Serikali tunaomba mruhusu uhamisho wa watumishi

bampami

JF-Expert Member
Nov 5, 2011
5,697
4,107
Wawenzangu,
Kwa sisi watumishi wa serikali, tumekuwa tukisubiri ruhusa ya uhamisho wa watumishi bila mafanikio, kiukweli kukaa mbali na familia ni jaribu lingine katika maisha, kwani:

1.Gharama za maisha zinakuwa juu kutokana na matumizi kuongezeka.

2.Mkikaa mbali kuna uwezekano mkubwa wa kuleta migogoro katika ndoa hasa ya kimahusiano na kimapenzi (ndivyo hali ilivyo sasa)

3. Familia kukosa huduma za wazazi wote wawili.

Na mambo mengi yafananayo na hayo.

Serikali tunaomba sasa mruhusu uhamisho wa watumishi ukizingatia kuwa vyeti vya ndoa tunavyo sidhani kama inaweza kuleta shida au ujanja ujanja.

Naamini ujumbe utawafikia, na mtalifanyia kazi.

Ahsante!!
 
kwa vile wanasiasa hawajui tabu tunayopata na wenzi wetu kuw mbali
Ni kweli kabisa ndugu yangu, mishahara yenyewe ndo hiyo then mnakuwa mbali halafu, migogoro kila siku, uaminifu katika ndoa unapungua, malezi ya watoto bila mzazi mmoja pia ni changamoto. Bora mmoja Mungu awe amemchukua kwa kweli.
 
Wawenzangu,
Kwa sisi watumishi wa serikali, tumekuwa tukisubiri ruhusa ya uhamisho wa watumishi bila mafanikio, kiukweli kukaa mbali na familia ni jaribu lingine katika maisha, kwani:

1.Gharama za maisha zinakuwa juu kutokana na matumizi kuongezeka.

2.Mkikaa mbali kuna uwezekano mkubwa wa kuleta migogoro katika ndoa hasa ya kimahusiano na kimapenzi (ndivyo hali ilivyo sasa)

3. Familia kukosa huduma za wazazi wote wawili.

Na mambo mengi yafananayo na hayo.

Serikali tunaomba sasa mruhusu uhamisho wa watumishi ukizingatia kuwa vyeti vya ndoa tunavyo sidhani kama inaweza kuleta shida au ujanja ujanja.

Naamini ujumbe utawafikia, na mtalifanyia kazi.

Ahsante!!
Kwanini wamezuia?
 
Ni kweli kabisa ndugu yangu, mishahara yenyewe ndo hiyo then mnakuwa mbali halafu, migogoro kila siku, uaminifu katika ndoa unapungua, malezi ya watoto bila mzazi mmoja pia ni changamoto. Bora mmoja Mungu awe amemchukua kwa kweli.
Daaah umeandika kwa unyonge Sana,pole mkuu.



Sintowaangusha
 
Kwanini wamezuia?
Wanasema wanaweka system kwenye kila computer ya serikali ili kila mtumishi aombe online. Sasa ukiangalia mpaka waweke hiyo system ni lini, fedha zitoke, zipitishwe, mchakato uanze tena tanzania yote hiyo si 2025? Ndicho kituumizacho hicho.
 
Back
Top Bottom