Serikali mnawanyonga Walimu!

Serikali mnawanyonga Walimu!

Malimu mnachangia CWT ili wale heal zenu,kwani kwa hli tatizo lenu hicho chama chenu kikowapi....?
Mnapenda kuliwa sn ,(akili yakuzaliwa.........)
 
Kwanza ni ufinyi wa fikra kwa viongozi wetu, mwalimu kazi yake ni kufundisha siyo kujenga maabara. Kama serikali inaona kuna haja ya watumishi kuchangia basi wawe watumishi wote siyo kuwabana walimu peke yake ilihali hizo maabara zinatumika na wananchi wote. Lakini kuna sababu kwa nini serikali haiwakati watumishi waengine isipokuwa walimu kwa sababu walimu wengi hawajitambui wanageukana wenyewe kwa wenyewe hawana msimamo wa kushughulikia matatizo yao wenyewe kwa umoja hivyo mimi nanukuu kauli ya Pinda kuwa wakatwe tu hadi siku wakijitambua
 
Agizo limetoka kwa mkuu wa kaya!
Kikinuka anawakacha kiaina
 
Hapo sasa! Yani walimu ni shidaaa!! Wako wengi nchi nzima lakini maamuzi hawafanyi! Walimu we need changes amkeni!

Tatizo kwetu huku wengi hasa wa zamani vyeti vya kufoji ndo maana waoga
mi nakwambia ngoja kizazi cha upe kiishe halafu sie tulionza kazi na vyeti halali tutawaonyesha tu
nyie madhulumati mi sikwati sh.kumi mbuzi nyieeeeeeee
nimesoma kwa hela ya baba angu
km kukatwa wakateni viongozi wenu huko juu
walimu tuacheni ujinga tupambane
mwakani mwl atakayeenda kuomba kuandikisha wapiga kura ntamsikitika sana
tuacheni njaaaa za ajabu ajabu
wanasiasa wanatutumia km kondomu tu
 
Wakishachanga hvyo kodi hawalipi?? Kama wanakatwa hvyo na kodi wanalipa basi huo utakuwa uzezeta
 
huu ni uonevu mkubwa sana kwa nini mkate mshahara wa mtumishi bila ithini yake?na mbona hamkukata za wabunge wa bunge la katiba na bunge la jamhuri?nasema tena huu ni uonevu wa hali ya juu na iko siku itakuwa ni mwisho
 
Wakishachanga hvyo kodi hawalipi?? Kama wanakatwa hvyo na kodi wanalipa basi huo utakuwa uzezeta

Hahahaha!! Hawa walimu tuwaombee!! Wale wa upe wakiisha naamini walimu watatukomboa
 
Mwalimu Kaijage badala ya kugombania hela za walimu wenziwe zinazokatwa pasipo kujua, yeye anagomaba na UKAWA. Shem on you Mwalimu Kaijage
 
CWT Hawana lolote wanakula pesa za walimu bure nakujilimbikizia mali tena kama ni ufisadi uko CWT. wanaopaswa kwenda mahakani ni CWT na wala siyo mwalimu aliyelia upo hapo ndugu! Walimu amkeni

lakin suala la kukatwa mishahara labda walimu wa mikoani hao,yaan umkate mwalim mshahara kwa mchango wa maabara,,,,,labda kama wanalazimishwa kuchanga na walim wengi mpaka sasa 'wamegoma' kuchanga
 
Wakishachanga hvyo kodi hawalipi?? Kama wanakatwa hvyo na kodi wanalipa basi huo utakuwa uzezeta

kama kuna mwalimu ameridhia KUKATWA HUO MCHANGO KWENYE SALARY SLIP YAKE NTAMUONA HANA MAANA,ME NACHOJUA TANGAZO LILISEMA WALIM 'MCHANGO' UNAWAHUSU ILA NI HIYARI BINAFS MPAKA SASA SIJATOA TENA NI SH 6000-1000 TU ILA SIJATOA,MAANA SIWEZ KUICHANGIA TENA SERIKALI
 
Ngugu! Ni hatariii!! Ungeona jana mama mmoja (mwalimu) alipokuwa akipaza sauti akitoa machozi ungelia ndugu! Tuwe na busara katika kufanya maamuzi hii ni nchi yetu sote tusikubali hata kidogo.

Hawa hawa walimu huwa wakipewa viposho vya kijinga wanashiriki katika kukakaa kimya CCM wakiiba kura wakati wa uchaguzi. Acha wakatwe , sio walishaambiwa ni mazoba...
 
Hawa hawa walimu huwa wakipewa viposho vya kijinga wanashiriki katika kukakaa kimya CCM wakiiba kura wakati wa uchaguzi. Acha wakatwe , sio walishaambiwa ni mazoba...

Dah! Kumbe walimu ni shidaaaa! Ngoja tusubiri waje wakanushe.
 
Kwa nini walimu wasiende mahakamani?
Au ndo uoga wao kama kawaida?
 
Acha wakatwe hata hiyo hela ni kidogo sana, walimu wengi ni wajinga ukubali au ukatae habari ndio hiyo kwani na mimi nilikua mwalimu kwa miaka miwili nilijionea mwenyewe ujunga wa walimu japo wamesomea lakini usomi wao walio wengi ni bure, kwanza hawajiamini hata kidogo hata mfagiaji wa ofisi ya mkurugenzi anawatisha mpaka wanapiga magoti walimu wenye degree zao. Kuwa mwalimu inakubidi uwe mjinga wa kupitiliza vinginevyo kazi itakushinda kama sisi tulivyoamua kuacha kazi tukaja mtaani ku burn CD. Ualimu ndio kazi ya mwisho kabisa ambayo kila mtumishi anajifunzia kutoa makaripio na kupiga biti. Acha walimu wakome kwanza ndio siku moja watajua nini maaana kuikataa CCM
Mkuu nimecheka sana aiseee
 
Acha wakatwe, wanafki sana. Walianzisha migomo ya kudahi stahiki zao matokeo yake wengine waligoma wengine waliendelea na kazi.
 
Acha wakatwe, wanafki sana. Walianzisha migomo ya kudahi stahiki zao matokeo yake wengine waligoma wengine waliendelea na kazi.

Hahahahaha!! Leo mmewaamkia walimu wangu yani unapendeza sana wanapata ujumbe mzito sana hapo! Walimu wa primary wanawaangusha walimu secondary. Muda ukifika kitaeleweka tu.
 
Kwa nini walimu wasiende mahakamani?
Au ndo uoga wao kama kawaida?

Kwa bahati mbaya hawezi kwenda mmojammoja wao wanachama chao ndicho kifanye hivyo! Ngoja tusubirie tamko la rais wa CWT maana naye mwoga sana! Anakula pesa za walimu bure tu.
 
Vp TBC walirusha hiyo habari,teh teh teh!
 
Back
Top Bottom