwa sasa imeamua kumalizana na walimu ili mwakani uchaguzi wa serikali za mitaa utoe big results pamoja na ule wa 2015.
Is this a big result now from big men and women? Shall we succeed with this strategy? Let us wait for it. Let me borrow words from Jenerali Ulimwengu as written in his Weekly Column in RaiaMwema tabloid, Where will Big Results come from without Big Ideas, which are born of Big thinking by Big Men and Women? Petty thinking never produced big results anywhere.
Pengine wote kwa pamoja lazima tuulizane huu mpango wa matokeo makubwa sasa una maanisha nini.Mimi sijajua kabisa kuwa malengo makuu ya haya mambo ni nini, lakini nimebahatika kuona kile kinachoendelea katika idara ya elimu.Sijui idara zingine za serikali kama vile Nishati na Madini wao wamepanga kutuonesha nini, lakini niseme tu kama huko nako kuna mpango kama huu wa sekta ya elimu basi tumepotea kabisa katika kubuni matokeo makubwa sasa.
Labda niwashirikishe yanayoendelea sasa kwenye elimu ya sekondari.Baada ya mwaka huu serikali kupata aibu ya matokeo mabaya ya kidato cha nne 2012 na baada ya malalamiko mengi kutoka kwa wadau na wananchi wa kawaida juu ya matokeo hayo, serikali iliamua kubatilisha na kuja na matokeo mapya. Hivi sasa serikali imepanga kuondoa aibu hiyo katika mtihani ujao utakaofanyika Novemba 2013, japo haijatamka rasmi lakini kwa macho maangavu utaona ni kama wanataka kujinasua na aibu hiyo.
Serikali hivi sasa imewakusanya baadhi ya walimu wa masomo manne ya kidato cha nne kila wilaya na kila shule ya sekondari, na kuwapa semina elekezi juu umuhimu wa masomo hayo kufundishwa kwa umakini katika kipindi hiki kilichobaki kabla ya mtihani wa kidato cha nne Novemba 2013. Serikali inataka kuondoa aibu ya mwaka huu isijitokeze tena mwakani.Masomo hayo ni Hisabati, Sayansi(Physics and Chemistry) na Kiingereza. Katika masomo hayo zimechukuliwa mada nne ambazo walimu hawa wanafundishwa. Tukumbuke kuwa walimu hawa wanafundisha haya masomo mashuleni, lakini kwa mujibu wa waelekezi wanasema serikali imesisitiza topics hizo zilizopendekezwa , walimu wafundishwe tena.
Walimu hawa kila baada ya kumalizika kwa topics wanafanyishwa mtihani. Na kituko kikubwa ni kuwa wakufunzi wanasema wazi kuwa maswali ambayo yanaulizwa ndio hayo hayo wakawafundishe wanafunzi wao kwani ndio yatakayotoka kwenye mtihani wa mwisho Novemba 2013.Usisahau kuwa walimu pia katika siku hizi 5 wanazofundishwa wanalipwa posho ya siku shilingi 15,000/=.
Labda kuna mwerevu mwingine anaweza kuuliza kwanini masomo manne tu wakati ufaulu wa mwanafunzi unaanza na masomo 7. Jibu toka kwa wakufunzi ni hili kuwa haya masomo manne ndio yanayoongoza kwa kufelisha wanafunzi.Lakini pia kama mwanafunzi atafaulu masomo haya 4 basi idadi ya sifuri na daraja la nne zitapungua na hivyo kuongeza asilimia ya ufaulu badala ya kila mwaka kushuka.Lakini pia kuna jibu la ziada toka kwa wakufunzi ni kuwa mtu akifaulu somo la hesabu na Kiingereza basi mengine kama historian a civics anaweza kufaulu. Haya ndio matokeo makubwa sasa tunayoyasubiria mwakani. Je huu ndio mpango wa kuzalisha matokeo makubwa sasa?Je sekta zingine kam afya nako wamebuni nini?
Lakini la mwisho ambalo walimu wamepewa kama motisha ya kuipenda CCM baada ya mahusiano yao kudorora ni kuwa serikali imeamua kubadilisha madaraja ya walimu na kuwapandisha na kuwapa mshahara mkubwa.Anasema utafiti uliofanywa na serikali ni kuwa walimu wanaichukia sana CCM na serikali yake.Na hivyo wamemwaga sumu sana kwa wanafunzi pamoja na wanachi wengine.Hivyo kwa sasa imeamua kumalizana na walimu ili mwakani uchaguzi wa serikali za mitaa utoe big results pamoja na ule wa 2015.
Is this a big result now from big men and women? Shall we succeed with this strategy? Let us wait for it. Let me borrow words from Jenerali Ulimwengu as written in his Weekly Column in RaiaMwema tabloid, Where will Big Results come from without Big Ideas, which are born of Big thinking by Big Men and Women? Petty thinking never produced big results anywhere.