Serikali kutumia nguvu ikibidi suala la gesi Mtwara

Niliangalia hicho kipindi dakika 45,haya uliyoyaandika sikuyasikia,labda itoe youtube utuletee hapa.
 
Polisi wenyewe ndio hawa wanaoshindwa nguvu na madereva wa bodaboda?

JWTZ hawawezi kutumika katika kazi za kipuuzi kama anavyodhani simbachawene. General Davis Mwamunyange hawezi kuwakosea adabu watanzania kiasi hicho cha kuwageuza wanajeshi kuwa polisi wa IGP Mwema.

the Hague inawasubiria kwa hamu! Waanzd hata leo!
 
hivi kikwete huwa anaokota wapi mawaziri wajinga kiasi kama hiki? sikutegemea kama simbachawene angeongea kitu kama hicho na elimu yake kweli elimu haisaidii kabisa
 
Nani kawaambia matumizi ya nguvu yanaleta suluhu,Tz kunajesh km la Islael?amakwel sikio la kufa...
 
kwani hao wanajeshi na polisi siyo wana Mtwara au watanzania bali ni mali ya mafisadi? kama ni watanzania hawatakuwa tayari kuwaua ndugu zao kwa kulinda upuuzi wa mafisadi watawala. Tazama Libya, Misri, Tunisia -kote huko kulikuwa na jeshi na polisi tena wenye maslahi na vifaa bora zaidi kuliko wa hapa kwetu -lakini waligeuka mara moja na kuunga mkono wananchi-Wasidhani tena kuwa wanajeshi na polisi wetu hawajui hali ya hewa ilivyo- Wanajua na hawatakuwa tayari kuua ndugu zao kwa ajili ya kulinda wapuuzi. labda wawe mbumbumbu kama wanajeshi wa Syria wanaomlinda mhuni wakaua ndugu zao:shut-mouth:
 
Wakuu nilishituka sana jana wakati wa kipindi kinachotumika kuwajenga viongozi mbali mbali wa serikali na CCM (dakika 45), mara hii kikimhusisha waziri Simbachaene. Akiongea kwa kujiamini waziri alidai kuwa "serikali ina polisi na JW hivyo ina uwezo wa kuvitumia vyombo hivyo kuhakikisha bomba linajengwa, lakini hatutaki tufike huko." Mtazamo wangu: kama serikali imeamua kuwa vyovyote vile bomba lazima lijengwe, basi kuna kitu kinafichwa nyuma ya mradi huu.
kunawenzao wengine watawala waliwaita wananchi mapanya wakasema wana polisi na jeshi wakaishia kuchomekwa majiti kusikotakiwa haya maCCM yasije yakadhani hata siku moja ya juu ya wananchi kauli zao za kuudhi kweli no wondoer walimkibiza puta kama ana polisi na jeshi kitu ganikilimfanya anywee alipokuwa huko amwambia Kinana,Ridhiwani na shemeji yake warudishe ten percent za watu mradi kuja Dar ni pale wanamtwara atakapojua faida yao
 
Nguvu ya hatari zaidi duniani ni nguvu ya umma. Historia imeonesha hivyo. Waziri kulopoka kuwa itatumia polisi na JW anahuhakika gani kama hakuna hata polisi mmoja au JW mmoja anayetoka kusini au mwenye mtazamo sawa na wanakusini. By the way Simbachawene is very junior minister hatuwezi kumchukulia serious. Mtu mzito aliyetoa kauli so far ni Mh. Kinana aliyesema kuna haja ya serikali kukaa chini na wanamtwara. Mpaka kinana atamke hivyo ujue hizo option za nguvu zilishakuwa nullfied kama option.
 
nilimsikia jana ndo nkasema hii serikali kweli inaombwe la uongozi, hivi kweli JK kakosa kabisa mawaziri wenye japo busara hata kidogo tu? eti anasema mtwara yote hakuna msomi hata mmoja, is it kweli? ndo sababu ya kuwachukulia gesi yao na kutowapa maendeleo au?? simbachawene ana jeuri ya kizamani kweli aisee...
Kwa hiyo hata wabunge wa huko siyo wasomi,Je mama yetu Kate Kamba, akina Beda Amuli Eng huyu na wamiliki wa Masasi siyo wasomi wa kaliba nzuri tu?.Simbachawene wakati anateuliwa kuwa WaZIRI nilisema wazi kuwa huyu hafai ni very corrupt to amazing level,tangu akiwa Mjumbe kamati ya LAAC chini ya Mgana Msindai na wenzake akina Chitalilo, zubeina Mhita ni wala rushwa hatari na katika kufuatilia miradi ya Council walikuwa wanalazimisha Wakurugenzi wawape fedha ,yeye akiwa ndiye engineer wa syindicate zote hafai kabisa hata kidogo na elimu za kuungaunga tu.Kauli yake hiyo ni upumbavu kabisa
 
ubabe wa serikali hauna nafasi. let say hilo bomba likijengwa huku JWTZ imesimamia ulinzi then baada ya ujenzi wataendelea kulilinda milele? hata kama watalilinda wataweza kuwapanga askari katika hilo bomba kutoka Mtwara hadi Dar? nimewahi kusikia kuwa gharama za ujenzi wa bomba hilo ziliongezwa kwa makusudi na wazito wakapata 10% zao. huenda ndio maana kwa gharama yoyote hata ya damu wanataka hilo bomba lijengwe!
 
mnakumbuka makaburi ya 'kiyeyeu' kule iringa,bara2 haikupita wala nyaya za umeme,mpaka serikali ilibidi ikaitafute ule ukoo/familia wakae chini wawaombe....ss ambao hamwamini bibi shauri yenu!
 
ubabe wa serikali hauna nafasi. let say hilo bomba likijengwa huku JWTZ imesimamia ulinzi then baada ya ujenzi wataendelea kulilinda milele? hata kama watalilinda wataweza kuwapanga askari katika hilo bomba kutoka Mtwara hadi Dar? nimewahi kusikia kuwa gharama za ujenzi wa bomba hilo ziliongezwa kwa makusudi na wazito wakapata 10% zao. huenda ndio maana kwa gharama yoyote hata ya damu wanataka hilo bomba lijengwe!

Waache wajenge kwa ubabe,halafu waone kitakachofika km ni gas au maji chumvi
 
Kuna mtu aliandika habari hapa jf akatabiri kikwete hatomaliza kipindi chake cha 2 sikuwahi kuamini, lakini kama watatumia nguvu nina hakika kikwete hatomaliza kipindi hiki cha pili na kama atamaliza basi lazima ataungana na charles wa liberia jela
 
Usiogope mkuu, ndo uvundo wa viongozi tulikuwa nao. Hawana utashi wa uongozi, busara hata kidogo na sifa za kuongoza. akili zao ndo ziko hivyoo, na ni lazima wateteee % zao za huo mkataba. Lakini uzuri ni kwamba mwisho wao ni 2015 na lazima washitakiwe
 
just this piece of words in case:
"Problems of the 21st century need brains and not guns and bullets."
 
Kuna mtu aliandika habari hapa jf akatabiri kikwete hatomaliza kipindi chake cha 2 sikuwahi kuamini, lakini kama watatumia nguvu nina hakika kikwete hatomaliza kipindi hiki cha pili na kama atamaliza basi lazima ataungana na charles wa liberia jela
kwa hali ilipofikia hilo linawezekana. serikali isiwalaumu viongozi wa vyama vya upinzani, wanaharakati au wananchi. uasi katika nchi hii unaasisiwa na serikali yenyewe kwa kuwapuuza wananchi. kama imefikia hatua kwamba wananchi hawaiogopi mabomu ya machozi wala risasi then tunaelekea kuwa like Tunisia na Libya!
 
Back
Top Bottom