Serikali tuwekeni wazi wakulima Juu ya ununuzi wa korosho"

Phd Hewa

JF-Expert Member
Oct 3, 2016
572
466
1475825759780.jpg

Kumekua na Sintofahamu Juu ya ununuzi wa korosho mwaka huu.

Kutokana na utaratibu wa ununuzi wa korosho inasemwa kwamba mkulima atakwenda kuuza korosho zake galani lakini pesa atakwenda kupokelea bank.

Kwa utaratibu huo maana yake mkulima atatakiwa afungue account ya bank.

Lakini wengi wamekua wakijiuliza maswali ikiwa unatakiwa kupokelea bank je yule wa kg 20
au kg 10 nae akafungue account au kuna utaratibu Mwingine juu ya malipo kwa mkulima ambae amepata mavuno madogo?

Kwani siyo wote ambao wanapata mavuno makubwa wengine kufeli kwa kukosa mazao ya kutosha kutokana na pembe jeo kuwa duni au hali ya hewa au ukata wa kifedha kutokana na kushindwa kuihudumia etc.

Pia kama utaratibu ndiyo huo mbona hatuoni elimu ikitolewa kwa wakulima?

Wengine wakaenda mbaaali na kusema tunapelekwa bank ili wakatukate kodi sina uhakika na hilo.

Lakini kwa hili la mkulima wa zao la korosho kutakiwa akapokelee bank tafadhali serikali tupeni ufafanuzi juu ya suala hili.
 
solution,akae na matajiri,amwambie mohamed dewji na wengine wamwambie watajenga kiwanda lini,cha kisasa cha korosho,hamna namna atawakwepa matajiri,ili kumlinda mkulima,vyama vya ushirika au serikali iweke hisa na iwe na members kwenye board watakaolinda maslahi ya umma.
 
solution,akae na matajiri,amwambie mohamed dewji na wengine wamwambie watajenga kiwanda lini,cha kisasa cha korosho,hamna namna atawakwepa matajiri,ili kumlinda mkulima,vyama vya ushirika au serikali iweke hisa na iwe na members kwenye board watakaolinda maslahi ya umma.
Wakulima wanahaha kwa utaratibu huu sababu wengine wanaishi mbali na mabenk.
Wakafikia kusema kama ni hivyo huo utararibu utawapa nafasi zaidi walanguzi mana mtu awezi kusafiri kilomita 20 au 30 kwa ajili ya kwenda bank kupokea sh 40000 au sh 20000.
 
solution,akae na matajiri,amwambie mohamed dewji na wengine wamwambie watajenga kiwanda lini,cha kisasa cha korosho,hamna namna atawakwepa matajiri,ili kumlinda mkulima,vyama vya ushirika au serikali iweke hisa na iwe na members kwenye board watakaolinda maslahi ya umma.
Safi
 
Sijui hii post kama utapata wachangiaji mana jamiiforums imetawaliwa na vijana wafia vyama bila kufuatilia na kuishawishi serikali juu ya maslahi ya mtu wa chini hasa mkulima

Ukitaka jamiiforums upate wachangiaji msifie mkuu au bwana yule.
 
Hii serikali imefilisika. Ni juzi tu hapa Jeshi la Polisi limemkamata mama mmoja aliyekutwa na beseni la visheti akibadilisha kwa korosho (kisheti kimoja korosho 20) huko Tandahimba mkoani Mtwara. Unaambiwa hali ni ngumu sana huko. Polisi wanazunguka vijijini kukamata wanaonunua korosho kienyeji wakiwemo wanaobadilisha bidhaa kwa korosho wakati wametangaza kufungua soko tangu tarehe 1 Septemba lakini hadi leo tarehe 7 Oktoba hakuna ghala lililofunguliwa tayari kwa ukusanyaji wa korosho za wakulima ili zipelekwe mnadani.
 
Hii serikali imefilisika. Ni juzi tu hapa Jeshi la Polisi limemkamata mama mmoja aliyekutwa na beseni la visheti akibadilisha kwa korosho (kisheti kimoja korosho 20) huko Tandahimba mkoani Mtwara. Unaambiwa hali ni ngumu sana huko. Polisi wanazunguka vijijini kukamata wanaonunua korosho kienyeji wakiwemo wanaobadilisha bidhaa kwa korosho wakati wametangaza kufungua soko tangu tarehe 1 Septemba lakini hadi leo tarehe 7 Oktoba hakuna ghala lililofunguliwa tayari kwa ukusanyaji wa korosho za wakulima ili zipelekwe mnadani.
Ni kweli ata huku kwetu bado hawajafungua maghala yani ni sheeda
 
Mfumo wa stakabadhi ghalani ulikuja bila elimu yoyote kwa mkulima na umefeli. Na huu mfumo wa malipo kupitia bank umeletwa bila ufafanuzi kwa mkulima na utafeli na kufa kibudu. Huu mfumo utawapa unafuu wakulima wakubwa ambao ni wachache na kuwatesa wakulima wadogo walio wengi. Waliobuni mtindo huu wachunguzwe haraka sana na huwenda wana ajenda ya siri kabisa. Hakuna msimu utashuhudiwa ulanguzi wa zao la korosho kama msimu huu ulioanza maeneo mengi. Matajiri wataweka kambi pembezoni mwa soko kusubiri wakulima wadogo wenye kilo 80 hadi 1000 ambaye hawezi kusubiri malipo ya bank. Waliobuni mfumo huu wana jambo wamelipanga na hawa matajiri.
 
Mikoa ya kusini upinzani unazidi kuimarika huku chama tawala kikichukua nafasi ya upinzani. Situation hii inatokana na serikali ya CCM kushindwa kulisimamia zao la korosho tangu ulipoanza mfumo wa Stakabadhi Mazao Ghalani mwaka 2008. Kila mwaka ni bla bla tu, huku target yao ikiwa kuwanyonya wakulima badala ya kuwaendeleza.
 
Mwaka huu ndugu zetu wamepata mapigo mawili. Kwanza ni kushuka kwa bei ya mbaazi, baadae ikashuka bei ya ufuta(the reverse is also true).Sasa kama na korosho itakosa soko la uhakika ni dhahma kwa wakulima!
 
solution,akae na matajiri,amwambie mohamed dewji na wengine wamwambie watajenga kiwanda lini,cha kisasa cha korosho,hamna namna atawakwepa matajiri,ili kumlinda mkulima,vyama vya ushirika au serikali iweke hisa na iwe na members kwenye board watakaolinda maslahi ya umma.
Interesting...
 
Wakulima wanahaha kwa utaratibu huu sababu wengine wanaishi mbali na mabenk.
Wakafikia kusema kama ni hivyo huo utararibu utawapa nafasi zaidi walanguzi mana mtu awezi kusafiri kilomita 20 au 30 kwa ajili ya kwenda bank kupokea sh 40000 au sh 20000.

Wanaotunga sheria sio wakulima wao wanakaa Dar na hawajui lolote kuhusu kilimo. Wanadhani kila mahaki ni kama Dar, na kwakuwa wanapata mishahara minono hata watoto wao wana account bank, hivyo wanajua kila mtanzania ana account bank. Wawakilishi wao wameambiwa wanaweza kuhama ccm.
 
Hii serikali imefilisika. Ni juzi tu hapa Jeshi la Polisi limemkamata mama mmoja aliyekutwa na beseni la visheti akibadilisha kwa korosho (kisheti kimoja korosho 20) huko Tandahimba mkoani Mtwara. Unaambiwa hali ni ngumu sana huko. Polisi wanazunguka vijijini kukamata wanaonunua korosho kienyeji wakiwemo wanaobadilisha bidhaa kwa korosho wakati wametangaza kufungua soko tangu tarehe 1 Septemba lakini hadi leo tarehe 7 Oktoba hakuna ghala lililofunguliwa tayari kwa ukusanyaji wa korosho za wakulima ili zipelekwe mnadani.
Mjiandae kukopwa tu!
 
Kisha kwenye hali kama hiyo unashangaa mbunge wa upinzani anahama anajiunga na ccm kuunga juhudi za rais, huku tatizo la msingi la wananchi tena toka ukanda wa waziri mkuu hakuna ufumbuzi wa jambo hili. Tukisema hao wanaosema wanaenda kuunga juhudi za rais wananunuliwa tunakosea?
 
Kisha kwenye hali kama hiyo unashangaa mbunge wa upinzani anahama anajiunga na ccm kuunga juhudi za rais, huku tatizo la msingi la wananchi tena toka ukanda wa waziri mkuu hakuna ufumbuzi wa jambo hili. Tukisema hao wanaosema wanaenda kuunga juhudi za rais wananunuliwa tunakosea?
Na haya huenda ndio madhara ya serikali kuchukua fedha za korosho.
 
Back
Top Bottom