Rais, najua huamini kama maisha ni magumu labda kwa sababu wewe una kila kitu, hujawahi kukosa hela ya kuilisha familia yako, mbaya zaidi wanaokuzunguka hawakuambii ukweli, pengine nao kwa sababu nao wana kila kitu kama wewe.
Ukweli ni kwamba maisha ni magumu sana iwe kwa wasomi waliokosa ajira na kwa Watanzania wengine. Ndugu Rais ajira hakuna, basi turudishie fao la kujitoa tupate hela zetu tujiajiri.
Tunakosa hata hela ya kulisha Familia zetu wakati hela tunazo ila zimeshikiliwa na hii mifuko. Hivi huoni kama ni uonevu kutuacha tuteseke kwa njaa wakati kuna mamilioni yetu yameshikiliwa kimabavu?
Rais tunaomba hela zetu tuweze kujiajiri maana ajira hakuna.
Siku zote umekuwa ukijipambanua wewe ni rais wa wanyonge, wanyonge turudishie fao la kujitoa.
Ukweli ni kwamba maisha ni magumu sana iwe kwa wasomi waliokosa ajira na kwa Watanzania wengine. Ndugu Rais ajira hakuna, basi turudishie fao la kujitoa tupate hela zetu tujiajiri.
Tunakosa hata hela ya kulisha Familia zetu wakati hela tunazo ila zimeshikiliwa na hii mifuko. Hivi huoni kama ni uonevu kutuacha tuteseke kwa njaa wakati kuna mamilioni yetu yameshikiliwa kimabavu?
Rais tunaomba hela zetu tuweze kujiajiri maana ajira hakuna.
Siku zote umekuwa ukijipambanua wewe ni rais wa wanyonge, wanyonge turudishie fao la kujitoa.