serikali itunge sheria juu ya mitaro iliyoko mitaani.

astranaut

JF-Expert Member
Jul 30, 2018
1,276
1,021
Wananchi wenyewe tunachangia miundombinu ya serikali kuharibika,mfano mvua zinapokua zinanyesha wananchi wamekua na tabia ya kumiminia taka taka kwenye mitaro eti isombwe na maji,kitu kinacho changia mitaro na makaruvati kuziba.Hivyo pengine kupelekea mafuriko yasiyo na ulazima kwa watu waishio mabondeni,lakini pia barabara zingine hua zinaharibiwa na haya maji yanayo chepuka kutokana na mitaro na makaruvati kuziba.

Hivyo basi mimi nashauri serikali itunge sheria kali kwa yeyote ambae katika eneo la uwanja wake,nyumba yake,eneo la kazi aidha kibanda,duka n,k kukikutwa mtaro umejaa takataka,karuvati limeziba,au mtaro haujasafishwa kwa muda sahihi basi achukuliwe hatua kali za kisheria.Yani hiyo iwe ni lazima kila mwananchi kusafisha eneo la mtaro wake na kuhakikisha mtaro haujai mchanga ambao utapelekea kizuizi maji kupita.Ni wajibu wetu kuitunza miundombinu iliyopo.
 
Wananchi wenyewe tunachangia miundombinu ya serikali kuharibika,mfano mvua zinapokua zinanyesha wananchi wamekua na tabia ya kumiminia taka taka kwenye mitaro eti isombwe na maji,kitu kinacho changia mitaro na makaruvati kuziba.Hivyo pengine kupelekea mafuriko yasiyo na ulazima kwa watu waishio mabondeni,lakini pia barabara zingine hua zinaharibiwa na haya maji yanayo chepuka kutokana na mitaro na makaruvati kuziba.

Hivyo basi mimi nashauri serikali itunge sheria kali kwa yeyote ambae katika eneo la uwanja wake,nyumba yake,eneo la kazi aidha kibanda,duka n,k kukikutwa mtaro umejaa takataka,karuvati limeziba,au mtaro haujasafishwa kwa muda sahihi basi achukuliwe hatua kali za kisheria.Yani hiyo iwe ni lazima kila mwananchi kusafisha eneo la mtaro wake na kuhakikisha mtaro haujai mchanga ambao utapelekea kizuizi maji kupita.Ni wajibu wetu kuitunza miundombinu iliyopo.
Ilo ni swala manispa husika,

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
Kwanini magari ya takataka hayafiki mtaani?

Maana mpaka watu wanatupa taka kienyeji inamaana hakuna mfumo rasmi wa kusoma takataka au siyo?!

Watu wanalipa kodi za Majengo mojawapo ya manufaa inapaswa kuwepo kwa huduma kama vile za maji taka , huduma za mitaro na mifereji n.k


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jukumu la kutoa takataka kimsingi ni la Halmashauri.

Kabla ya kuweka sheria waweke kwanza utaratibu wa kuchukua hizo taka.
Kwamba atakaeenda kinyume na utaratibu ndipo sheria ichukue mkondo wake.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom